TCU na Loans Board, hii imekaaje?

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,307
12,602
Tumedahiriwa vyuo vikuu fulani nchini vyenye ada kubwa kuliko 3,1 mil tunayolipiwa na Loans Board kama mkopo, lakini tumesimamishwa masomo Kwa muda usiojulikana eti Kwa kosa la kupungukiwa kidogo na kile kiasi cha nyongeza tulichopaswa kuongeza ili kukamilisha kiasi cha Ada yao yote ya vyuo hivi. Tumesoma lakini tukazuliwa kufanya mitihani yote hadi tutakapolipa Ada yote.hivyo hatuwezi kuendelea na miaka mingine tena, Sisi ni watoto wa wazazi wanaomudu kulipa Ada kidogo kidogo Kwa kadiri wanavyopata lakini chuo wanataka zote hapohapo kabla hujaingia darasani kusoma.

Tunaomba ufafanuzi Kwa maswali yetu yafuatayo.

1. Ni haki kufukuzwa shule wakati hela yetu ya loans board wamechukuwa?

2. TCU na Loans Board mmebariki kitu kama hiki kufanywa vyuoni?
3. Tutalipaje deni la loans board ikiwa tumefukuzwa tusimalize chuo kwasababu ya Ada ya nyongeza ya vyuo?

4. Je, tukileta ushahidi wa kusimamishwa masomo na vyuo hivyo loans board mko tayari kutukopesha zaidi ili tulipe deni la vyuo?

5. Mnatusaidiaje tuweza kumaliza masomo kwenye hivi vyuo ghali Sana?

6. Kutusimamisha masomo Kwa mtindo huu ni sawa Kwa mujibu wa kanuni za TCU na Loans Board?

7. Hatima yetu ya kuendelea kupata mikopo tutakaporejea vyuoni ikoje? sasa hivi nasikia hela zetu zitarudishwa loans board kwakuwa sisi hatupo darasani
 
Pole sana kijana...ubaya wa Taifa hili kila secta ni malalamiko juu yao tu
 
Mdhamini wako anaweza akawa amepanga kukudhamini nauli ya kwendea sehemu fulani, lakini kwa makadirio ya uwezo wake na idadi ya watu anaowafadhili akaamua atakupatia ela ya kukutosha kutumia usafiri wa daladala kila siku.
Sasa wewe ukiamua kutumia bodaboda au taxi kusafiri yeye hana tatizo atakupa hela ya kutosha kupanda daladala kama ilivyo makubaliano.
Sasa ukishindwa kulipa nauli ya bodaboda uliyoamua kupanda na ukishushwa njiani karibu na kufika yeye anahusikaje?
Aje amwambie bodaboda amalizie safari bure?
Au akulipie nauli ya bodaboda wakati kuna watu walitamani hiyo ya daladala na hawakupata?
Mfumo haujakosea na hakuna wa kumlaumu pambana utafute solution nyingine. Na wengine tujifunze kufanya maamuzi yatakayo affect muda mrefu.

Mfano wako ni feki, haufanani na hilo. Hiyo hela ya nauli hakunipa mimi alimlipa mwenye bodaboda ili anisafirishe ninakotaka kwenda, mtoa pesa kamlipa mwenye usafiri hela pungufu kuliko kiasi anachotaka akitegemea kuwa mimi nitatafuta hela ya kujalizia patakapopungua, matokeo yake hela yake imeliwa na yangu pia imeliwa na safari imekomea njiani, tena katikati ya pori nene. Bahati nzuri mtoa fedha anaufahamu vema mji nilikotaka kwenda na gharama yake, pia anafahamu kuwa mimi sina hela ya kuongezea kwenye ile aliyonipa ndiyo maana nilimlilia msaada wa hali na mali. Je, yeye atanidai hela yake hata kama mwenye bodaboda alinishushia njiani, tena porini? au ni yeye amdai mwenye bodaboda amrudishe hela yake kwakuwa hajanifikisha niendako? au ni yeye amuongeze mwenye usafiri ili anifikishe safari yangu ili aje anidai mimi? Kosa la mwenye bodaboda hakumwambia mapema mtoa nauli kuwa ile hela punguvu ingemfikisha mteja wake hadi wapi, alipokea tu na kuitia mfukoni. Angeniambia mapema kama hii hela niliyopewa ingetosha kunisafirisha hadi pale porini aliponishusha kamwe nisingeukubali msaada ule, maana ingekuwa sana na mtu aliyeshonewa shati pekee bila kaptura ya kuvalia lile shati.
 
