TBC wanaichukulia Zanzibar kama nchi jirani

TBC wanaichukulia Zanzibar kama nchi jirani

THINKINGBEING

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2010
Posts
2,779
Reaction score
1,304
Mchungaji Mtikila alishawahi kupata misukosuko wakati fulani kwa kusema "nchi yetu iliwahi kuongozwa na rais kutoka nchi jirani ya Zanzibar". Leo katika kipindi cha NYUMBA YA JIRANI kinachorushwa na TBC wameturushia habari kutoka Rwanda na Zanzibar.Hivi TBC kama tv ya taifa ni sahihi kuiweka Zanzibar kwenye kundi la majirani?
 
Wako sawa kwa watu wanaoupenda ukweli, kilchobaki ni kiini macho,tuuu
 
Ni nchi mbili jirani zenye uhusiano mkubwa wa kidiplomasia unaoitwa Tanzania.
 
Zanzibar ni nchi? Wenyewe wanadai ni nchi sasa kuna tatizo gani tukiwa treat kama majirani?
 
ndugu yangu ni sawa kabisa kwani tanganika iliungana na Zimbabwe au hukumsikiya waziri wetu wa elimukule Africa ya kusini
 
Mchungaji Mtikila alishawahi kupata misukosuko wakati fulani kwa kusema "nchi yetu iliwahi kuongozwa na rais kutoka nchi jirani ya Zanzibar". Leo katika kipindi cha NYUMBA YA JIRANI kinachorushwa na TBC wameturushia habari kutoka Rwanda na Zanzibar.Hivi TBC kama tv ya taifa ni sahihi kuiweka Zanzibar kwenye kundi la majirani?

Channel Ten sikumbuki ni kipindi gani kile kuna mtangazaji alikuwa akimhoji Polisi mmoja badala ya kusema Tanzania Bara akawa anasema Tanganyika. Hakika kuna makanjanja wengi sana wasiojua fani ya utangazaji ni muhimu sana hata kuliko Rais Malaika.

Hata kuwepo Rais Malaika, Vyombo vya Habari vinaweza kumgeuza Rais yule akawa Ibilisi. Waandishi wa Habari wana nguvu sana katika wino wao.
 
Hata mimi naamini Zanzibar ni nchi jirani, ushahidi huu hapa, wane rais, wanayo katiba yao na wanalo Bunge, sasa hapo mnataka tbccm wasemeje? Imesemwa hivi na wahenga, ukiwa Muongo jitahidi kua na kumbukumbu.
 
Ukweli haufichiki hata kama utauficha miaka elfu,jamhuri ya watu wa zanzibar kwanza shengesha baadae.
 
Hata mimi naamini Zanzibar ni nchi jirani, ushahidi huu hapa, wane rais, wanayo katiba yao na wanalo Bunge, sasa hapo mnataka tbccm wasemeje? Imesemwa hivi na wahenga, ukiwa Muongo jitahidi kua na kumbukumbu.

Kama wana nchi mbona kila siku majukwaani wanadai nchi? Open your eyes mkuu!
 
kwani sio nchi jirani? Katiba yao si inaonyesha ni nchi? Hivyo ni majirani
 
Ni kweli hiyo ni nchi jirani AKA koloni la Tanganyika..
 
Zanzibar ni nchi? Wenyewe wanadai ni nchi sasa kuna tatizo gani tukiwa treat kama majirani?
Kwa hiyo wale wazenj waliomo serikalini tuwaite ma-expert walioazimwa kufanya kazi Tanzania Bara? Mfano, waziri wa afya mzenj wakati wizara ya afya siyo ya muungano.
 
Kweli mkuu TBC hawajakosea Zanzibar ni nchi jirani na Tanganyika. Kwamba kuna Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni viini macho tu
Ni sawa kabisa kwani hiyo ni nchi jirani kwani kule kuna ZBC
 
Ni sawa kabisa kwani hiyo ni nchi jirani kwani kule kuna ZBC
Zanzibar Broadcasting Corporation sawa sawa na Tanganyika (Tanzania) Broadcasting Corporation, na tunasahau kuwa hata namba za magari (plate numbers) zinaanzia na Z.........
 
Ni koloni letu tu, na hakuna kuliachia hawana nchi hawa msiwape ujiko
 
Na Shein ni amiri jeshi mkuu wa vikosi maalum! Hakukosea kabisa hii ni nchi sisi tunaoshi huku tunajua maana ukishuka kwenye boti unasachiwa kama unaingia marekani!hata kikwete haji kufanya ziara huku
 
Back
Top Bottom