Tatizo Ni Mume Au Mtoto?

Tatizo Ni Mume Au Mtoto?

Joined
May 10, 2017
Posts
5
Reaction score
0
Nimemuoa Mwanamke Aliye Na Mtoto Wa Miaka 8, Dogo Ameleta Shida Ana Kiburi Hadi Ukimuongelesha Analia Tu Ovyo Kila Mara...,ukimtuma Haendi Nikiuliza Naambiwa Eti Ni Mtoto Mchanga...Nmechanganyikiwa Nashindwa Kuelewa Nimuache Mke Au Nifanyeje, Naitaji Msaada Wenu Wakuu
 
Msaada gani unahitaji?

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Haya Ndio madhara ya kuoa single mothers maana dhamira yako na yake Pamoja kimapenz ila tofauti kimawazo pole sana mkuu
Ushaur wangu ni kuwa amua kuwa mwanaume ndani ya nyumba kama unayo fanya kwake ni Mazur Weka maamzi na Msimamo atakuelewa na atabadilika Yeye Pamoja na mwanae

Kama atagoma kubadilika Weka Msimamo kama mwanaume Mwambie sheria za ndani kwako akiona zinaendana na Yeye azifate akiona hazimfai Mwambie maisha bado yanawezekana hivyo achague furaha yake Iko wapi maana naamni asilimia Mia huyo mtoto ana jazwa Kiburi na mama ake

NB: fata Ushauri wangu kama wewe ndie kichwa cha family ila kama wewe ni marioo Endelea kuwa mvulana ndani kwako
 
Nimemuoa Mwanamke Aliye Na Mtoto Wa Miaka 8, Dogo Ameleta Shida Ana Kiburi Hadi Ukimuongelesha Analia Tu Ovyo Kila Mara...,ukimtuma Haendi Nikiuliza Naambiwa Eti Ni Mtoto Mchanga...Nmechanganyikiwa Nashindwa Kuelewa Nimuache Mke Au Nifanyeje, Naitaji Msaada Wenu Wakuu

Huyo mtoto alidekezwa kupita kiasi mama yake alimfanya yai na pia huyo mama akili hana, mwambie muungane pamoja mtumie njia nzuri za kisaikolojia kumshape mtoto kwa manufaa ya mtoto akikua baadae.

Kwakuwa mama ndiye alikuwa naye mda mrefu aanze yeye kumuelewesha mtoto kuwa hapendezwi na tabia yake.
Tumieni rewarding, mpe moyo akifanya jambo jema linalokupendeza.

Hebu fanya vitu unavyopenda akufanyie kwani watoto huiga zaidi ya kuambia maneno mengi mfano mfundishe asante, pole, samahani kwanza.

Kikubwa mjengee urafiki mkubwa ndani ya mwezi mmoja kwanza halafu akishakuwa karibu na wewe tumia hiyo nafasi kumwambia ujue nikikutuma huendi wewe ni mtoto mbaya, Ukiwa mkubwa utakosa marafiki n.k ataogopa kumuumiza rafiki yake atabadilika miezi 2 tu hutaamini.
Sali naye kula naye, mpe zawadi with resoan za kumpongeza ukiwa kazini piga simu uongee naye
 
Nasikitika sana jombaa maana ukishindwa kuidhibiti tabia ya mtoto mpka kufikish miaka nane bas tena hapo kumgeuza ni kaz kwel kwel,itakuchukua miaka nane mingine kumweka sawa nae akaelewa,

Na umesahau mtoto ajifunzi anavyosikia bali anajifunza anavyoshuhudia,so anashuhudia nn kwenu?? Tatzo weng wanaokujaga kuomba ushauri huku naona wanaelezea tu mabaya ya mwenzake na hawasem tabia yao halis,huo ni msalaba wako,komaa nao uunyooshe kama Sizonje anavyotunyoosha,japo tumekua wabish lakin tunannyooka mdogo mdogo.
 
Amkalishe mtoto chini na aweke boundaries Huyu mtoto alishzoeshwa kujiona yeye ndiye mwanaume kwenye maisha ya mama yake. Hapo una onewa wivu wewe kuingilia mapenzi yake na mama yake, kwakifupi anakuchukia. Dawa ya chuki ni upendo, mpeleke cinema mkiwa nyinyi wawili bila mama yake na kuangalia mpira, kula ice cream jitahidi kuwa na man to man bound na mtoto
 
Nasikitika sana jombaa maana ukishindwa kuidhibiti tabia ya mtoto mpka kufikish miaka nane bas tena hapo kumgeuza ni kaz kwel kwel,itakuchukua miaka nane mingine kumweka sawa nae akaelewa,

Na umesahau mtoto ajifunzi anavyosikia bali anajifunza anavyoshuhudia,so anashuhudia nn kwenu?? Tatzo weng wanaokujaga kuomba ushauri huku naona wanaelezea tu mabaya ya mwenzake na hawasem tabia yao halis,huo ni msalaba wako,komaa nao uunyooshe kama Sizonje anavyotunyoosha,japo tumekua wabish lakin tunannyooka mdogo mdogo.

Usimkatishe tamaa, mwanadamu hukua kila siku samaki mbichi sana huyo. Nilikaa na watoto wa kiume 2 wa sekondari niliamua kuwanyoosha walinyooka from cruel kwao to atleast hard working and obedient.

Halafu sio tu kwakuwa ni mtoto wa mke tunaishi na watoto majumbani wako na baba na mama mzazi ila wanatisha ni panya road vibaka, n.k Tuviombee vizazi vyetu na watoto wetu.
 
khaa! .sasa angalia umeoa juz tu una anza kuwaza mtoto hata hujatulia kwenye ndoa. mnavo oa kuweni makini jaman khaa!
huyo dogo asha shindikana, halaf angekuwa wako ningesema umtie fimbo hadi akome ila ndio hvo tena hakuna namna jikaze naye tuu.
 
Back
Top Bottom