Teknolojia; neno linalotokana na maneno mawili ya Kigiriki -- technología (τεχνολογία😉 - téchnē (τέχνη😉, ufundi, "skill" or "craft" na -logía (-λογία😉, elimu au mafunzo kuhusu kitu fulani, tawi la elimu (ufahamu?).
Kama alivyosema mkuu redSilverdawg, ni vigumu sana kujadili teknolojia kama teknolojia. Ni lazima uwe specific kiasi, sababu kuna teknlojia mbalimbali k.v. teknolojia ya elimu, teknolojia ya ujenzi, teknolojia ya kompyuta n.k.
Ukianza kuiangalia teknolojia utagundua hata ugunduzi wa zana za mawe, moto na hata mavazi na makazi ni teknolojia. Ila matumizi ya neno 'teknolojia' yalianza kubadilika kwenye karne ya 20. Hapo ndipo matumizi ya ya neno hili ndipo yalipoanzan kutumika kwa maana ambayo ipo hata sasa.
Kwamba, teknolojia ni 'matumizi ya vitendo ya ujuzi (elimu, ufahamu wa jambo) katika eneo fulani'. Mara nyingi ni 'matumizi' ya ufahamu wa kisayansi.