East African
JF-Expert Member
- Nov 27, 2013
- 704
- 989
Ndugu wana JF wananchi wengi wamekuwa na maswali ni jinsi gani serikali itaweza kuendesha mfumo wa serikali tatu.
huu ni mchanganuo nilioufanya na kuona kuwa serikali tatu sio mzigo mkubwa hata kidogo;
1. Bunge la sasa la Jamhuri ya Muungano Tanzania lina wabunge takribani 350 ikiwa ni pamoja na wazanzibar 55 + 189 ya majimbo ya bara+ kumi wa Rais+ viti maalum zaidi ya 90. Hivyo kama katiba mpya itakubalika maana yake ni kuwa;
a) hakutakuwa na wabunge 55 tena kutoka Zanzibar na hivyo JMT itakuwa na wabunge 75. kwa maana hiyo napendekeza Tanganyika iwe na wabunge 189 wa majimbo+61 ya viti maalum na kufanya jumla ya wabunge 250 tu wa bunge la Tanganyika. hivyo kupunguza mzigo wa wabunge karibu 100 ambao fedha zao zitahamishiwa serikali ya Muungano.
b. bunge la JMT litakuwa na wabunge 75 ambao 20 watatoka Zanzibar na 50 watatoka Tanganyika na 5 watateuliwa na Rais.Ikumbukwe kuwa bunge hili halitakuwa na shughuli nyingi kwani litakuwa na wizara chini 10 na ikumbukwe kuwa serikali ya JMT haitashughulika na masuala yeyote ya shughuli za maendeleo zaidi ya shughuli za utawala za mambo saba ya JMT.
2. Mambo ya muungano yamependekezwa yawe 7 hivyo nashauri mawaziri wa JMT wawe saba tu na ma naibu angalau wanne hivi ili kupunguza mzigo na hasa ukizingatia kuwa wizara za JMT hazitakuwa na kazi nyingi kama ilivyo sasa.
3. Napendekeza kuwa ofisi za wizara hizi saba zinaweza kuwa na wafanyakazi walau wasizidi 100 lika wizara na wizara zote ziwe katika jengo moja kubwa walau la ghorofa 5 au kumi hivi linaweza kubeba wizara zote hizi na kupunguza safari. kwa maana hiyo serikali ya Tanganyika inaweza kutoa jengo moja la wizara linaloweza kutumiwa na ofisi zote za serikali ya JMT. mfano lile jengo la Nishati na madini pale Ohio linaweza kubeba wizara zote za JMT.
4. Taasisi kama mahakama, msajili wa vyama vya siasa na maadili ya uongozi wa umma zitaendelea kuwapo kama ilivyo sasa hakutakuwa na gharama za ziada.Ikumbukwe kuwa mahakama inaweza kupewa jengo moja tu kwani hawatakuwa na kesi nyingi maana mambo ya muungano yamepunguzwa sana hadi kufikia 7 tuu.
5. Gharama mpya zinazojitokeza hapo ni Rais na makamu wa rais ambao wao watajengewa ikulu mpya eneo lingine na gharama zao zitabebwa na nchi washirika.
6. Kwa haraka haraka naonna kiasi cha shilingi bilioni 200 kinatosha kuendesha serikali ya muungano ukiondoa gharama za uendeshaji wa wizara za ulinzi na polisi. Nasema hivi kwa kuwa serikali ya zanzibar kwa sasa bajeti yao ya nchi nzima pamoja na shughuli za maendeleo ni takribani Bilioni 400 hivi hivyo kwa serikali pekee ya JMT yenye mawaziri chini ya 15 na mahakama ya juu na msajili wa vyama inatosha kabisa.
7. Pia napendekeza kuwa ili kuondoa mkanganyiko wa kiutawala serikali ya Zanzibar na Tanganyika ziongozwe na mawaziri wakuu wenye mamlaka katika serikali zao na wapatikane kwa kupigiwa kura.
8. Upande wa Tanganyika napendekeza kupunguza idadi ya wizara kutoka 29 za sasa na kuwa walau 17 au 20 hivi na kwa maana hiyo tutakuwa tumepunguza mawaziri na manaibu mawaziri zaidi ya 20 na gharama zao kuhamishiwa ktk shughuli za maendeleo.
