TCU ongezeni muda wa udahili wengi watakosa vyuo

Pendo Julliet

JF-Expert Member
Sep 15, 2017
243
324
Takwimu za TCU zinaonesha hadi sasa wengi waliofanya application kwa awamu ya kwanza wamekosa vyuo.

Kati ya waombaji 180,640 majina kutoka vyuoni yalitumwa TCU na TCU inaeleza kutokana na kasoro nyingi yalihakikiwa na kupunguzwa hadi 77,756.

Waliochaguliwa na vyuo ni 44,627 tu hii sawa na 57.4% ya waombaji wote.

Waombaji 33,129 waliosalia sawa na 42.6% hawakuchakuguliwa na vyuo kutokana na ushindani au kukosa sifa katika programu walizoomba.
Hadi sasa kati waombaji 44,627 ambao wamechaguliwa na vyuo waombaji 38,831 tu ndiyo wanaoeza kujiunga na vyuo direct ukiacha zile kasoro za multiple selection nk.

Sasa Tume inaeleza imefungua tena maombi kwa awamu ya pili kuanzia tarehe 4 hadi 10 Oktoba 2017 ili kuruhusu walochaguliwa chuo zaidi ya kimoja kutaarifu chuo husika, waombaji walokosa nafasi kwenye awamu ya kwanza kwa ushindani au kukosa sifa katika programu walizoomba na wengine wote waloshindwa kuomba katika awamu ya kwanza waombe awamu hii ya pili yani kuanzia tarehe 4 hadi 10 Oktoba 2017.

Kutokana na ugumu wa zoezi hili la uombaji wanaokumbana nao waombaji hawa kwa sababu ambazo ni za mifumo ile wanayotumia kuomba kuwa unstable[hili siyo kosa la waombaji] muda huu wa siku 6 ni mfupi na hautoshi.

Ni heri sana TCU walione hili na waongeze muda zaidi ya tarehe 10 Oktoba ili wengi wakamilishe zoezi la uombaji ili kuepuka wengi kukosa vyuo na kukatisha ndoto zao za kupata elimu ya chuo ambayo ni haki ya kila Mtanzania mwenye sifa na vigezo vya kujiunga na kusoma chuo.

Nimeona vijana wengi wanahangaika na wengine wanaanza kukata tamaa sababu tu wanaona hawatendewi haki hali vigezo vya kujiunga na chuo wanavyo.

TCU kazi kwenu.
 
Vyuo tuu...watu tunatokwa povuu namna hii he mkopo ..!!! Ni kilio na kusaga meno
 
bora nipate chuo mkopo baadae maana mzaz atajibana utaomba mchango kwa mtu atakusaidia utaomba kwenye ngo bt chuo utaomba wapi? hapo unaanza mwakan hivi hawa wakuu wa tcu walisomea hapa hapa tanzania au nje ya tz ila ndo sifa za watanzania ukishapata kitu unamsahau mwingine ndo maana tunaangaika tu kama wafa maji
 
Yani tunaishi kama ndege tu ni bora mtu upate chuo mkopo utajua huko mbele ya safari kuliko ukose chuo mkopo pia nahisi utaleta kelele hizihizi za vyuo.
Mikopo italiza wengi zaidi ya mwaka ulopita.
Jamaa hawataki watu waelimike kwa makusudi kabisa.
 
Takwimu za TCU zinaonesha hadi sasa wengi waliofanya application kwa awamu ya kwanza wamekosa vyuo.

Kati ya waombaji 180,640 majina kutoka vyuoni yalitumwa TCU na TCU inaeleza kutokana na kasoro nyingi yalihakikiwa na kupunguzwa hadi 77,756.

Waliochaguliwa na vyuo ni 44,627 tu hii sawa na 57.4% ya waombaji wote.

Waombaji 33,129 waliosalia sawa na 42.6% hawakuchakuguliwa na vyuo kutokana na ushindani au kukosa sifa katika programu walizoomba.
Hadi sasa kati waombaji 44,627 ambao wamechaguliwa na vyuo waombaji 38,831 tu ndiyo wanaoeza kujiunga na vyuo direct ukiacha zile kasoro za multiple selection nk.

Sasa Tume inaeleza imefungua tena maombi kwa awamu ya pili kuanzia tarehe 4 hadi 10 Oktoba 2017 ili kuruhusu walochaguliwa chuo zaidi ya kimoja kutaarifu chuo husika, waombaji walokosa nafasi kwenye awamu ya kwanza kwa ushindani au kukosa sifa katika programu walizoomba na wengine wote waloshindwa kuomba katika awamu ya kwanza waombe awamu hii ya pili yani kuanzia tarehe 4 hadi 10 Oktoba 2017.

