Tatizo la watu kushindwa kujielezea

Tatizo la watu kushindwa kujielezea

mutant gene

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
876
Reaction score
326
Watanzania tuna tatizo sana la kujielezea au kutoa ufafanuzi wa jambo fulani au nini kifanyike juu ya jambo fulani. Ukitaka kukubaliana na mimi angalia vipindi vya kwenye television au radio ambavyo vinahoji Watanzania au hata humu JF unaweza ukathibitisha.

Unaweza kupigwa butwaa mtu anavyojibu au anavyoelezea jambo mpaka unajiuliza hivi huyu anaelewa anachoongea/kuulizwa au anaongea na ye aonekane ameongea! hili tatizo si kwa wale wasioenda shule pekee bali hata waliofanikiwa kupata elimu.

Najiuliza sana hii hali inasababishwa na nini? kutojiamini, kukosa ufahamu, uvivu wa kufikiri, kujifanya tunajua sana wakati hatujui au ukosefu wa lishe bora toka utotoni umedumaza akili za watanzania wengi?! na kama tumerogwa basi alieturoga, ameturoga pabaya. tuna safari ndefu sana! Kwa ufupi hili taifa kuja kufanikiwa ni ndoto ya saa sita mchana.
 
watanzania tuna tatizo sana la kujielezea au kutoa ufafanuzi wa jambo fulani au nini kifanyike juu ya jambo fulani. ukitaka kukubaliana na mimi angalia vipindi vya kwenye television au radio ambavyo vinahoji watanzania au hata humu JF unaweza ukathibitisha. unaweza kupigwa butwaa mtu anavyjibu au anavyoelezea jambo mpaka unaiuliza hivi huyu anaelewa anachoongea/kuulizwa au anaongea na ye aonekane ameongea!! hili tatizo si kwa wale wasioenda shule pekee bali hata waliofanikiwa kupata elimu.

najuliza sana hii hali inasababishwa na nini? kutojiamini, kukosa ufahamu, uvivu wa kufikiri, kujifanya tunajua sana wakati hatujui au ukosefu wa lishe bora toka utotoni umedumaza akili za watanzania wengi??! na kama tumerogwa basi alieturoga, ameturoga pabaya. tuna safari ndefu sana!! kwa ufupi hili taifa kuja kufanikiwa ni ndoto ya saa sita mchana.
Wazungu wanarudi taifa hili litaendelea tu.....! Labda useme watanzania kuendelea ndo itakuwa ngumu maana elimu yenyewe ni ya kukaririshwa majibu......
 
watanzania tuna tatizo sana la kujielezea au kutoa ufafanuzi wa jambo fulani au nini kifanyike juu ya jambo fulani. ukitaka kukubaliana na mimi angalia vipindi vya kwenye television au radio ambavyo vinahoji watanzania au hata humu JF unaweza ukathibitisha. unaweza kupigwa butwaa mtu anavyjibu au anavyoelezea jambo mpaka unaiuliza hivi huyu anaelewa anachoongea/kuulizwa au anaongea na ye aonekane ameongea!! hili tatizo si kwa wale wasioenda shule pekee bali hata waliofanikiwa kupata elimu.

najuliza sana hii hali inasababishwa na nini? kutojiamini, kukosa ufahamu, uvivu wa kufikiri, kujifanya tunajua sana wakati hatujui au ukosefu wa lishe bora toka utotoni umedumaza akili za watanzania wengi??! na kama tumerogwa basi alieturoga, ameturoga pabaya. tuna safari ndefu sana!! kwa ufupi hili taifa kuja kufanikiwa ni ndoto ya saa sita mchana.
Nadhani hata wewe una shida ya kujieleza pia. Daima anza na herufi kubwa mwanzoni mwa kila sentensi.
 
Hatuhamasishwi au kupewa uhuru wa kuwa na ujasiri kwa kujielezea tokea utotoni. Wakati bado mtoto kila utakachoongea utambiwa nyamaza tabia mbaya hiyo, mkubwa anapoongea unakaa kimya. Mathalan kwenye nyumba wazazi wote hawapo, mtu anakuja kuulizia kitu kidogo tu, lakini mpaka asubiri wazazi warudi, hata kama unajua/unaweza ole wako uwaeleze au kujielezea wakirudi ujue ni adhabu tu.
 
Wale vijana watatu walikua wanaenda kujieleza kwa Profesa IKULU.
UMEONA CCM ILICHOWAFANYA.??

TATIZO NI MIFUMO. MKOLONI MWEUSI NI SHIDA, BORA HATA MZUNGU.
 
Mkuu swala lipo mtambuka,linatokana na malezi tangia utotoni,wazazi kukujenga kujiamini,nakumbuka mzizima kuna somo kabisa la public speaking na pia kuna baadhi ya shule kuna morning talk,hivyo inamjengea mwanafunzi kusoma na kujijenga kujieleza maana before morning talk lazima umeze desa.
 
Kaka ni vizuri ungekuja na majibu pendekezi ya hili tatizo ili kuisaidia jamii yetu.

