Tatizo la Watoto wa Mitaani : Nini Kifanyike

Tatizo la Watoto wa Mitaani : Nini Kifanyike

#Ndetichia kweli Obama alipokuja ni mengi sana kama vile yalipatiwa uvumbuzi lakini kwa nini tusubirie hao akina Obama ndo tujitume? Serikali ina power kubwa sana tatizo kujituma ndio shida maana pale inapoamua kufanya jambo linafanyika. Kama leo Rais Kikwete atatoa tamko kali kwa wakuu wa mikoa yote kwamba ndani ya miezi mitatu ufumbuzi wa watoto hao upatikane na ambaye hawezi aachie ngazi mapema unadhani haliwezi kufanikiwa kwa zoezi hilo. Hili linawezekana sana maana hawatakubali kipoteza kazi zao. Wao nao watatoa amri kali kwa wakuu wa wilaya. Wilaya nao Tarafani. Tarafa nao katani ambapo kwa mtiririko huo inawezekana.
 
mi naona wengi wanaongelea tatizo sioni mtu anayeongelea suluhisho ukweli kuna watoto wengi wa mitaani kama utabahatika kutembea kariakoo usikuutakuta wengi wanachukua mabox na kulala barabarani au kwenye viambaza vyenye maduka na hili limefumbiwa macho kwa sababu usitawi wa jamii ama wamesahaulika na hawapewi kipaumbele kama cha bajeti na pia wizara husika mawaziri hawajui kazi yao ni nini lakini hawa watoto baadae ndio wanageuka majambazi,vibaka,machangudoa,mashoga na mateja kwa hiyo tusidhani tuko salama kwa sababu tu watoto wetu tumewaandalia mazingira mazuri ni wakati wa kuwakumbusha wahusika watimize wajibu wao
 
Ni kweli kabisa #Roderick_Alexander . Hawa watoto ni wengi na ndio wanabadilika kuwa majizi hatari baada ya maisha kuwa magumu kwao. Suluhisho ni Rais kutoa amri kali kwa wizara husika bila hivyo watazidi kila siku.
 
Watoto wa mitaani wameongezeka, na wengi.wametokea mikoani kukimbilia kwenye majiji.
Tatizo linaanzia kwenye familia, malezi kufikia mpaka binti kupata mimba, inakuja kijana aliyempa mimba na kuikataa.
Hapo ndio familia inatakiwa isimamie malezi ya mtoto hata kama kijana kakataa, kinyume cha hapo, binti akifukuzwa ndio anamtupa mtoto.

Wanawake km unaona huwezi kutunza mtoto tumia protection, matatizo yakikupata huyo kijana hutomuona.
Mnatesa tu watoto mitaani.
Nyingine ni wamama wa kambo nao wanachangia watoto kutoroka majumbani.
Mwisho mimi nalia na Wizara ya Jinsia wanawake na watoto, hii wizara iko butu sn kushughulika na watoto wa mitaani.
Hiyo wizara viongozi wake wapo busy zaidi kushawishi wamama wajiunge na umoja wa wanawake tz na kuchagua lichama furani ambalo limeshapitwa na wakati, badala ya kushughulikia matatizo kama hayo. Na huo umoja wa wanawake bora uitwe umoja wa wanawake wa chama cha magamba, sababu hauwawakilishi wana mama wote toka kila chama na itikadi tofauti zaidi ya CCM. Sasa kwa nini uitwe umoja wa wanawake TZ?
 
Serikali haina mda wa kuwajali hawa watoto bali wanajali maslahi yao binafsi. Mfano wabunge wa bunge la katiba wao wanadai tu posho kubwa bila kujali hali ya nchi.
 
Hili suala la watoto wa mitaani linazidi kukuwa kwa kasi sana maana Mwanza sasa wameongezeka ombaomba na watoto wa mitaani na huu ni uzembe unaotokana na serikali kutodhibiti hali hii.
 
bf9517f048d6cabf48eb628dbbf5c6e2.jpg


Serikali ya mkoa wa Mwanza inabidi iangalie namna ya kudhibiti kundi kubwa la watoto wa mitaani ( chokoraa) na omba omba wenye watoto wadogo

Kiukweli ukipita maeneo mengi ya katikati ya jiji utakutana na watoto wengi wa mitaani ambao usiku wanageuka wahalifu hatari mi nishakabwa usiku mmoja na kuporwa pia mji umejaa kina mama na kindada ambao wanaendesha shughuli ya kuomba wakiambatana na watoto wao wadogo kiukweli inatia huruma kwa hawa malaika wanaozunguka kutwa na mama zao wanaoomba omba

Nawasilisha
 
Jinsi ulivyoandika watu watadhani mwanza ina watoto wengi chokoraa mpaka hamna amani. Mleta mada kuwa fair taja mitaa,hawa watoto kweli wapo ila sio kero kihivyo.

Kinadada ombaomba sijawahi waona naona wababa omba omba wapo wengi tu(mitaa ya kenyatta) wamama wachache.
 
Mtaa haujawahi kuzaa watoto, hao ni watoto waliotelekezwa na wazazi wao.

Kuepukana na hili janga, elimu ya uzazi wa mpango itolewe kila wanapokusanyika watu.
 
