Shirika la viwango Tanzania lina jukumu kubwa la kusimamia viwango vya bidhaa zinazozalishwa hapa nchini na zile zinazoingizwa kutoka nje. Ajabu ni kwamba Soko la bidhaa mbalimbali kutoka nje limefurika bidha zisizokIdhi viwango, fake.
Bidhaa nyingi kutoka China, hasa vifaa vya ujenzi na vipuri vya magari na mitambo mbalimbali ni fake. Kama nchi inabidi tutumie fedha za kigeni mara kwa mara kuagiza bidhaa fake, zisizodumu.
Huko TBS ina wasomi kibao walioajiriwa na wanalipwa mishahara mikubwa na kusomeshwa ndani na nje ya nchi lakini hawana tija kwa taifa.
Hali hii isipodhibitiwa haraka, nchi itaendelea kuwa maskini kwa kuwa soko la bidhaa bandia na kutumia pesa kidogo tuliyonayo kutengeneza ajira kwa wachina. Pia hali kama hii inadhihirisha udhaifu serikali, ufisadi na ubinafsi wa viongozi walio madarakani.
Tunatokaje hapa?
Bidhaa nyingi kutoka China, hasa vifaa vya ujenzi na vipuri vya magari na mitambo mbalimbali ni fake. Kama nchi inabidi tutumie fedha za kigeni mara kwa mara kuagiza bidhaa fake, zisizodumu.
Huko TBS ina wasomi kibao walioajiriwa na wanalipwa mishahara mikubwa na kusomeshwa ndani na nje ya nchi lakini hawana tija kwa taifa.
Hali hii isipodhibitiwa haraka, nchi itaendelea kuwa maskini kwa kuwa soko la bidhaa bandia na kutumia pesa kidogo tuliyonayo kutengeneza ajira kwa wachina. Pia hali kama hii inadhihirisha udhaifu serikali, ufisadi na ubinafsi wa viongozi walio madarakani.
Tunatokaje hapa?