Hiyo ni kazi yetu sasa,yeye ametimiza wajibu wake wa kutuletea changamoto iliyopo kwahyo syo lazima yote atekelza yeye, upo bro?
 
Nahisi wewe ni mmoja wao. A thin line between true and false!!!
 
Jombaa!!hilo tatizo ni janga la Afrika Ndio maana wazungu wanatucheka ila kwa kwetu serikali sikivu ya CCM imezidisha ujinga
 
watanzania tuna tatizo sana la kujielezea au kutoa ufafanuzi wa jambo fulani au nini kifanyike juu ya jambo fulani. ukitaka kukubaliana na mimi angalia vipindi vya kwenye television au radio ambavyo vinahoji watanzania au hata humu JF unaweza ukathibitisha. unaweza kupigwa butwaa mtu anavyjibu au anavyoelezea jambo mpaka unaiuliza hivi huyu anaelewa anachoongea/kuulizwa au anaongea na ye aonekane ameongea!! hili tatizo si kwa wale wasioenda shule pekee bali hata waliofanikiwa kupata elimu.

najuliza sana hii hali inasababishwa na nini? kutojiamini, kukosa ufahamu, uvivu wa kufikiri, kujifanya tunajua sana wakati hatujui au ukosefu wa lishe bora toka utotoni umedumaza akili za watanzania wengi??! na kama tumerogwa basi alieturoga, ameturoga pabaya. tuna safari ndefu sana!! kwa ufupi hili taifa kuja kufanikiwa ni ndoto ya saa sita mchana.

Umeongea kweli mkuu, labda nitoe mfano hai kabisa niliouona kwa macho yangu.

Wiki mbili zilizopita msanii RECHO alikua anaojiwa na mtangazaji wa BBC Chazi Hilary.

Aliulizwa 'kuna changamoto gan katika muziki unaofanya'
Jibu alilotoa ni 'Anatongozwa sana na wanaume wengi wakitoa ahadi ya kumpa fedha.

Nilitegemea kua angesema labda soko bado liko chini au wizi WA kazi ni mkubwa na udhibit ni mdogo.
 
unaposema watanzania wewe ni mtu wa wapi
umetoa mfano wa msanii recho lakini unajua back ground yake maana wasanii wengi kutoka nchi zilizoendelea kimuziki wengi ama wamepitia vyuo vya sanaa au wana elimu kubwa ambayo si inamsaidia katika muziki bali pia na mambo mengine mfano wanamuziki wa nigeria
Ningekuelewa zaidi kama ungesema baadhi ya watanzania unazungumzia watu wanaohojiwa kwenye tv angalia hao watu wanapatikanaje
mwisho labda ungesema kwanini watanzania wengi wanapenda kulalamika kama wewe umetoa malalamiko lakini sikusikia ukitoa hata ufumbuzi mmoja
 
1. Ninaamini tuna tamaduni zilizojaa mizaha
2. Mafundisho mengi yanatia mkazo kujua kuongea - lakini hakuna msisitizo wa kufundisha 'kuongea nini'
3. Tamaduni nyingi Tanzania zinatilia mkazo na kufundisha 'kuamini' na kuheshimu - lakini hazitoi nafasi ya kuuliza maswali ya kwamba kwa nini uheshimu!
4. Kuna mambo mengine ambayo ni malezi ya kutokuwa wabishi au watu wa kuthubutu - ambavyo ninaamini kunasababishwa na makuzi ya kisiasa ( hasa siasa za ujamaa, michango ya imani za dini zetu)
5. Kutokuwa na viwango binafsi (personal standards) kwamba jambo lolote ni sawa tu ilmradi ninakula
6. Kuabudi kula - na kufanya chakula kama currency for exchange for anything including morals and convictions - yaani mtu anaweza hata kukuvulia suruali ilimradi anapata chakula!
 
Watanzania tumelelewa katika mazingira ya kuwa waoga na kutojiamini kuanzia nyumbani kwa wazazi mpaka mashuleni....ujasiri wetu tunautumia katka mambo yasiyo na faida hata kidogo....kutokana na matumizi ya lugha isiyo sahihi katika mfumo mzima wa elimu , lugha ambayo hata mwalimu haimudu ni jambo gumu sana kwa mtanzania kuongea mbele ya halaiki ya watu....vile vile watanzania ni watu wenye mawazo mazuri na ya msingi sana isipokuwa tuna jinamizi la kuogopa kuthubutu....
 
Tetere uko juu. Jamani jamii yetu inatuzuia kujieleza na kujiamini.
Wakuu(viongozi na wazazi) wetu wanashangaa mtu anapojieleza na kuuliza maswali. Inatafsiriwa kama uasi au dharau kwa mkuu. Hivyo tunayo safari ndefu kujijengea uwezo binafsi wa kujiamini ili kuweza kujieleza kwa ufasaha.
Bahati mbaya shule kama Mzizima wanapofundishakujieleza si nyingi.
 
Na wewe umeshindwa kujieleza vile vile. Unajua tatizo lakini huna ufumbuzi, umebaki kuhisi kulogwa, lishe duni n.k
 
Back
Top Bottom