mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,663
- 18,036
Tunashukuru TCU hatimaye wametoa majina ya waombaji waliochaguliwa kwenye chuo zaidi ya kimoja na wahusika wanatakiwa wa-confirm chuo wanachokitaka. Tatizo ni kuwa hawajaainisha kozi alizochaguliwa kwenye kila chuo maana mwombaji alikuwa anaomba zaidi ya kozi moja kwenye kila chuo. Kwa taarifa ya TCU waombaji bado hawajajua wamechaguliwa kozi zipi. Cha maana zaidi ni aina ya kozi wala siyo chuo maana chuo utakiacha lakini kozi ndiyo itakayohusika na maisha yako. Haiwezekani mtu aka-confirm chuo wakati hajui ni kozi ipi amechaguliwa huko kati ya zote alizozichagua. TCU fanyieni update taarifa yenu ili iainishe kozi pia aliyopata kwenye kila chuo alichochaguliwa.