Watu wameshaanza kukanusha wakati ukweli ni huu mwanza watoto wasikuwa na makazi wanaongezeka kwa kasi ukisimama kwenye mataa tayari wameshajaa mitaa Liberty Rwagasore kamanga ferry huko kwenye garden ukijichanganya wana wewe Mabatini Uhuru Rufiji omba omba na wenyewe wamekuwa ni miradi ya watu
 
Hili linalosemwa limeshaanza, kuliacha likawa kero ni kushindwa kupanga utaratibu mzuri wa mji, kinachotakiwa serikali ilidhibiti mapema kabla halijazaa "Panya Road"
 
Tatizo la watoto wanaolala mitaloni na kwenye maduka (ambao tunawaita machokoraa, japo sidhani kama ni sahihi) ni tatizo la nchi nzima hasa kwenye miji mikubwa.

Wengi sio yatima kama tunavyofikiria ila ni watoto walioamua kukacha kwao na kuamua kuishi mitaani sababu kubwa unyanyasaji, hali ngumu ya kimaisha(wanavyosema wenyewe.)
 
bf9517f048d6cabf48eb628dbbf5c6e2.jpg


Serikali ya mkoa wa Mwanza inabidi iangalie namna ya kudhibiti kundi kubwa la watoto wa mitaani ( chokoraa) na omba omba wenye watoto wadogo

Kiukweli ukipita maeneo mengi ya katikati ya jiji utakutana na watoto wengi wa mitaani ambao usiku wanageuka wahalifu hatari mi nishakabwa usiku mmoja na kuporwa pia mji umejaa kina mama na kindada ambao wanaendesha shughuli ya kuomba wakiambatana na watoto wao wadogo kiukweli inatia huruma kwa hawa malaika wanaozunguka kutwa na mama zao wanaoomba omba

Nawasilisha
Ndugu Wazabanga kuku hoja yako kwangu inamashiko tena mkubwa

Nakuja na Nchi mbili kama mfano waliopata ktk kupuuzia lundiko la watoto walio telekezwa mtaani ( Uganda 2000's-2012 na Liberia )

Uganda ilikuwaje 2000-2016

Kulizuka na kundi linalopingana serikali , likijiita LORD RESISTANCE ARMY ( LRA ) likiwa chini ya Mhasi Mkuu Joseph Kony

Je Kony alianzaje kuliunda hilo kundi , yeye aliwateka wanafamilia mbali mbali pia aliona fulsa mkubwa sana uwepo wa watoto wa mitaani walio kuwa Uganda kaskazini magharibi ,
Kony aliwachukuwa na kuwatunza kisha akaanza kuwalisha sumu ( pumba au ujinga ) kuwa selikali ndo adui wao kwa iyo wapambane dhidi yao , kweli Kony alifanikiwa na akawa kikwazo Uganda

HUYU JOSEPH KONY ALIMPIGA RISASI KAMANDA WAKE VINCENT OTTI , BAADA YA OTTI KULIDHIA HATI YA MAKUBALIANO YA AMANI NA SERIKALI ,
NDPO 2006 KUANZISHWA KWA MAZUNGUMZO YA " JUBA PEACE TALK " LAKINI HAWAKUFANIKIWA

Tukaangalie muvi inayoitwa JOHN MAD DOG ( JONI KICHAA )


KWA UPANDE WA LIBERIA

Ndugu Charles Taylor baada ya kusndwa uchaguzi yeye aliamua kukusanya watoto wa mitaani na watoto mateka na kuwafunza ukatili naye akafanikiwa
( siyo muvi ya chazi ila ni mfano wa Liberia ile muvi ya BLOOD DIAMOND )

Binafsi nimeishi Mwanza , nimepata kutembea sana pale mwanza hoteli na maktaba ya wahindi hawa madogo wapo wengi wana viwembe mda wa usiku , usiku wakikuomba pesa wape ondoka zako
Sasa watoto kama hawa hii sumu waliojipandkiza ni mbaya na hatarishi kwa usalama wa jiji la Mwanza
 
Mkuu saa 2 usiku unatafuta nini katikati ya jiji,? Hiyo mida ikifika waachie wahindi, machangu na machokolaa..
 
Kuna mama mmoja mmene mweusi yupo hapo round about karibu na benki kuu ana vitoto vidogo , ndivyo anavitumia kuomba mtu akipita anakufuata akidai hela ya chakula na asipopewa mama yake anamtukana na kumwambia kwanini wakati unaomba hukuwa unalia? Hili ni janga na sijui hawa watoto watakuwaje huko mbeleni
 
Mkuu saa 2 usiku unatafuta nini katikati ya jiji,? Hiyo mida ikifika waachie wahindi, machangu na machokolaa..
Nazani unapozungumizi sifa za jiji lolote lile lazma kuwe na mizunguko ya watu wakitafuta riziki kwa usahihi wa kisheria ,
Morogoro , Kibaha si majiji lakini kuna mizunguko ya watu wengi mpaka sita usiku
Mm naona swala zima ni ufumbuzi na mtazamo wa hao watoto walio telekezwa mitaani
 
Back
Top Bottom