Drone Camera
JF-Expert Member
- Jul 25, 2017
- 14,007
- 13,799
Ndugu zangu Watanzania, wale wahuni bado wapo sana. Sahivi sio ile hela tuma kwenye namba hii au niwekee laki tatu nikuwekee milioni moja. Leo wamenijia na mbinu mpya kabisa kwangu. Au wengine walishawajia kwa pigo hizi? Kwangu mimi hizi pigo ni mpya.
Nimetulia nafanya mambo yangu mara namba ngeni inaingia, nikajifikiria kuitosa ila nikasema wacha nisikie huyu boya ana habari gani. Mazungumzo yakaanza:
Jamaa: Hellow mteja, mimi ni customer care wa tigo. Natumai u mzima na unafurahia huduma zetu.
Mimi: Naam, bila shaka.
Jamaa: Asante sana ndugu mteja. Sasa kuna shida moja tungependa utusaidie wewe kama mteja mwaminifu..
Mimi: Jambo gani hilo?
Jamaa: Kuna pesa imetumwa humo kwako kimakosa ndugu mteja. Tunatumai umeiona ili tukupe maelezo zaidi.
Mimi: Sijaona meseji mimmi
Jamaa: Basi kata ikiingia tutakupigia.
Ujumbe ukaingia, kiasi hewa kilichoingia 498,000/=(Ntaweka screenshot hapa chini). Akapiga baada ya sekunde chache. Maongezi yakaendelea tena;
Jamaa: Umeiona ndugu mteja mwaminifu?
Mimi: Ndiyo nimeiona.
Jamaa: Unaweza kututajia ni kiasi gani kama hutojali.
Mimi: Ndiyo naweza.
Jamaa: Ni kiasi gani.
Mimi: 498,000/=.
Jamaa: Vizuri sana ndugu mteja mwaminifu. Sasa tunaomba uaminifu wako katika hili. Chukua kalamu na karatasi, nenda sehemu kimya kabisa tulivu tukupe maelezo, usikate simu.
Mimi: Haya tayari
Jamaa: Mbona tumesikia sauti ya vyuma kugongana.
Mimi: Nimefunga geti
Jamaa: Haha, vizuri sana ndugu mteja. Unaonekana mwaminifu halafu mjanja sana. Kwa kweli tumepata bahati sana pesa ya mteja wetu kufika kwako. Upo wapi kwanza?
Mimi: Nipo Mwanza
Jamaa: Haha kumbe mtani kabisa (Akasifia wee)
Mimi: Nipe maelezo unanipotezea muda
Jamaa: Samahani ndugu mteja, Andika hii namba 0675566220 jina ni Elizabeth Nyanda. Hebu rudia(Nikarudia)
Jamaa: Sasa nenda kwa wakala wa tigo pesa. Usimwonyeshe hiyo SMS wala usimwambie mtu kakosea namba..Hao mawakala ni wahuni sana. Cha kufanya Mwambie wakala Atume 450,000 kwenye hiyo namba. Hiyo 48,000 inayobaki itakuwa zawadi ya uaminifu wako kwetu. Tumefurahishwa sana na uaminifu wako.
Mimi: Sawa bro. Sasa mzee nakuuliza swali (akakubali). Kwanini hiyo hela nisiitume kwenye hiyo namba mimi mwenyewe.
Jamaa: Hapana ndugu mteja, hiyo hela imeingia humo kwa Master Card. Haiwezekani kufanya hivyo
Mimi: Kaka yaani mimi ni wakala mstaafu hivyo naelewa kila kitu. Huwezi nidanganya
Jamaa: Ulikuwepo kwenye semina ya mawakala jana? Ndio ilipitishwa hivyo
Mimi: Sawa mzee. Sasa mi nafanya hivi; hiyo hela siitoi wala siigusi. Nyie wenyewe Tigo muitoe muirudishe kwa mwenye nayo.
Jamaa: Hiyo hela imeingia kwa MasterCard, mwenye nayo katuma kwa USD hivyo sisi hatuwezi irudisha. Hiyo njia niliyokuambia ndio msaada pekee.
Mimi: Wewe ni tapeli
Jamaa: Unasemaa?
Mimi: Wewe ni tapeli mchanga kwenye utapeli
Jamaa: Kwa nini ndugu mteja?
Mimi: Meseji za tigopesa kwangu zikiingia zinakuwa na Jina la tigo pesa na sio namba ya mtu
Jamaa: Usikariri ndugu mteja, siku mitambo ikisumbua tuna haki ya kutumia namba yoyote ile.
Mimi: Mshenzi wewe kawatapeli wa kuja labda, wewe bado sana kwangu.
Jamaa: Ahaa unatutukana, ngoja nimwambie bosi hapa akufungie laini halafu tunamwambia na polisi hapa aje akukamate kwa kutudhalilisha sisi taasisi kubwa.(akampa simu huyo bosi wake).
Bosi fake: Wewe unatuchezea. Tutakupeleka polisi
Mimi: Polisi na tigopesa wapi na wapi. Washenzi tu nyie katapelini wajinga huko sio watanzania wajanja.Tulishajanjaruka sasa hivi
Jamaa: Mjanja wapi wewe (tusi halafu akakata)
…………………………
======
TCRA hawa watu bado wapo. Sijui kama kuna ambao walishachukuliwa hatua. Ukiona maelezo hapo juu ni rahisi kwa watanzania wengi kulizwa.