Huu ni mchanganuo wangu kama mtanzania naomba na ninyi murekebishe au muongezee maeneo ambayo sijagusia.
huu ni mchanganuo nilioufanya na kuona kuwa serikali tatu sio mzigo mkubwa hata kidogo;
1. Bunge la sasa la Jamhuri ya Muungano Tanzania lina wabunge takribani 350 ikiwa ni pamoja na wazanzibar 55 + 189 ya majimbo ya bara+ kumi wa Rais+ viti maalum zaidi ya 90. Hivyo kama katiba mpya itakubalika maana yake ni kuwa;
a) hakutakuwa na wabunge 55 tena kutoka Zanzibar na hivyo JMT itakuwa na wabunge 75. kwa maana hiyo napendekeza Tanganyika iwe na wabunge 189 wa majimbo+61 ya viti maalum na kufanya jumla ya wabunge 250 tu wa bunge la Tanganyika. hivyo kupunguza mzigo wa wabunge karibu 100 ambao fedha zao zitahamishiwa serikali ya Muungano.
b. bunge la JMT litakuwa na wabunge 75 ambao 20 watatoka Zanzibar na 50 watatoka Tanganyika na 5 watateuliwa na Rais.Ikumbukwe kuwa bunge hili halitakuwa na shughuli nyingi kwani litakuwa na wizara chini 10 na ikumbukwe kuwa serikali ya JMT haitashughulika na masuala yeyote ya shughuli za maendeleo zaidi ya shughuli za utawala za mambo saba ya JMT.
2. Mambo ya muungano yamependekezwa yawe 7 hivyo nashauri mawaziri wa JMT wawe saba tu na ma naibu angalau wanne hivi ili kupunguza mzigo na hasa ukizingatia kuwa wizara za JMT hazitakuwa na kazi nyingi kama ilivyo sasa.
3. Napendekeza kuwa ofisi za wizara hizi saba zinaweza kuwa na wafanyakazi walau wasizidi 100 lika wizara na wizara zote ziwe katika jengo moja kubwa walau la ghorofa 5 au kumi hivi linaweza kubeba wizara zote hizi na kupunguza safari. kwa maana hiyo serikali ya Tanganyika inaweza kutoa jengo moja la wizara linaloweza kutumiwa na ofisi zote za serikali ya JMT. mfano lile jengo la Nishati na madini pale Ohio linaweza kubeba wizara zote za JMT.
4. Taasisi kama mahakama, msajili wa vyama vya siasa na maadili ya uongozi wa umma zitaendelea kuwapo kama ilivyo sasa hakutakuwa na gharama za ziada.Ikumbukwe kuwa mahakama inaweza kupewa jengo moja tu kwani hawatakuwa na kesi nyingi maana mambo ya muungano yamepunguzwa sana hadi kufikia 7 tuu.
5. Gharama mpya zinazojitokeza hapo ni Rais na makamu wa rais ambao wao watajengewa ikulu mpya eneo lingine na gharama zao zitabebwa na nchi washirika.
6. Kwa haraka haraka naonna kiasi cha shilingi bilioni 200 kinatosha kuendesha serikali ya muungano ukiondoa gharama za uendeshaji wa wizara za ulinzi na polisi. Nasema hivi kwa kuwa serikali ya zanzibar kwa sasa bajeti yao ya nchi nzima pamoja na shughuli za maendeleo ni takribani Bilioni 400 hivi hivyo kwa serikali pekee ya JMT yenye mawaziri chini ya 15 na mahakama ya juu na msajili wa vyama inatosha kabisa.
7. Pia napendekeza kuwa ili kuondoa mkanganyiko wa kiutawala serikali ya Zanzibar na Tanganyika ziongozwe na mawaziri wakuu wenye mamlaka katika serikali zao na wapatikane kwa kupigiwa kura.
8. Upande wa Tanganyika napendekeza kupunguza idadi ya wizara kutoka 29 za sasa na kuwa walau 17 au 20 hivi na kwa maana hiyo tutakuwa tumepunguza mawaziri na manaibu mawaziri zaidi ya 20 na gharama zao kuhamishiwa ktk shughuli za maendeleo.
Huu ni mchanganuo wangu kama mtanzania naomba na ninyi murekebishe au muongezee maeneo ambayo sijagusia.