TCU mnafanya haya madudu kwa faida ya nani?

herikipaji

JF-Expert Member
Aug 23, 2016
1,198
1,345
Sintofahamu nyingi zinajitokeza na bado zinaendelea kutokea kutokana na hii taasisi inayosimamia elimu ya juu kukosa umakini na kuwajibika ipasavyo kwa makusudi au kwa sababu nyingine wanazozijua wao wenyewe hali inayosababisha usumbufu na matatizo lukuki kwa wanafunzi.

Application ya vyuo vikuu ilifunguliwa tarehe 15 August kwa Diploma holders lakini ajabu ni hawa TCU kufanya deadline tarehe 31 August huu ni muda mfupi sana, siku 15 tuu hivi TCU mna ajenda gani ya siri na mnayafanya haya yote kwa faida ya nani? Kama mnataka watu wasisome basi kuweni wazi tu ifahamike moja.

Baadhi ya vyuo hata matokeo ya final overall hadi hivi sasa bado hayajatoka na wanafunzi wa vyuo hivyo wameshalipia ada ya udahili ina maana hawa wanafunzi wanakosa nafasi na haki yao ya msingi ya kuendelea kusoma? Mlichelewa sana kufungua application na sasa mnawahi kufunga mna makusudi gani hivi?

Ilianza GPA na cut off point kwa A-level watu wamekwishafanya mitihani mnakuja na viwango vipya ni sawa na kwenda kumtoa mfungwa aliyeko gerezani kufuta hukumu yake na kumhukumu upya kwa sheria mpya iliyotungwa, maajabu haya!!
Haya sasa wale wachache waliofikisha hata hizo GPA mnakuja tena kuwachimbia mashimo ya mitego ili tu waanguke kwa kuwapangia siku 14 za application, hivyo vyuo vikuu mnataka nani akasome mwaka huu?
Madudu haya yote mnayoyafanya ni kwa faida ya nani??

Kazi mnayoonekana kufanikiwa kuifanya vema ni kuwachimbia mashimo watu wasisome vyuo vikuu mwaka huu, mmegeuka WACHIMBA MASHIMO.
Hamtendi haki.
 
Ila kwa Dit bado hayajapelekwa , so nimajanga kwa watoto wa dit OD 13 waliyotaka kuunga atakama haukupata supp.
Huyo unaemuelewesha amekimbilia kujibu mada bila hata kuelewa na kutafakari nilichoandika, yani hajui na hajui kama hajui ila anajifanya anajua huyo ni .....
 
Usiangaike na upuuzi wa watu wenye ngozi nyeusi, hebu wasuliana na hawa jamaa gel.co.tz ukasome nje ya nchi huko...
Ndugu huwa tunashindwa kuwaprove wrong wale wanaosema mtu mweusi kalaaniwa, huwa nikifikiri hata sipati majibu sababu ya kuwa hivi.
 
Sintofahamu nyingi zinajitokeza na bado zinaendelea kutokea kutokana na hii taasisi inayosimamia elimu ya juu kukosa umakini na kuwajibika ipasavyo kwa makusudi au kwa sababu nyingine wanazozijua wao wenyewe hali inayosababisha usumbufu na matatizo lukuki kwa wanafunzi.

Application ya vyuo vikuu ilifunguliwa tarehe 15 August kwa Diploma holders lakini ajabu ni hawa TCU kufanya deadline tarehe 31 August huu ni muda mfupi sana, siku 15 tuu hivi TCU mna ajenda gani ya siri na mnayafanya haya yote kwa faida ya nani? Kama mnataka watu wasisome basi kuweni wazi tu ifahamike moja.

Baadhi ya vyuo hata matokeo ya final overall hadi hivi sasa bado hayajatoka na wanafunzi wa vyuo hivyo wameshalipia ada ya udahili ina maana hawa wanafunzi wanakosa nafasi na haki yao ya msingi ya kuendelea kusoma? Mlichelewa sana kufungua application na sasa mnawahi kufunga mna makusudi gani hivi?

