TBS kimenuka interview

TBS kimenuka interview

TBS shortlist ilikua imefanyika na majina kwa ajili ya interview yalikua yatoke soon watu hawakuwa wengi kama ilivyo sasa. ila baada ya sakata la Uhamiaji kilichofanyika sasa ni kwamba walichukuliwa watu woote walioomba na kuitwa kwenye hivyo written. ambao waliachwa ni wale ambao hawajakidhi vigezo vya waziwazi, hao wakawekwa kando ndio maana mnaona idadi ni kubwa.
Taarifa ya usaili ilitoka baada ya sakata la Uhamiaji kwa wenye kumbukumbu.

sasa wame hire kampuni itakayohusika na zoezi zima la kuajiri watu katika hizo nafasi TBS imejiweka pembeni. mitihani imeshaandaliwa maandalizi ya mwisho yakiwa yanafanyika huku kila paper kugongwa muhuri wa TBS kuepusha dhahama za aina yoyote....


NB: niwatakie kila la kheri mnaoenda kwenye interview kuanzia hiyo kesho hapo Yombo.

Mimi nimekosa qualification moja na wameniita mbona?
 
haihitajiki kunijua mimi, mlinzi wala mfagizi. we jiandae tu vizuri...

uliomba nafasi gani???

Ambapo sihitaj kumjua mtu ni Tanzania hii hii au?
Nliomba hr officer asee, ila uhakika wa kupata 0.09% kulingana na nafasi zilizopo ambazo ni 2 then waloitwa zaid ya 800
 
ndo huo, me nafanya hro pia...kama huamin angalia post zote mtihan kesho mda n tofaut kuanzia sa 1asbh...ndo utaelewa
 
me nili apply kwa kutumia transcript na wameniita kwenye interview

hizo mambo za kusema umetumia transcript au result slip halijaangaliwa ndugu ndio maana unaona umeitwa...

kiufupi ni karibia woote mliotuma mmeitwa walioachwa ni wachache sana
 
Kuna watu wengi sana hapa na baadhi ya ratiba zimechange.
Nafasi ya HRO wameita watu 845 lakn nafasi za Ajira ni 2 tu.
Yaani nafasi 1 inawaniwa na watu 422.
 
ni shidah jamani tupo yombo hall hapa tunasubiri hiyo pepa..nimeapply ass. accountant short list ni zaidi ya 1500 tunatakiwa 4
 
Imefika wakati sasa tuangalie upya namna ya kutengeneza ajira. Wahitimu wengi sana na kazi bado zile zile za uhamiaji, na TBS.
 
Ambapo sihitaj kumjua mtu ni Tanzania hii hii au?
Nliomba hr officer asee, ila uhakika wa kupata 0.09% kulingana na nafasi zilizopo ambazo ni 2 then waloitwa zaid ya 800

Hayo majina mnayaangalia wapi?
 
Mimi nimekosa qualification moja na wameniita mbona?

nafikiri umeitwa coz wanaamini kuwa muda wa kuapply hadi interview utakuwa umeshapata hivyo vyeti wanavyovihitaji sasa ukishindwa tena kuviwalilisha siku ya usaili basi utakuwa hujaqualify, angalizo: ni mtazamo wangu tu
 
TBS waangalie mawasiliano mtandaoni, maoni wayafanyie kazi ipasavyo. Ila uangalifu unatakiwa sana. Kutokana na shida ya kazi, hongo za aina yote zinaweza kuwa ni sehemu ya kushinda usaili na hatimaye kuajiriwa. Foreigners wana pesa na ndo wataajiriwa na WAZAWA masikini wataachwa labda Wachumba au Ndugu. Kazi kwenu Vyombo vya Dola!
 
Back
Top Bottom