TCRA washughulikieni Halotel

ESCORT 1

JF-Expert Member
Dec 7, 2015
1,267
2,519
Kampuni Ya Simu Ya Halotel Kupitia Mawakala Wake Imekuwa Ikiuza Laini Za Wanachuo Kwa Wananchi Wa Kawaida Ambao Si Wanachuo Hivyo Kuwa Wamekiuka Kanuni Na Masharti Zilizowekwa Na Mamlaka Husika. HALOTEL Ni Kama Wanakwepa KODI Tu.

Kwa Sasa Ukiwa Na Buku Mbili Yako Unapata Laini Ya Chuo Kutoka Halotel Ambapo Inakuwezesha Kuunga Bando La Chuo Popote Ulipo Hivyo Kufanya Kampuni Nyingine Kukosa Wateja Kabisa.

TCRA Wachukulieni Hatua Hawa Wavietnam Wanaowanyima Haki Wanachuo Wetu Wa Tanzania.
Pia Watanzania Wenzangu Ambao Sio Wanachuo Tuache Kupenda Kitonga, Bando Za Chuo Tuwaachie Wanafunzi.
Nasubiria MADONGO Yenu Maana Ukweli Siku Zote HUUMA.

Jumapili Njema Kwenu.
 
Huenda wewe ni yule jamaa wa pale TIGO Customer care ambaye ni kiherehere ajabu utazani unahisa kwenye kampuni!..sasa hao wanachuo watakaa chuoni milele? mwanachuo ni nani? mimi naefanya kazi halafu nasoma utaniitaje? ovyo kabisa wewe, chuoni sio mahabusu hadi TCRA waweze kucontrol hilo. watu chuoni wanasoma short course kibao nakusepa, wanaodisco kibao, evening class kibao, wanaomaliza kibao, sasa wewe umetumia kigezo gani kusema hayo? waacheni wawakaange nyie bakieni na tabia yenu ya kupunguza bando tu, na 4G isiyo na maana...TENA WACHA NIHAMASISHE WATU WENGI TUKAJIUNGE HALOTEL.....Mpango mzima...
 
Back
Top Bottom