Kutokana na ugumu wa zoezi hili la uombaji wanaokumbana nao waombaji hawa kwa sababu ambazo ni za mifumo ile wanayotumia kuomba kuwa unstable[hili siyo kosa la waombaji] muda huu wa siku 6 ni mfupi na hautoshi.

Ni heri sana TCU walione hili na waongeze muda zaidi ya tarehe 10 Oktoba ili wengi wakamilishe zoezi la uombaji ili kuepuka wengi kukosa vyuo na kukatisha ndoto zao za kupata elimu ya chuo ambayo ni haki ya kila Mtanzania mwenye sifa na vigezo vya kujiunga na kusoma chuo.

Nimeona vijana wengi wanahangaika na wengine wanaanza kukata tamaa sababu tu wanaona hawatendewi haki hali vigezo vya kujiunga na chuo wanavyo.

TCU kazi kwenu.
Hivi kwanini TCU wanIngilia selection? Nilivyo fahamu mwanzo ni kwamba vyuo vinachagua na kuwaambia TCU tumechagua hawa.... Na kwamba nafasi zimejaa au bado tuna upungufu.
Pia nilicho jua ni kwamba minimum entry qualification ni 4points na siyo lazima minimum ziwe D mbili. Sasa kama una D moja na E mbili wanasema hustahili
 
TCU ndiyo wameharibu mchakato.Vyuo vingi vitapata wanafunzi wachache sana.Kwani wengi watakimbilia UDSM,MUHAS NA SUA/UDOM pekee Wengine ni kilio na kusaga meno.
 
Ni muda wa e-communication kufanya kazi, kwani kuna waombaji wengine wamechaguliwa na vyuo lakini, anaonekana yuko Chuo kingine ambacho alichaguliwa lakini hakuweza kwenda kwasababu mbalimbali,

anatakiwa aende Chuo alichochaguliwa mwanzo akapewe barua ya kuonyesha hakuripoti Chuo hicho, kisha aende TCU, apeleke barua hiyo na kujaza fomu ya re application ili selection ya Chuo alichopata iweze kuwa released na TCU ili apate fursa ya Ku confirm Chuo alichochaguliwa, kwahiyo you can see huo mzunguko ulivyo, na kulingana na time limit ya tar 4 hadi 10 na kuna siku mbili za tar 8 na 9 ni siku za mapumziko kwa hizi ofisi husika you can see how the time is too short,

that's why nikasema e-communication inabidi iwe faster and reliable ili waombaji wa vyuo waweze kufanikisha malengo yao, pamoja na vyuo vile vile na TCU na ku respond on time vigezo hivyo vinapokamilishwa, but so far TCU wanajitahidi kwenda na kasi ya mabadiliko, na siku zote mwanzo huwa ni mgumu, thanks.
 
Hivi kwanini TCU wanIngilia selection? Nilivyo fahamu mwanzo ni kwamba vyuo vinachagua na kuwaambia TCU tumechagua hawa.... Na kwamba nafasi zimejaa au bado tuna upungufu.
Pia nilicho jua ni kwamba minimum entry qualification ni 4points na siyo lazima minimum ziwe D mbili. Sasa kama una D moja na E mbili wanasema hustahili

TCU ndiyo wameharibu mchakato.Vyuo vingi vitapata wanafunzi wachache sana.Kwani wengi watakimbilia UDSM,MUHAS NA SUA/UDOM pekee Wengine ni kilio na kusaga meno.

Ni jukumu la TCU kisheria kuhakikisha wanaodahiliwa wana sifa. TCU hawajaharibu mchakato, wao wamefuata maagizo waliyopewa (kama wana kosa basi ni kunyamaza na kufuata agizo bila kulifanyia kazi na kushauri ipasavyo). Point 4 ndo TCU wanazofuata na sio D2 kama wengi wanavyofikiria (D2 na CE zote zinakubaliwa) lakini hizo zinakuruhusu kuomba bali kupata ni habari nyingine (nafasi zilizopo ndo kikubwa + namba ya waombaji). Point 4 ni kutoka masomo mawili na siyo matatu hivyo DEE ni point 3 tu mkuu.

Sababu kuu za kukosa ni pamoja na kujazana vyuo pendwa hata kama kuna vyuo vingine vina quality ya kutosha kwenye program fulani. Upande wa afya tumeona issue ya PCB-DCC kuhitajika na mbaya zaidi nafasi kuwa chache baada ya vyuo vingi kuzuiwa kudahili pamoja na UDSM. Nafikiri serikali inatakiwa kuliangalia hili-sio kwamba bora liende lakini wakae na vyuo vya afya na chama cha madakitari waangalie nini cha kufanya.

