TBC Mnatuvunja Moyo Jamani

TBC Mnatuvunja Moyo Jamani

hp4510

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
8,245
Reaction score
8,533
Kuna mambo hiki chombo chetu cha habari kinafanya kwa kweli kinavunja moyo sana

Leo kuna swala la kimbunga huko Mtwara, serikali ya mkoa mpaka imetangaza leo watu wasiende makazini, na vyombo vikubwa vya kimataifa vyote vinaongelea swala hilo hilo la kimbunga

Cha ajabu sasa naangalia taarifa Dira ya mchana sijaona taarifa yoyote ikisema swala hilo zaidi ya taarifa za mikoa mingine

Kwa maoni yangu nilidhani hii ilipaswa kuwa taarifa ya Kwanza au hata pale chini kuwe na maandishi yanatembea ambayo yanatoa update ya mambo yanayovyokwenda
 
Kwa kumbukumbu zangu mambo yote ya aina hiyo(majanga) TBC sio kipaumbele chao.
Nakumbuka mabomu ya Mbagala,Gongolamboto,Kuzama kwa Meli kwenye mkondo wa Nungwi(MV Islander) Tetemeko la Kagera, kuzama kwa kivuko kule Ukara. Kwa uchache ..TBC inakua ya mwisho kuripoti.
Inaanza kuriport pale kiongozi fulani anapokua amekwenda eneo hilo.
TBC kipaumbele chao ni kung'arisha kazi za serikali na watendaji wake sio shida za watu.
Very Sad
 
Kwa maoni yangu nilidhani hii ilipaswa kuwa taarifa ya Kwanza au hata pale chini kuwe na maandishi yanatembea ambayo yanatoa update ya mambo yanayovyokwenda

Itaonekana baadae wazamiaji wakiwa kazini kama ilivyokuwa MV Nyerere!
 
Walipaswa kuwa Mtwara wakirusha matangazo mubashara siku nzima ya leo mpaka kimbunga kitakapopita.

Yah Coz kama wao ndio chombo cha serikali ndio inatakiwa wananchi wapate habari ya ukweli na uhakika kutoka kwao ila dah, hatari sana
 
Yah Coz kama wao ndio chombo cha serikali ndio inatakiwa wananchi wapate habari ya ukweli na uhakika kutoka kwao ila dah, hatari sana
Unaweza ona namna ambavyo tunashindwa na vitu vidogo vidogo kama hivi. Matokeo yake raia wamebaki mitandaoni wakirushiana picha za Msumbiji kwa kuwa hakuna mahali sahihi pa kuweza kupata kinachoendelea Mtwara na lindi kwa sasa.
Watu wana ndugu na jamaa zao huko na wamebaki na taharuki.
 
Kweli Madaraka matamu. nikikumbuka makala za Dr. Ryoba kwenye magazeti mbalimbali enzi hizo, sikutegemea kabisa angeshindwa kusimamia Shirika la habari kwa kiwango duni kiasi hiki........
 
Yah Coz kama wao ndio chombo cha serikali ndio inatakiwa wananchi wapate habari ya ukweli na uhakika kutoka kwao ila dah, hatari sana

Hiyo TV kazi yake ni kusifu serekali tu, haijui habari nyingine yoyote. 50%+ ya matangazo yake ni propaganda tu. Iko so outdated
 
Kwa kumbukumbu zangu mambo yote ya aina hiyo(majanga) TBC sio kipaumbele chao.
Nakumbuka mabomu ya Mbagala,Gongolamboto,Kuzama kwa Meli kwenye mkondo wa Nungwi(MV Islander) Tetemeko la Kagera, kuzama kwa kivuko kule Ukara. Kwa uchache ..TBC inakua ya mwisho kuripoti.
Inaanza kuriport pale kiongozi fulani anapokua amekwenda eneo hilo.
TBC kipaumbele chao ni kung'arisha kazi za serikali na watendaji wake sio shida za watu.
Very Sad
Umeeleza vyema mkuu, yaan wao hawataki mwananchi wa kawaida awe chanzo cha habari ni mpaka awe mkuu wa wilaya, mkoa nk
 
Tbc inakuwa live pale wapinzani wakifukuzwa bungeni au wabunge wake wakihamia ccm
 
Kuna mambo hiki chombo chetu cha habari kinafanya kwa kweli kinavunja moyo sana

Leo kuna swala la kimbunga huko Mtwara, serikali ya mkoa mpaka imetangaza leo watu wasiende makazini, na vyombo vikubwa vya kimataifa vyote vinaongelea swala hilo hilo la kimbunga

Cha ajabu sasa naangalia taarifa Dira ya mchana sijaona taarifa yoyote ikisema swala hilo zaidi ya taarifa za mikoa mingine

Kwa maoni yangu nilidhani hii ilipaswa kuwa taarifa ya Kwanza au hata pale chini kuwe na maandishi yanatembea ambayo yanatoa update ya mambo yanayovyokwenda
TBC ni wehu tu kama unajihangaisha kutegemea habari kutoka kwao utaachwa sana
 
TBC ni wapuuzi na mikamera yao uchwara kama simu za mbao za mwaka 47!!!


Picha mbovu full mchele mchele, habari za ajabu zisizovutia.

Mbaya zaidi hawataki kubadilika. Ukiwapa maoni, wanapaniki mbaya!!


Cc Dr Ryoba!
Sidhani kama kuna mtangazaji wa hiyo channel anaweza kwenda tv station nyingine akaweza kufanya kazi za kiushindani
 
Mkuu bdo unasumbukaga tu na hao TBC wenzako tushawakimbia muda mrefu sanaaaa, angalia BBC News ama Aljazeera mkuu.
Jamaa wana tia mihasira sana alafu hawashauriki
 
Back
Top Bottom