TCU fungueni Dirisha la Nne

Oct 12, 2015
74
67
Wanabodi habari ya asubuhi murua kabisa, nilikua napita vijiweni nakuta vijana wanalalamika sana hawa wanaoomba vyuo vikuu, nasikia utaratibu umebadilika sio kama zamani sie tulikua tuna apply directly TCU.

Sasa ivi vijana wanaomba kwenye vyuo husika sio mbaya lakini wengi nimeona wanalalamika kuhusu kukosa nafasi hasa zile kozi za afya competition ikiwa ya juu.

Lakini pia, nikasikia kuna watu wamechaguliwa vyuo viwili viwili hii inaleta ufinyu wa nafasi, nikasikia mmeshafungua dirisha la kwanza mpaka la tatu, nawasihi waongezeeni dirisha la nne hawa vijana watimize ndoto zao, wasibabaike mitaani.
 
Ufaulu kwa mwaka huu umekuwa mkubwa sana, ni ngumu kupata nafasi ya kozi ambayo mwanafunzi anaitarajia!
 
Back
Top Bottom