Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,307
- 33,925
Yaani hivi sasa CCM hapa Iringa wako bize kupambana na Peter Msigwa Mbunge wa Iringa mjini. Yaani harakati zao ukiziangalia wakati mwingine ni kama vile wamepata wazimu.
Jimbo la Iringa mjini limeshawahi siku za nyuma kuongozwa na Mfalamagoha Kibasa toka NCCR- Mageuzi wakati huo kwa miaka mitano 1995-2000 na baada ya hapo CCM kupitia kwa Monica Mbega ikaongoza kwa miaka kumi 2000 - 2010 alipochukua Msigwa.
CCM wanajifaragua kwamba kuchaguliwa kwa Msigwa kunatokana na makosa yao wenyewe lakini wanajisahaulisha kwamba Iringa walishawahi kuwakataa mwaka 1995. Iringa kuikataa CCM hakutokani na Msigwa hata kama yeye ni sehemu ya kichocheo cha kukataliwa kwa CCM kwani CCM kukataliwa Iringa ni Historia ya tangu mwaka 1995.
Msigwa mwaka 2015 alimpita mpinzani wake David Mwakalebela kwa zaidi ya kura elfu kumi kwa kupata kura 43, 154 dhidi ya kura 32,406 za Mwakalebela. Ukiangalia tofauti ya kura hizo zaidi ya elfu kumi utagundua kwamba ni wana Iringa ndiyo waliikataa CCM na si Msigwa peke yake.
CCM wanatafuta sababu zisizo na mashiko kumdhuru Msigwa kibinafsi na wala si kupambana naye kisiasa. Udhaifu wa CCM Iringa ni mkubwa kiasi kwamba haiwezekani bila ya dola kushinda uchaguzi wa Ubunge mwaka 2020.
Jimbo la Iringa mjini limeshawahi siku za nyuma kuongozwa na Mfalamagoha Kibasa toka NCCR- Mageuzi wakati huo kwa miaka mitano 1995-2000 na baada ya hapo CCM kupitia kwa Monica Mbega ikaongoza kwa miaka kumi 2000 - 2010 alipochukua Msigwa.
CCM wanajifaragua kwamba kuchaguliwa kwa Msigwa kunatokana na makosa yao wenyewe lakini wanajisahaulisha kwamba Iringa walishawahi kuwakataa mwaka 1995. Iringa kuikataa CCM hakutokani na Msigwa hata kama yeye ni sehemu ya kichocheo cha kukataliwa kwa CCM kwani CCM kukataliwa Iringa ni Historia ya tangu mwaka 1995.
Msigwa mwaka 2015 alimpita mpinzani wake David Mwakalebela kwa zaidi ya kura elfu kumi kwa kupata kura 43, 154 dhidi ya kura 32,406 za Mwakalebela. Ukiangalia tofauti ya kura hizo zaidi ya elfu kumi utagundua kwamba ni wana Iringa ndiyo waliikataa CCM na si Msigwa peke yake.
CCM wanatafuta sababu zisizo na mashiko kumdhuru Msigwa kibinafsi na wala si kupambana naye kisiasa. Udhaifu wa CCM Iringa ni mkubwa kiasi kwamba haiwezekani bila ya dola kushinda uchaguzi wa Ubunge mwaka 2020.