Tax on Salary goes down from 15% to 14%. Is it Significant enough?

Hawezi kuzikamilisha sasa, labda aseme hata ahidi tena ili azitekeleze awamu ijayo akichaguliwa. Mfano aliahidi umeme wa grid ya Taifa katika maeneo yanayotumia generators mfano Songea. hata kwenye ilani ya CCM utasoma hilo lakini hakuna alichofanya, hata nguzo moja haijachimbiwa wala kuangushwa barabarani toka Makambako kwenda Songea. hata bajeti hii sidhani kama kuna suala la kupeleka umeme huo.

Mkapa aliahidi kuunganisha mikoa ya kusini na kaskazini kwa barabara, alikuwa akikampain Kikwete aliahidi kuendeleza mradi huo mfano barabara ya Mtwara corridor.Toka aingie madarakani mradi huo ndiyo umekufa hata zile file za upembuzi yakinifu uliofanywa kipindi cha Mkapa upo kwenye mafile tu yanapata kutu.

Kikwete aliahidi mambo mengi yanayohitaji gharama kubwa hajatekeleza kabisa, anapiga domo tu.
 
NISHATI
MUHTASARI WA ILANI YA UCHAGUZI YA 43.
(b) Kufikisha umeme katika miji mikuu ya Wilaya za Bukombe, Kilindi, Simanjiro, Kibondo, Kasulu, Mbinga na Tunduru na kuanza hatua za kuipatia umeme miji mikuu ya Wilaya nyingine mpya.
(c) Kuongeza kasi ya kupeleka umeme vijijini kupitia Mfuko wa Nishati Vijijini utakaoshirikisha sekta binafsi na wahisani.
(d) Kuweka mkakati wa uzalishaji umeme wa kutosha na wa gharama nafuu zaidi kwa lengo la kuongeza ufanisi viwandani.
(e) Kuiunganisha Mikoa ya Kigoma na Ruvuma na gridi ya Taifa.
(f) Kuendelea kutafuta wawekezaji wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza.
(g) Kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi katika uzalishaji na usambazaji wa umeme.
(h) Kuendelea kutafuta mafuta kwa kasi zaidi.
(i) Kuanzisha mradi wa gesi kwa matumizi ya nyumbani kutokana na gesi ya Songosongo kwa lengo la kupunguza matumizi ya kuni na mkaa majumbani.
lipi limetekelezwa katika haya? Lipi limewekwa kwenye bajeti hii?
 
MUHTASARI WA ILANI YA UCHAGUZI YA Barabara
(c) Kuendelea kuimarisha barabara nchini zitakazounganisha nchi yetu na nchi jirani kwa barabara za lami; zitakazounganisha Makao Makuu ya Mikoa yote pia kwa barabara za lami na kuunganisha Makao Makuu ya Wilaya zote kwa barabara zinazopitika wakati wote;
(d) Kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara zifuatazo:-
Tunduma-Sumbawanga;Marangu-Tarakea-Rongai; Minjingu-Babati-Singida; Rujewa-Madibira-Mafinga; Mbeya-Chunya-Makongolosi; Msimba-Ikokoto-Mafinga; Arusha-Namanga; Tanga-Horohoro; na ukarabati wa Barabara ya Kilwa (DSM), Barabara ya Mandela (DSM) na Barabara ya Sam Nujoma (DSM).
(e) Kuzifanyia upembuzi yakinifu na usanifu barabara zifuatazo kwa ajili ya kujengwa kwa kiwango cha lami: Maganzo-Maswa-Bariadi-Mkula-Lamadi; Babati-Dodoma-Iringa; Sumbawanga-Kigoma-Nyakanazi; Musoma-Fort-Ikoma; Korogwe-Handeni-Kilosa-Mikumi; Nzega-Tabora-Sikonge-Chunya; Mtwara-Masasi-Songea-Mbamba Bay; MUHTASARI WA ILANI YA UCHAGUZI YA Manyoni-Itigi-Tabora; Ipole-Mpanda-Kigoma na Bagamoyo-Saadani.