Halafu huu mfumo wa kuwa na namba nyingi unawanufaisha hawa sababu mwananchi anajua ana laini moja kumbe kuna nyingine zilizosajiliwa kwa taarifa zake zinatumika bila kujua.TCRA liangalieni hili tena halafu fanyeni hima kuwakamata wajinga hawa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimetulia nafanya mambo yangu mara namba ngeni inaingia, nikajifikiria kuitosa ila nikasema wacha nisikie huyu boya ana habari gani. Mazungumzo yakaanza:
Jamaa: Hellow mteja, mimi ni customer care wa tigo. Natumai u mzima na unafurahia huduma zetu.
Mimi: Naam, bila shaka.
Jamaa: Asante sana ndugu mteja. Sasa kuna shida moja tungependa utusaidie wewe kama mteja mwaminifu..
Mimi: Jambo gani hilo?
Jamaa: Kuna pesa imetumwa humo kwako kimakosa ndugu mteja. Tunatumai umeiona ili tukupe maelezo zaidi.
Mimi: Sijaona meseji mimmi
Jamaa: Basi kata ikiingia tutakupigia.
Ujumbe ukaingia, kiasi hewa kilichoingia 498,000/=(Ntaweka screenshot hapa chini). Akapiga baada ya sekunde chache. Maongezi yakaendelea tena;
Jamaa: Umeiona ndugu mteja mwaminifu?
Mimi: Ndiyo nimeiona.
Jamaa: Unaweza kututajia ni kiasi gani kama hutojali.
Mimi: Ndiyo naweza.
Jamaa: Ni kiasi gani.
Mimi: 498,000/=.
Jamaa: Vizuri sana ndugu mteja mwaminifu. Sasa tunaomba uaminifu wako katika hili. Chukua kalamu na karatasi, nenda sehemu kimya kabisa tulivu tukupe maelezo, usikate simu.
Mimi: Haya tayari
Jamaa: Mbona tumesikia sauti ya vyuma kugongana.
Mimi: Nimefunga geti
Jamaa: Haha, vizuri sana ndugu mteja. Unaonekana mwaminifu halafu mjanja sana. Kwa kweli tumepata bahati sana pesa ya mteja wetu kufika kwako. Upo wapi kwanza?
Mimi: Nipo Mwanza
Jamaa: Haha kumbe mtani kabisa (Akasifia wee)
Mimi: Nipe maelezo unanipotezea muda
Jamaa: Samahani ndugu mteja, Andika hii namba 0675566220 jina ni Elizabeth Nyanda. Hebu rudia(Nikarudia)
Jamaa: Sasa nenda kwa wakala wa tigo pesa. Usimwonyeshe hiyo SMS wala usimwambie mtu kakosea namba..Hao mawakala ni wahuni sana. Cha kufanya Mwambie wakala Atume 450,000 kwenye hiyo namba. Hiyo 48,000 inayobaki itakuwa zawadi ya uaminifu wako kwetu. Tumefurahishwa sana na uaminifu wako.
Mimi: Sawa bro. Sasa mzee nakuuliza swali (akakubali). Kwanini hiyo hela nisiitume kwenye hiyo namba mimi mwenyewe.
Jamaa: Hapana ndugu mteja, hiyo hela imeingia humo kwa Master Card. Haiwezekani kufanya hivyo
Mimi: Kaka yaani mimi ni wakala mstaafu hivyo naelewa kila kitu. Huwezi nidanganya
Jamaa: Ulikuwepo kwenye semina ya mawakala jana? Ndio ilipitishwa hivyo
Mimi: Sawa mzee. Sasa mi nafanya hivi; hiyo hela siitoi wala siigusi. Nyie wenyewe Tigo muitoe muirudishe kwa mwenye nayo.
Jamaa: Hiyo hela imeingia kwa MasterCard, mwenye nayo katuma kwa USD hivyo sisi hatuwezi irudisha. Hiyo njia niliyokuambia ndio msaada pekee.
Mimi: Wewe ni tapeli
Jamaa: Unasemaa?
Mimi: Wewe ni tapeli mchanga kwenye utapeli
Jamaa: Kwa nini ndugu mteja?
Mimi: Meseji za tigopesa kwangu zikiingia zinakuwa na Jina la tigo pesa na sio namba ya mtu
Jamaa: Usikariri ndugu mteja, siku mitambo ikisumbua tuna haki ya kutumia namba yoyote ile.
Mimi: Mshenzi wewe kawatapeli wa kuja labda, wewe bado sana kwangu.
Jamaa: Ahaa unatutukana, ngoja nimwambie bosi hapa akufungie laini halafu tunamwambia na polisi hapa aje akukamate kwa kutudhalilisha sisi taasisi kubwa.(akampa simu huyo bosi wake).
Bosi fake: Wewe unatuchezea. Tutakupeleka polisi
Mimi: Polisi na tigopesa wapi na wapi. Washenzi tu nyie katapelini wajinga huko sio watanzania wajanja.Tulishajanjaruka sasa hivi
Jamaa: Mjanja wapi wewe (tusi halafu akakata)
…………………………
======
TCRA hawa watu bado wapo. Sijui kama kuna ambao walishachukuliwa hatua. Ukiona maelezo hapo juu ni rahisi kwa watanzania wengi kulizwa.
Halafu huu mfumo wa kuwa na namba nyingi unawanufaisha hawa sababu mwananchi anajua ana laini moja kumbe kuna nyingine zilizosajiliwa kwa taarifa zake zinatumika bila kujua.TCRA liangalieni hili tena halafu fanyeni hima kuwakamata wajinga hawa.
Nawasilisha.
Sent using Jamii Forums mobile app