TBC Mnakera sana!

Hivi hili haliwezi kuleta mkanganyiko hususani wa kimaadili ya vyombo vya habari?...

Maana kwa tafsiri ya haraka ni kuwa Star TV imetumika kuiponda TBC, hata kama Ndg Machali kaeleza ukweli

Machali ametoa maoni yake, na kwa vyovyote si maoni ya STAR TV. Hata hao wasimamizi wa maadili ya vyombo vya habari wanajuakuwa TBC wana TABIA MBAYA.
 
TBC ni tarumbeta refuuuu wapulizaji wapo Magogoni.
 
Anataka kualikwa akatie shombo? Kama mtu haipendi TBC1 asiangalie
 
Swali la kujiuliza hivi ni kwanini TBC1 wanakwepa kuwakaribisha wazungumzaji wenye mitazamo tofauti (Wanaotaka serikali 2 v wanaotaka serikali 3). Je ni kweli kwamba TBC1 wameshagundua kwamba wanaotaka serikali 2 hawa HOJA bali VIOJA, hivyo kuwashindanisha kwa HOJA na wanaotaka serikali 3 itakuwa ni kumvua nguo MFALME? Hivi katika zama hizi za TEHAMA ki/viongozi wanaweza kuficha UDHAIFU wao kwa njia hii? Just thinking aloud
 
Hivi hili haliwezi kuleta mkanganyiko hususani wa kimaadili ya vyombo vya habari?...

Maana kwa tafsiri ya haraka ni kuwa Star TV imetumika kuiponda TBC, hata kama Ndg Machali kaeleza ukweli
Acha uzushi wewe!Tena mtangazaji alifanya juhudi kumkatisha Machali asiendelee kuiponda TBC lakini Machali alikomaa.
 
JAMANI INAITWA TBC-CCM; TBC AMEONDOKA NAYO TIDO MHANDO SIKU NYINGI SANA,mm tbc naifungua kulitazama bunge tu baada ya hapo nahamia ITV,ila kuna taarifa kuwa hujuma hizo hazina tija mbele ya maoni ya wananchi maana huo ndio msingi wa katiba duniani kote
 

Kila chombo na idara ya serikali hapa nchini kinatumika kisiasa....
Na kwa miaka mingi sasa CCM wamekuwa wakitumia muungano kisiasa vile vile!
 

CCM daima ni waoga kuukabili ukweli!
Hawapendi wapingwe hata kama wanapotosha....
Hili halijaanza leo... fuatilia hata kwenye midahalo mbali mbali
Wakijua kuna hoja nzito zinapingana na zao basi wanaingia mitini! (Ref: Kikwete, mchakato majimboni, BMK, n.k)
 
Acha uzushi wewe!Tena mtangazaji alifanya juhudi kumkatisha Machali asiendelee kuiponda TBC lakini Machali alikomaa.

Sasa hapo uzushi wangu upo wapi?

Pamoja na ubaya wote wa TBC lakini mtu au taasisi ikikiuka ethics tukae kimya na kutokumueleza?

Kutumia chombo fulani cha habari kukikandia chombo kingine cha habari tena vilivyo katika kada moja sio maadili sahihi na hata sheria inaweza kutumika kushtakiana...
 

Ndugu yangu jambo hilo haliitaji elimu ya chuo kikuu, TBC ni chombo cha serikali, serikali iliyopo madarakani inataka muungano wa serikali mbili, hivi kweli hata kama ungekuwa wewe ungeleta watu wanaounga mkono serikali tatu kwa ajili ya kupiga propaganda hiyo? sual la kuwa tbc inaendeshwa kwa kodi za wananchi ni kweli kabisa lakini utambuzi huo si kwa TANZANIA ambayo Rais na makame wake wanashiriki kampeni za uchaguzi mdogo kwa gharama za kodi za wananchi wakati chama chao kina fedha magari na kila uwezo wa kutumi raslimali za chama kufanikisha kampeni zao.
 

Labda CCM ya miaka hii ndiyo imekuwa OGA ya kukimbia midahalo yenye HOJA na KUFIKIRISHA akili. Mbona Nyerere alikuwa anakuja Nkrumah Hall (UDSM) na kutukabiri kwa hoja na sometimes kututoa nock out! Mbona BW Mkapa 1995 alimkabiri Mrema kwenye mdahalo wa wazi wa president candidates na kumpiga nock out Mrema!
 
Hivi si unafahamu kuwa kuna Uhariri wa habari?

Umenishangaza kwa kiwango kikubwa! Wewe ulitaka "mhariri" aingie kichwani mwa Mh. Machali na kumkataza asiseme alichosema? Jamani tusiwe wepesi wa ku-criticize bila kutafakari hoja za wenzetu!
 
Umenishangaza kwa kiwango kikubwa! Wewe ulitaka "mhariri" aingie kichwani mwa Mh. Machali na kumkataza asiseme alichosema? Jamani tusiwe wepesi wa ku-criticize bila kutafakari hoja za wenzetu!

Kama ni live coverage mwandishi anayefanya mahojiano huwa anaomba radhi moja kwa moja na wakati huo huo anatoa angalizo kwa yule anayemuhoji...

Hapa si suala la kufanya criticism bali ni kuelezana ukweli, hizi thics zipo na zimeandikwa ni suala la kukumbushana tu...

Ndio hatuipendi TBC kwa kuwa inatumiwa na serikali kama ilivyo magazeti ya Uhuru nk lakini tusisahau katika kukosoa tujaribu kujenga hoja...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…