Nadhani namba 4 nikuwa haiwezekani, sababu hiyo ni ada anayolipiwa alieko private , ada ya serkalini haifiki huko, na ukichagua vyuo hivyo maana yake unaweza kumudu.
nadhani utaratibu wa chuo kuwasimamisha hauko vizuri, zaidi waweke utaratbu wa malipo ya awamu, hali si nzuri kwa kila mmoja na vyuo vya serkali haviwezi kuwabeba wote.
 
Punguza jazba
Mi ninavyofahamu ada ya kozi yako unaijua kabla hujaaply. Tatizo labda kama mtu hatataka kujua hilo au ada imebadilika badae, na bodi wanatoa hela ya ada kulingana na gharama iliyoko katika vyuo vya serikali.
Kwa iyo ukichagua vyuo vyenye ada kubwa na unajua possibility ya kupata mkopo mwisho maybe ni 1.5ml utahitajika kulipa iliyobaki mwenyewe.
Na bodi wanafahamu kabisa kuna vyuo vyenye ada kubwa zaidi ya mkopo wanaokupa na sambamba na hilo wanafahamu kuwa kozi hiyo hiyo katika chuo cha serikali itakuwa inaendana na hela waliyokupa.
Na hawajui kama huna ela ya kuongezea kwa sababu ulichagua mwenyewe.
Sipo apa kuonesha kuwa ulikosea ila natamani uelewe kuwa usijaribu kutafuta wa kumlaumu, bodi haiwezi kuongeza hela kamwe na chuo hawewezi kukuruhusu kuendelea kama ujamalizia kulipa.
Kama ni mapema acha chuo uanze kwingine, kama ushafika mbali tafuta namna ya kulipa iyo ada. Au kama vipi acha chuo kabisa kwa sababu sio kwamba ukimalliza ni guarantee ya mafanikio

Naona tunaokumbwa na kadhia kama hii tuko wengi, hii inaonyesha kuwa serikali inapoteza hela zake kusomesha watoto wa maskini kama sisi kwenye vyuo vya private vyenye ada kubwa sana kuliko mkopo, maana kuna uhakika wa wazazi wa aina hii kupata kwa wakati hela ya kuongezea. Mimi sikupenda kabisa kusoma vyuo kama hivi vyenye ada kubwa, lakini ningefanya nini kama nafasi kwenye vyuo vya umma nilikosa? Seikali nadhani iache kabisa kutoa hela kusomesha wanafunzi kwenye vyuo binafsi vya bei kubwa ambavyo havina uvumilivu na watoto wa maskini wanaopata fedha kidogokidogo kwa kuuza vyungu, mazao ya msimu yanayosubiri mvua, na mihogo ya kukaanga. Ona sasa, kama mzazi asipoipata hiyo hela serikali itazipataje hela zake ilizonikopesha kwa ada, meals na accommodation kwa miaka 3? ni hasara kwangu, kwa mzazi na kwa erikali.

Vyuo binafsi waende kusoma watu wenye hela zao tu, sio sisi watoto wa maskini wanaopewa hela kidogo na HESLB wakitegemea kuwa wakatafute sh. 5,000,000 za ziada kwa mwaka.
 
Nadhani namba 4 nikuwa haiwezekani, sababu hiyo ni ada anayolipiwa alieko private , ada ya serkalini haifiki huko, na ukichagua vyuo hivyo maana yake unaweza kumudu.
nadhani utaratibu wa chuo kuwasimamisha hauko vizuri, zaidi waweke utaratbu wa malipo ya awamu, hali si nzuri kwa kila mmoja na vyuo vya serkali haviwezi kuwabeba wote.
Kama hakuna majibu ya TCU tutakwenda kupiga hodi ofisi No 1, aende achukue hela yake kule isipotee bure au bodi ya mikopo kuja kunidai hela hiyo bure wakati sijasoma na kumaliza, sawa na mtu aliyenyanyuliwa juu ya kifua cha mpenzi wake katikati ya "shughuli" muda mfupi karibu na kupiga mshindo.
 
