TCRA Mko wapi? Hiki kinachoendelea Mtama Fm ni aibu.

TCRA Mko wapi? Hiki kinachoendelea Mtama Fm ni aibu.

astalavista

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2014
Posts
261
Reaction score
304
Nafahamu weledi ni tatizo kwenye 'media' nyingi sasa hivi, imekuwa ni kawaida kutozingatia misingi na miiko ya taaluma ya habari. Mtama Fm ni miongoni mwa sehemu ya aibu kwa vyombo vyetu vya habari nchini.

Pamoja na uchanga wake lakini si sahihi kuacha watangazaji wenye makosa ya wazi ya matamshi, tatizo la R na L ni la kitaifa lakini kwenye chombo hiki cha habari ni zaidi.

Ipo wazi kwa mikoa ya kusini kuna changamoto ya kutamka M, kmv Mtoto/Ntoto. Makosa haya ya matamshi hayakutakiwa yaje kwenye radio, sehemu ambayo tunaamini makosa yatakuwa machache.

Rai yangu kwa TCRA tafadhalini kuweni karibu na hivi vyombo vya habari hasa vichanga ili kuhakikisha maudhuhi kwa hadhira yanaenda pasipo kunajisiwa kiswahili chetu.

Rai yangu kwa wahusika kiutawala Mtama Fm zingatieni weledi na miiko ya taaluma kwa kuwa na angalau mtu mmoja mwenye taaluma ambaye ataweza kuwashape wengine kwenye njia nzuri.
 
Mods iende jukwaa la habari mchanganyiko tafadhali, ni makosa yamefanyika kuja hapa.
 
Nafahamu weledi ni tatizo kwenye 'media' nyingi sasa hivi, imekuwa ni kawaida kutozingatia misingi na miiko ya taaluma ya habari. Mtama Fm ni miongoni mwa sehemu ya aibu kwa vyombo vyetu vya habari nchini.

Pamoja na uchanga wake lakini si sahihi kuacha watangazaji wenye makosa ya wazi ya matamshi, tatizo la R na L ni la kitaifa lakini kwenye chombo hiki cha habari ni zaidi.

Ipo wazi kwa mikoa ya kusini kuna changamoto ya kutamka M, kmv Mtoto/Ntoto. Makosa haya ya matamshi hayakutakiwa yaje kwenye radio, sehemu ambayo tunaamini makosa yatakuwa machache.

Rai yangu kwa TCRA tafadhalini kuweni karibu na hivi vyombo vya habari hasa vichanga ili kuhakikisha maudhuhi kwa hadhira yanaenda pasipo kunajisiwa kiswahili chetu.

Rai yangu kwa wahusika kiutawala Mtama Fm zingatieni weledi na miiko ya taaluma kwa kuwa na angalau mtu mmoja mwenye taaluma ambaye ataweza kuwashape wengine kwenye njia nzuri.
Nilipoona Mtama FM na TCRA nikawa nasoma mpaka mwisho nijue kama tayari yule jamaa wa Mtama anatumia redio kukashifu wengine na kuhatarisha amani ya nchi. Kumbe ni mambo ya L na R. Sidhani kama TCRA wanashughulika na mambo ya sarufi ya lugha bali wao wanashughulika na maudhui hatarishi kwa amani.

Hao waandishi wa habari unakuta wana vyeti vya taaluma lakini kwa sasa Watanzania hatujui Kiingereza wala Kiswahili.

Wito uende kwa wizara ya elimu kutilia mkazo masomo ya lugha kikamilifu kwa sababu lugha ni chombo cha mawasiliano
 
Back
Top Bottom