MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 710
Habari nilizozipata hivi punde zinaeleza kwamba majengo ya Shirika la Utangazaji Tanzania (Tanzania Broadcasting Corporation) yaliyopo Mikochen, Barabara ya Ali H. Mwinyi, yamebadilishwa muonekano wake kwa nje.
"Kama unafika pale kwa mara ya kwanza unaweza kudhani umepotea kwani hakuna hata kabango kadogo kenye nembo ya TBC", kilisema chanzo cha habari hizi na kusema habari zaidi zitapatikana pamoja na ushahidi wa picha.
Itakumbukwa kwamba jengo la Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia liliwahi kupakwa rangi ambayo ilikuwa mchoro wa nembo ya kampuni ya simu ya Vodacom, jambo ambalo liliweka taswira mbaya mbele ya jamii.
Lakini hili la Startimes linaashiria kuvuka mipaka ya uvumilivu, kwani linaitambulisha TBC kuwa ni ama kampuni tanzu ya Startimes au ndio Startimes yenyewe.
Haiyumkini uongozi wa TBC ulikuwa katika hali gani kukubali jengo lake kubatizwa jina la Startimes na utambulisho wote wa TBC kuondolewa.
Je, walighafilika?
Tutazidi kuwaletea habari zaidi za tukio hili.
"Kama unafika pale kwa mara ya kwanza unaweza kudhani umepotea kwani hakuna hata kabango kadogo kenye nembo ya TBC", kilisema chanzo cha habari hizi na kusema habari zaidi zitapatikana pamoja na ushahidi wa picha.
Itakumbukwa kwamba jengo la Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia liliwahi kupakwa rangi ambayo ilikuwa mchoro wa nembo ya kampuni ya simu ya Vodacom, jambo ambalo liliweka taswira mbaya mbele ya jamii.
Lakini hili la Startimes linaashiria kuvuka mipaka ya uvumilivu, kwani linaitambulisha TBC kuwa ni ama kampuni tanzu ya Startimes au ndio Startimes yenyewe.
Haiyumkini uongozi wa TBC ulikuwa katika hali gani kukubali jengo lake kubatizwa jina la Startimes na utambulisho wote wa TBC kuondolewa.
Je, walighafilika?
Tutazidi kuwaletea habari zaidi za tukio hili.