Mfano wako ni feki, haufanani na hilo. Hiyo hela ya nauli hakunipa mimi alimlipa mwenye bodaboda ili anisafirishe ninakotaka kwenda, mtoa pesa kamlipa mwenye usafiri hela pungufu kuliko kiasi anachotaka akitegemea kuwa mimi nitatafuta hela ya kujalizia patakapopungua, matokeo yake hela yake imeliwa na yangu pia imeliwa na safari imekomea njiani, tena katikati ya pori nene. Bahati nzuri mtoa fedha anaufahamu vema mji nilikotaka kwenda na gharama yake, pia anafahamu kuwa mimi sina hela ya kuongezea kwenye ile aliyonipa ndiyo maana nilimlilia msaada wa hali na mali. Je, yeye atanidai hela yake hata kama mwenye bodaboda alinishushia njiani, tena porini? au ni yeye amdai mwenye bodaboda amrudishe hela yake kwakuwa hajanifikisha niendako? au ni yeye amuongeze mwenye usafiri ili anifikishe safari yangu ili aje anidai mimi? Kosa la mwenye bodaboda hakumwambia mapema mtoa nauli kuwa ile hela punguvu ingemfikisha mteja wake hadi wapi, alipokea tu na kuitia mfukoni. Angeniambia mapema kama hii hela niliyopewa ingetosha kunisafirisha hadi pale porini aliponishusha kamwe nisingeukubali msaada ule, maana ingekuwa sana na mtu aliyeshonewa shati pekee bila kaptura ya kuvalia lile shati.

Sasa hapa unachopinga ni nini? Jamaa alikuelekeza vizuri sana na alitumia mfano unao lingana na mazingira yako. Nionavyo vijana wengi huwa hamna uelewa wa kutosha wakati kuchagua vyuo. Serikali ina kiwango cha ada katika kila taaluma, ukichagua chuo unapaswa uangalie na fee structure ya chuo na ukomo wa Serikali. Ukichagua maana yake kinachozidi utalipa wewe.

Katika hili TCU na HESLB usiwabebeshe mzigo hilo ni lako na familia yako.
 
Sasa hapa unachopinga ni nini? Jamaa alikuelekeza vizuri sana na alitumia mfano unao lingana na mazingira yako. Nionavyo vijana wengi huwa hamna uelewa wa kutosha wakati kuchagua vyuo. Serikali ina kiwango cha ada katika kila taaluma, ukichagua chuo unapaswa uangalie na fee structure ya chuo na ukomo wa Serikali. Ukichagua maana yake kinachozidi utalipa wewe.

Katika hili TCU na HESLB usiwabebeshe mzigo hilo ni lako na familia yako.
Mnakosea kusema hivyo, anayeshindwa kulipa ada sio mwanafunzi bali mzazi wake ambae alidhani ataweza ghafla anajikuta gunia lake la mahindi linakosa bei sokoni.

Lakini asilimia 99 ya watoto wa Tanzania tunaapply vyuo vya umma na wanalazimika kwenda vyuo vya private kama last resort. Hivyo hata kama ungekuwa na uhodari na uelewa wa kozi na vyuo ni kazi bure. Huwezi kwenda kusoma kozi yoyote hata kama haiko moyoni eti kwasababu Tu ina ada ndogo, huo ni usomi gani unauonyesha kwetu vijana, yaani ukasomee vetenary eti kwakuwa Ada ndogo
 
Hivi kwa nini usingeacha wewe kwenda ili wenzako wenye uwezo wa kuongeza wapate nafasi kuliko unavyo shauri?
Huo ni upuuzi, hayo mwambie mzazi wangu sio mm. Lakini kila mtu ana haki ya kupata elimu, vyuo hivi vingetangaza kabisa kuwa mwanafunzi mwenye wazazi wanaolipa Kwa kudunduliza wasikanyage vyuo vyao. Serikali ilinilipia kwao 3.1 m kwa mwaka, je hiyo wamemwambia mzazi na serikali kama inatosha kupata huduma zipi na zipi hapo chuoni? Sio kwamba mzazi asingelipa kiasi kinachotakiwa, angelipa Tu lakini sio Kwa mkupuo kama wanavyotaka wao. Hivi Yuko mtu mwenye akili sahihi atakayekiacha cheti chake chuoni milele bila kukikomboa?
 
Back
Top Bottom