Afadhali wawape waombaji wa afya mikopo lakini ikibidi wavipe vyuo vinavyo onyesha nia ruzuku/mikopo wawe na miundo mbinu mizuri pamoja na walimu. Haipendezi kuona vijana wanaufaulu mzuri wanakosa nafasi. Tuna achwa nyuma africa mashariki.
TCU baada ya zoezi hili itabidi ikae na NACTE na WIZARA na wadau watathmini yaliyotokea, sio tusubiri hadi mwakani tuwe na vilio vingine.
 
Ni jukumu la TCU kisheria kuhakikisha wanaodahiliwa wana sifa. TCU hawajaharibu mchakato, wao wamefuata maagizo waliyopewa (kama wana kosa basi ni kunyamaza na kufuata agizo bila kulifanyia kazi na kushauri ipasavyo). Point 4 ndo TCU wanazofuata na sio D2 kama wengi wanavyofikiria (D2 na CE zote zinakubaliwa) lakini hizo zinakuruhusu kuomba bali kupata ni habari nyingine (nafasi zilizopo ndo kikubwa + namba ya waombaji). Point 4 ni kutoka masomo mawili na siyo matatu hivyo DEE ni point 3 tu mkuu.
Sababu kuu za kukosa ni pamoja na kujazana vyuo pendwa hata kama kuna vyuo vingine vina quality ya kutosha kwenye program fulani. Upande wa afya tumeona issue ya PCB-DCC kuhitajika na mbaya zaidi nafasi kuwa chache baada ya vyuo vingi kuzuiwa kudahili pamoja na UDSM. Nafikiri serikali inatakiwa kuliangalia hili-sio kwamba bora liende lakini wakae na vyuo vya afya na chama cha madakitari waangalie nini cha kufanya. Afadhali wawape waombaji wa afya mikopo lakini ikibidi wavipe vyuo vinavyo onyesha nia ruzuku/mikopo wawe na miundo mbinu mizuri pamoja na walimu. Haipendezi kuona vijana wanaufaulu mzuri wanakosa nafasi. Tuna achwa nyuma africa mashariki.
TCU baada ya zoezi hili itabidi ikae na NACTE na WIZARA na wadau watathmini yaliyotokea, sio tusubiri hadi mwakani tuwe na vilio vingine.
 
Hivi kwanini TCU wanIngilia selection? Nilivyo fahamu mwanzo ni kwamba vyuo vinachagua na kuwaambia TCU tumechagua hawa.... Na kwamba nafasi zimejaa au bado tuna upungufu.
Pia nilicho jua ni kwamba minimum entry qualification ni 4points na siyo lazima minimum ziwe D mbili. Sasa kama una D moja na E mbili wanasema hustahili
Minimum entry qualification ni point 4 kutoka kwenye masomo mawili. Lakini kila kozi INA matakwa yake. Kozi nyingi zinataka Hizo pinti 4 zotokane na D mbili. Kwa hiyo japokuwa ukipata C na E una point NNE na una sifa ya kuingia chuo kikuu lakini kama kozi uliyoomba inataka at least D mbili, basi utakuwa huna sifa ya kusoma kozi hiyo!
 
Je kama mtu kachaguliwa vyuo 3 na course zote asizo zipenda,vp ana weza apply upya?

Dogo wangu Kasoma PCB ana penda awe Doctor au Pharmacia. Ana Div 1 point 8.

Ila amechaguliwa Geology UDSM
Aquatic Sciences-UDOM

Land Mgt- Ardhi Univ.

Course zote hizo hazipendi. Alizijaza tu kama last option kutimiza idadi ya viboma vya machaguo.

Msaada wa mawazo. Je aombe upya au a confirm tu UDSM - Geology?
 
bora nipate chuo mkopo baadae maana mzaz atajibana utaomba mchango kwa mtu atakusaidia utaomba kwenye ngo bt chuo utaomba wapi? hapo unaanza mwakan hivi hawa wakuu wa tcu walisomea hapa hapa tanzania au nje ya tz ila ndo sifa za watanzania ukishapata kitu unamsahau mwingine ndo maana tunaangaika tu kama wafa maji
Hili la TCU ni outcome tu lakini kiini cha matatizo yote haya ni mfumo mbovu wa kusimamia elimu kwa ujumla wake aidha elimu haijapewa kipaumbele ndiyo maana likiisha la TCU litakuja la HESLB nk nk.
Yani utaona matatizo yanajirudia miaka na miaka bila kutafutiwa ufumbuzi au yanaongezeka zaidi na zaidi.

