Tatizo ni TCRA kutoweza kutekeleza wanachozungumza au kudanganya wananchi.Nilisha wahi wauliza startimes wakasema haiwezekani wao walipie local Chanel afu wafanye bure kuzionesha so wataendelea kuziuza, nadhani kunatatizo some where.
Wajua hili tamko liko kisiasa zaidi kwakuwa ili warushe hizo channel bure inabidi wenye hizo channel walipe kampuni za ving'amuzi kufanya hivyo wasipolipa hawazirushi.No kihusu malipo ya bure kwa TV za ndani. Star time wamegoma kabisaaa hadi dakika hii nakwenda hewani. Jamaa walitoa tamko kutafuta kiki ya mwisho wa mwaka ika wamekutana na watoto was mjini zaidi yao.
Hapo ndio huwa naona watz wengi wajinga. Kabisa unakuta wanapongeza kwa mabadiliko. Mabadiliko yepi?eti rushwa imeisha,wakati huohuo kuna jitu lina vyeti feki na ni RC?nini maana ya rushwa?Huwa nashangaa eti watu kuambiwa kuna mabadiliko ya kiutendaji nchi hii. Hao TCRA sio mara moja tumewaandikia e-mail na wala hawajibu huu uhuni unaofanywa na hayo makampuni. Ukienda kwenye ofisi za hao jamaa wa ving'amuzi utakuta wanakutoza malipo ya kubadili smart card eti ili uone hizo local channels bure. Kuna wakati napata hisia ni mchezo unachezwa kati ya hao watu na serekali ili kuibia wananchi wake. Ni nani hajasikia hilo tangazo la TCRA kuhusu local channels kuwa bure, na kwanini halitekelezwi bali ya kurudiwarudiwa kila mara?