TBC wanaichukulia Zanzibar kama nchi jirani

TBC wanaichukulia Zanzibar kama nchi jirani

"Zanzibar ni nchi ndani ya jamhuri ya muungano wa Tanzania, Zanzibar sio nchi nje ya Tanzania" kama sikosei haya ni maneno ambayo aliyasema JK baada ya waziri mkuu Pinda kusema Bungeni Zanzibar sio nchi.
 
Tbc wako sahihi zanzibar ni koloni la tanganyika,huoni hata uteuzi wa mgombea urais unafanyika tanganyika koloni letu lile.
 
Zanzibar wana rais, katiba, bendela, balaza la wawakilishi n.k, Muundo wa kiserikali kwa Zanzibar umekamilika ila japokuwa wana hivyo vigezo vyote haiwezi kuitwa nchi hata siku moja kwa kukosa kitu kimoja tu... Hawana sarafu yao! Dola ili ikamilike lazima iwe na pesa yake yenyewe ndipo itaitwa nchi. Hivyo basi siku ambayo Zanzibar wataweza kuwa na pesa yao wenyewe hapo ndipo itaitwa nchi. Otherwise itabaki kuwa kama mkoa.
 
Hata mimi naamini Zanzibar ni nchi jirani, ushahidi huu hapa, wane rais, wanayo katiba yao na wanalo Bunge, sasa hapo mnataka tbccm wasemeje? Imesemwa hivi na wahenga, ukiwa Muongo jitahidi kua na kumbukumbu.
Hivi hii sehemu ya katiba ya Jamhuri ya Muungano ya kuitambua Jamhuri inayosema "Tanzania ni nchi moja na ni jamhuri ya muungano,sehemu ya jamhuri ya muungano ni Tanzania bara na Tanzania visiwani na sehemu ya bahari inayoizunguka" imefutwa?
 
Back
Top Bottom