Tatizo lipo kwetu Waafrika, si kwa Mataifa ya Magharibi

KAYGREKO

Member
Jan 18, 2013
37
32
TATIZO LIPO KWETU SI KWAO

Madhara na unyonge unaotukumba Waafrika, sababu kuu ni sisi wenyewe. Ni kweli wazungu wanaendelea kutubana kwa kutumia mbinu tofauti lakini uhusika wetu katika kufika hapa tulipo bado unabaki kwetu.

Huwa najiuliza na kukosa jibu nikiangalia mifano michache ifuatayo:

1. Kagame amekubali nchi yake kufanywa dampo ya wakimbizi hata wa Syria, Bangladesh, nk. Amefadhilisha vijimilioni toka UK. Je, madhara ya baadae ameyazingatia?

2. Nchi kadhaa za Kiafrika zimeuza wanyama wengi Uarabuni kiasi cha kwamba Dubai imeanzisha Safari park yenye mvuto wa hali ya juu hadi wengi washaanza kufadhilisha kwenda huko badala ya kuja Afrika. Je, watalii watapopungua kuja kuangalia wanyama Afrika tutawalaumu wazungu/Waarabu?

3. Eti sisi wa kukosa ngano kwa sababu ya vita vya Ukraine na Urusi? Tunategemea kuagiza wakati tuna ardhi yenye rutuba kuliko ya huko tunakotegemea kuagiza. Je, na hapa tutawalaumu Wazungu?

4. Kuna mifano mingi mno ya kila pande ambayo kwa ujumla wake inaonesha wazi kuwa tatizo kuu lipo kwetu si kwa wenzetu .

Je, tunaanzaje kujinasua kwenye tope hili?
 
Viongozi wako wanachumia matumbo yao na c kuijengaa nchii,unamkutaa mtu kakaa ofc ya serikali n mkurugenzii anapigaa story na rfk yake anamwambia aiseee kpndi tunasomaa tulipitiaa msotoo sanaa ukuu wanachekaa nakusemaa huu ndio wkt wakulaaa maishaa nakusahau shdaa tulizopitiaaa ,yy anaamini kupewa kile cheo n sehemu yakulaa c kwendaa kusaidiana na wengineee kulikomboa taifaaa,,,,unategemeaa nchi itasongaa vp mbelee mkuuu
 
Viongozi wako wanachumia matumbo yao na c kuijengaa nchii,unamkutaa mtu kakaa ofc ya serikali n mkurugenzii anapigaa story na rfk yake anamwambia aiseee kpndi tunasomaa tulipitiaa msotoo sanaa ukuu wanachekaa nakusemaa huu ndio wkt wakulaaa maishaa nakusahau shdaa tulizopitiaaa ,yy anaamini kupewa kile cheo n sehemu yakulaa c kwendaa kusaidiana na wengineee kulikomboa taifaaa,,,,unategemeaa nchi itasongaa vp mbelee mkuuu
Umefafanua vyema tatizo ambalo sote tunakubaliana kuwa lipo. Lakini bado hujatusaidia ushauri wako wa nini kifanyike ili tuondokane na tatizo. Unajua moja ya matatizo ambayo wengi tunayo, ni hii hali ya kuendelea kulichambua tatizo bila ya kujaribu kushauri hatua za kulitatua.
 
Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
Nakubaliana nawe kuwa binadamu siku hizi ni wabishi, lakini ktk huu ubishi walionao, je unashauri nini kifanyike ili tuondokane na hali hii mbaya tunayoendelea kuishi nayo?
 
ni kweli kuwa matatizo makubwa ni kwetu na inatokana na approach ya self egoism yaani sisi ni wabinafsi na ubinafsi huu umetengenezwa kutokana na mfumo wa kiuchumi na kijamii pamoja siasa za kimagharibi hivyo tatizo limeratibiwa na wao kwa kutulazimisha kukopi mifumo yao ya maisha badala yake inakuwa oversize kwetu.

ndio maana uuzaji wa wanyama no one care about future zaidi ya tumbo lake na kwa bahati mbaya program inatekelezwa na hao marais wanaoenda nje kila kukicha.

upokeaji wa wahamiaji ni athari na atari za kiusalama kwa miaka ya baadae,

nini kifanyike

kama ingelikuwa siku zinarudi nyuma basi basi tungemrejesha magufuli kwani aina ya viongozi wanaohitajika katika uthubutu ni yeye pia aliubadili mfumo wa ubepari kwa namna ambayo haijatamb ulika kwa haraka na kujenga mfumo wa kikomunist ambao unaorelate na ujamaa na ndio rafiki kwa afrika japo ilipaswa kuwepo miaka mingi kulipokea hili.

seminar za kila mwezi kutoa elimu kwa viongozi wa taasisi ni muhimu kwa kulijali taifa na kulipa kipaumbele.

katiba katiba katiba coz hatuna taasisi huru ya kufatilia ujinga wa viongozi zaidi ya CAG ambae anapiga domo na hakuna any legal actions,
 
Back
Top Bottom