Ilianza GPA na cut off point kwa A-level watu wamekwishafanya mitihani mnakuja na viwango vipya ni sawa na kwenda kumtoa mfungwa aliyeko gerezani kufuta hukumu yake na kumhukumu upya kwa sheria mpya iliyotungwa, maajabu haya!!
Haya sasa wale wachache waliofikisha hata hizo GPA mnakuja tena kuwachimbia mashimo ya mitego ili tu waanguke kwa kuwapangia siku 14 za application, hivyo vyuo vikuu mnataka nani akasome mwaka huu?
Madudu haya yote mnayoyafanya ni kwa faida ya nani??

Kazi mnayoonekana kufanikiwa kuifanya vema ni kuwachimbia mashimo watu wasisome vyuo vikuu mwaka huu, mmegeuka WACHIMBA MASHIMO.
Hamtendi haki.
Sio kila kitu kuwalaumu TCU,mbona mwaka jana watu waliwahi kufanya maombi na hakukuwa na malalamiko?! Let say TCU wangefungua udahili mapema unategemea mpaka sasa deadline ingekuwa bado?!
Maana yake ungekosa pia nafasi ya kufanya maombi. Kwanini usilaumu chuo chako kwa kuchelewa kufanya mtihani ili muende sambamba na kipindi cha udahili?!
Tusipende kila kitu kulaumu,hata wangefanya nn wasingeweza kuridhisha wadahiliwa wote!
Nawasilisha..!
 
Sio kila kitu kuwalaumu TCU,mbona mwaka jana watu waliwahi kufanya maombi na hakukuwa na malalamiko?! Let say TCU wangefungua udahili mapema unategemea mpaka sasa deadline ingekuwa bado?!
Maana yake ungekosa pia nafasi ya kufanya maombi. Kwanini usilaumu chuo chako kwa kuchelewa kufanya mtihani ili muende sambamba na kipindi cha udahili?!
Tusipende kila kitu kulaumu,hata wangefanya nn wasingeweza kuridhisha wadahiliwa wote!
Nawasilisha..!
Hiyo mwaka jana nao walipangiwa siku 14 na TCU?
 
Hiyo mwaka jana nao walipangiwa siku 14 na TCU?
Wewe unasimamia wapi?! Wiki 2 au ungependa na wewe ufanye maombi?!
Kuna vyuo vya afya now ndo wapo kwenye mitihani so na wao walalamike deadline isifungwe mpaka matokeo yatakapotoka?!
Usijione wewe tu ndo hupendwi na TCU after all hata mwakani pia unaweza kuapply sioni nini kinakufanya ulalame.
 
Kumbe wanaoomba kusoma Diploma wanatuma maombi yao TCU?! nilidhani wanatuma NACTE
 
Wewe unasimamia wapi?! Wiki 2 au ungependa na wewe ufanye maombi?!
Kuna vyuo vya afya now ndo wapo kwenye mitihani so na wao walalamike deadline isifungwe mpaka matokeo yatakapotoka?!
Usijione wewe tu ndo hupendwi na TCU after all hata mwakani pia unaweza kuapply sioni nini kinakufanya ulalame.
There you are, unanishambulia mie na ukikimbia hoja ilioko kwenye mada ndugu.
Halafu sio wote tuko na hizo tabia za kibinafsi za umimi kwa kujiangalia mwenyewe tuu, hizi ndiyo zinasababisha umaskini kwenye jamii na taifa zima. Yanapofanyika mambo ya hovyo na wale walopewa dhamana ya kuyasimamia siwezi kubaki kimya nitapinga, kweli nitapinga na nitaendelea kupinga mpaka wajirekebishe na kufanya kazi kwa ueledi na siyo kwa mazoea hii haijalishi kama mimi ni mhanga au laa. Wanalipwa kwa kodi zetu hawa lazima nipinge na kuhoji uwajibikaji wao pale wanapotenda sivyo hilo ufahamu.

Turudi kwenye swali langu hujanijibu mwaka jana nao walipangiwa siku 14?
 
Back
Top Bottom