Hatuezi kuendelea kamwe kama nchi na kujenga taifa la waloelimika vizuri kwa ujuzi na maarifa kama sekta ya elimu ikiendelea kupuuzwa na kuwekwa kapuni kama hivi kila mwaka wanakuja na mapya wanafanya majaribio yasoisha kwenye elimu.

Wanaoumia nia wengi hasa vijana na mie nafikiri ni muda wa vijana kuamka na kukataa haya.
 
Je kama mtu kachaguliwa vyuo 3 na course zote asizo zipenda,vp ana weza apply upya?

Dogo wangu Kasoma PCB ana penda awe Doctor au Pharmacia. Ana Div 1 point 8.

Ila amechaguliwa Geology UDSM
Aquatic Sciences-UDOM

Land Mgt- Ardhi Univ.

Course zote hizo hazipendi. Alizijaza tu kama last option kutimiza idadi ya viboma vya machaguo.

Msaada wa mawazo. Je aombe upya au a confirm tu UDSM - Geology?

Hii itabidi awasiliane na vyuo husika anavyotaka kuomba. Isije itakapopelekwa TCU for verification wakasema ameshachaguliwa au amekataa ku-confirm kule alikochaguliwa. Haya ni mawazo yangu sina uhakika na ukweli ukoje bali ni tahadhari tu ya kuchukua. Deadline ya kukonfirm inakaribia hivyo mfanye hima. Huko MD na Pharmacy naona mwaka huu ni majanga na inasikitisha vijana wenye ufaulu mzuri kukosa nafasi. Kama mawasiliano nimagumu aangalie uwezekano wa kukonfirm moja wapo ya hizo ambayo ina nafuu kwake akifika huko anaweza jaribu kuhama degree ingawapo hakuna guarantee.
 
Hii itabidi awasiliane na vyuo husika anavyotaka kuomba. Isije itakapopelekwa TCU for verification wakasema ameshachaguliwa au amekataa ku-confirm kule alikochaguliwa. Haya ni mawazo yangu sina uhakika na ukweli ukoje bali ni tahadhari tu ya kuchukua. Deadline ya kukonfirm inakaribia hivyo mfanye hima. Huko MD na Pharmacy naona mwaka huu ni majanga na inasikitisha vijana wenye ufaulu mzuri kukosa nafasi. Kama mawasiliano nimagumu aangalie uwezekano wa kukonfirm moja wapo ya hizo ambayo ina nafuu kwake akifika huko anaweza jaribu kuhama degree ingawapo hakuna guarantee.
Ahsante mkuu. Nitajaribu kufika moja ya chuo cha MD kesho niongee nao b4 ya ku confirm.
 
kama wakiongeza muda na muda wa kwenda chuonj usogezwe mbele...
Kalenda za vyuo mara nyingi masomo yana anza mwanzo wa Oktoba au katikati hivyo mwaka huu utaona masomo ya vyuo vingi yataanza mwanzo wa November ambacho sio kitu cha kawaida. Kwa hiyo sidhani kama muda utaongezwa zaidi. Kwenya application cycle waliotoa mwanzo TCU/NACTE hakukuwa na round ya pili. Hata hivyo "watasaidia" kupunguza namba ya waliokosa kwa kufungua hii round ya pili ingawa sijui kama kuna mahali wanaonyesha nafasi zilizobaki ni ngapi kwa kila chuo course-ikimaanisha watu wanaomba wakiwa gizani.
 
Ahsante mkuu. Nitajaribu kufika moja ya chuo cha MD kesho niongee nao b4 ya ku confirm.
Ni vizuri katika mazungumzo yako pia ucheck wana nafasi ngapi (kama wanajua) na cut off point yao iko ngapi so far au waliochukuliwa wana ufaulu wa ngapi mwisho ili muangalie ana nafasi gani ya kuchaguliwa. Kama uko Dar aangalie pia vyuo binafsi kama Kairuki na St Joseph (ingawa nasikia ada zao ziko juu ukilinganisha na vya umma).
 
Je kama mtu kachaguliwa vyuo 3 na course zote asizo zipenda,vp ana weza apply upya?

Dogo wangu Kasoma PCB ana penda awe Doctor au Pharmacia. Ana Div 1 point 8.

Ila amechaguliwa Geology UDSM
Aquatic Sciences-UDOM

Land Mgt- Ardhi Univ.

Course zote hizo hazipendi. Alizijaza tu kama last option kutimiza idadi ya viboma vya machaguo.

Msaada wa mawazo. Je aombe upya au a confirm tu UDSM - Geology?
Awe makini sana,kuliko kuharibu ndoto za maisha yake bora apoteze mwaka
 
Back
Top Bottom