(f) Kuhimiza maandalizi na ujenzi wa Daraja la Kigamboni chini ya uongozi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ili kuunganisha Kigamboni na Jiji la Dar es Salaam;
(g) Kuhakikisha upatikanaji wa kivuko kipya cha Kigongo-Busisi (Mwanza);
(h) Kukamilisha ujenzi wa daraja jipya la Mpiji ambalo litawezesha njia mbadala ya Dar es Salaam-Tanga.
(i) Kufanya upembuzi yakinifu, usanifu na ujenzi wa daraja la Mto Kilombero na kukamilisha ujenzi wa daraja la Mto Mwatisi katika Mkoa wa Morogoro.
(j) Kufanya usanifu wa daraja jipya la Ruvu;
(k) Kuendelea kuandaa mazingira mazuri ya kuishirikisha sekta binafsi katika ujenzi na matengenezo ya barabara kwa kutumia mfumo wa Jenga, Endesha na Kabidhi (BOT).
(l) Kuanza ujenzi wa Daraja la Umoja (Tanzania na Msumbiji).
(m) Kuanzishwa Programu ya Taifa ya Usafiri Vijijini.



Nini kimefanyika katika haya? je bajeti hii itakamilisha haya?
 
(a) Kuendelea kuliimarisha Shirika la Reli Tanzania (TRC) kwa lengo la kulipa uwezo wa kutoa huduma bora kwa bidhaa na abiria wa ndani na wa nchi jirani. Pia, Shirika litaendelezwa kama muhimili wa mpango wa maendeleo wa eneo la Ukanda wa Kati.
(b) Kuendelea kuliimarisha Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) ili liweze kuhimili kwa uwezo mkubwa zaidii majukumu ya kuboresha huduma kwa bidhaa na abiria na kusaidia shughuli za uendelezaji wa mpango wa eneo la Ukanda wa Mtwara.
(c) Kuendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa reli mpya za Arusha-Musoma, Isaka-Kigali na eneo la Ukanda wa Mtwara ambayo itaunganisha Bandari ya Mtwara, Songea, Mbamba Bay, Mchuchuma na Liganga.
(d) Kuimarisha Bandari za Kigoma na Kasanga. (g) Kukamilisha ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe na kuimarisha Viwanja vya Ndege vya Kigoma, Tabora na Shinyanga.
(h) Kutekeleza mradi wa mabasi ya usafiri wa haraka jijini Dar es Salaam.

Na haya tena!
 
Ahadi kuu kuliko zote na ambayo haijatekelezwa hata kwa 1% ni ya kuleta "Maisha Bora kwa Kila Mtanzania!"
 
(a) Kuwawezesha wananchi mijini na vijijini kupata maji safi, salama na ya kutosha kwa matumizi yao ya kawaida karibu na sehemu wanazoishi na kwa mahitaji ya kiuchumi. Lengo ni kuwafikishia huduma hiyo asilimia 90 ya wakaazi wa mijini na asilimia 65 ya wakaazi wa vijijini ifikapo mwaka 2010.
(d) Kukamilisha miradi mikubwa ya maji ambayo ni pamoja na Mradi wa Maji toka Ziwa Victoria kwenda Wilaya za Shinyanga Mjini na Kahama, Mradi wa Maji wa Chalinze katika Mkoa wa Pwani na Mradi Kabambe wa Kufufua Mifumo ya Maji Safi na Maji Taka Katika Jiji la Dar es Salaam.

Naomba wanaCCM mlete maelezo Serikali ya CCM imefanya nini kutimiza ahadi zake. 2010 ndiyo hii, je? 90%mijini na 65% vijijini wamepata maji safi?
 
Kawakebehi wafanyakazi na kura zao....jana alikuwa anaombaomba kura za wanafunzi Dodoma........kazi kwelikweli
 
Ahadi kuu kuliko zote na ambayo haijatekelezwa hata kwa 1% ni ya kuleta "Maisha Bora kwa Kila Mtanzania!"

ili tuweze kuwapata vizuri tuanze na hizo ndogondogo. Nauliza wamefanya nini? mbona ukisoma ilani sioni walichofanya? kama kipo is not promising at all. Nakumbuka maneno ya Steve Biko (cry freedom) dhidi ya Serikali ya makaburu alipoulizwa 'hakuna kizuri kilicgofanya na Serikali?'
 
Kuhamia Makao Makuu Dodoma
125. CCM itaendelea kusisitiza na kusimamia utekelezaji wa uamuzi wa kuhamishia Dodoma Makao Makuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika kipindi cha 2005-2010, hatua zifuatazo zitachukuliwa kwa lengo la kuzidisha kasi ya kuhamia Dodoma:-
(a) Kutunga sheria ya kuitambua rasmi Dodoma kuwa Makao Makuu ya Serikali na kuweka utaratibu wa Serikali kuhamia huko.
(b) Kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Iringa-Dodoma-Arusha na kukamilisha ujenzi wa barabara ya Dar es Salaam-Dodoma-Mwanza kama mkakati wa kuendeleza mji wa Dodoma ili uweze kuvutia vitega uchumi.
(c) Kuweka vivutio kwa sekta binafsi ili ishiriki katika uwekezaji kwenye ujenzi wa miundombinu inayohitajika katika ukuaji wa mji, na katika uwekaji wa huduma mbali mbali zinazokidhi mahitaji ya watumishi wa Serikali na wananchi kwa jumla.
(d) Kuongeza kasi ya Wizara za Serikali kuhamia Dodoma, kwa kuwa sasa Serikali inajenga nyumba nyingi za kuishi watumishi.

Chama kilichojaa porojo, CCM
 
near to zero achievement na bado wanatudanganya. naomba magazeti yaandike hizi ahadi ili kila mtu aone kwa macho yake.
 
Chama kilichojaa porojo, CCM
Kuhamia Makao Makuu Dodoma
125. CCM itaendelea kusisitiza na kusimamia utekelezaji wa uamuzi wa kuhamishia Dodoma Makao Makuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika kipindi cha 2005-2010, hatua zifuatazo zitachukuliwa kwa lengo la kuzidisha kasi ya kuhamia Dodoma:-
(a) Kutunga sheria ya kuitambua rasmi Dodoma kuwa Makao Makuu ya Serikali na kuweka utaratibu wa Serikali kuhamia huko.


Teh teh ati kuhamia Dodoma kwanza ni ndoto,

Cha kustahajabisha ni huku wakifikiria kuhamia Dom huku wakati hapo walipo tuuu niwakumbusheni Ule mpango wa kujenga Fly Overz Road zao za Dar kwa taarifa yenu huo mradi upo na umedhaminiwa na serikali ya Japan mkae mjue ivyo sasa niambieni hiyo Dom itakuwepo katika hizo ndoto na porojo zao??

Badala ya kutupa hizo fund kwenda Dom na kuukarabati mji wa Dom na kupunguza purukushani Dar hawataki kabisa hii ni jinsi gani viongozi wetu wa serikali,CCM,manicpl, na wengineo wanao husika na mikakti ya mipango miji walivyo na upeo mchache kabisa kwa Karne hii,

Huyo Kimbisa na kuwa katoke Dom hata kushadadia na kupiga hata porojo za hapa na pale wahamishie hizo Fund Dom walaaa yeye kakaa na kuwazi kupata ubunge Dom Mjini na atangojea sana kama watu wa kondoa hawamtakiiii tuuu sijui, yaaani ni taaaabu kweli kweli.
 
Re: anaepinga apinge tu lkn Ahadi za Jk kutimia: Bajeti 2010/11 mishahara juu

Huyu MS ni wa kusamehewa tu hajui atendalo.
 
Well huu ndio usanii tunaosemaga kila siku walichokifanya ni kutoa na kujumlisha wamepunguza tax kwa minimum wage but wanawaongezea tax kwenye VAT hivyo wanatoa huku wanachukua kule. Mbaya zaidi wameongeza kodi zaidi ya PAYE kuzidi kuwanyonya wafanyakazi. Halafu kuna watu wanadai JK ametimiza ahadi ya kuongeza mshahara mie nawashangaa sana wamesahau ile kodi 15%-14% inawahusu wafanyakazi wenye kima cha chini. Hapo hapo wanasema waziri wa utumishi atatangaza kupandisha mishahara. Tuassume tuna wafanyakazi 20% ni minimum wage wakipandisha mshahara hao wanaoqualify minimum wage ni wangapi? na chukulia mfano mtu alikuwa akipata 150,000 na hakuwa akikatwa kodi, ukimuongezea hadi 350,000 halafu unachukua 30% ya mshahara wake huku kuna makato mengine nayo yanaongezeka je umemuongezea mshahara??.

Kimsingi mie naona hili swala la kodi kwa watumishi liangaliwe upya. Vitafutwe vyanzo vipya vya kodi badala ya kuendelea kumnyonya mtumishi wa serikali kwakuwa ni njia rahisi ya kuongeza mapato. Otherwise, ni kuwaonea watumishi tu.
 
Back
Top Bottom