Tatizo la kuzeeka haraka

Tatizo la kuzeeka haraka

mbwewe

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2014
Posts
3,267
Reaction score
3,409
Wakuu habari za jioni?

Mimi ni kijana wa miaka 32 kuna tatizo kwa kweli limekuwa likinikosesha raha sana, nimeona nikilileta hapa jamvini ninaweza kupata suluhisho.

Kama nilivyoainisha hapo juu umri wangu ni miaka 32 lakini nina muonekano kama wa mtu mwenye miaka 40+ , yaani imefikia nikimwambia mtu yoyote umri wangu huwa wanashangaa sana na kuhisi labda ninadanganya.

Yaani sometimes watu walionizidi umri huwa wananiamkia na wengi niliowauliza wanahisi naweza kuwa na umri gani huwa wanasema may be 43 au 45.

Sasa sijaelewa tatizo langu litakuwa linahusiana na hormone au vipj.

Kwa muonekano ni mnene kiasi nikiwa nina kilo 90 na urefu wa futi 5 na inchi 10.

Sasa wadau ninaweza kupata suluhisho lolote kuhusu hii hali inayonikabili?

Nb: Sinywi pombe wala sivuti sigara.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Fanya mazoezi, ongeza matunda na mboga za majani katika milo yako. Punguza pombe na nyama.

Jitahidi usiwe na stress na ukiwa nazo ziwe za muda mfupi.

Kunywa sana maji yanasaidia kulainisha ngozi.

kilo 60-70 ideally but 90kg it’s a bit too much.
 
Punguza unene bro toa hiko kitambi
Usivae misuruali na mishati mipana
Usifuge nywele na ndevu nyingi
Penda kufanya mazoezi
Kama unaupaa, nyoa nywele zote usiache hata moja
Sometimes penda kuvaa jinsi, tshirt, raba
Ukiwa na ukwasi wakutosha itapendeza zaidi maana pisi kali zote zitakuita baiiibee

Sent from my SM-J701F using JamiiForums mobile app
 
Wakuu habari za jioni?

Mi ni kijana wa miaka 32 kuna kwa kweli limekuwa likinikosesha raha sana, nimeona nikilileta hapa jamvin ninaweza kupata suluhisho...
Mkuu kwanza nakuuliza.

UNA KIPARA KICHWANI AMA HUNA ?
 
1621964803296.png
 
Kuna pepo la kuzeesha watu wanatupiwa, waweza kuta una mwonekano wa kawaida tu, ila kila mtu anakuona mzee, madem ambao unapaswa kutoka nao wanakuona BABU badala ya BABY! So check check na body scanning kujua kama unalo!
 
Fanya mazoezi, ongeza matunda na mboga za majani katika milo yako. Punguza pombe na nyama.

Jitahidi usiwe na stress na ukiwa nazo ziwe za muda mfupi.

Kunywa sana maji yanasaidia kulainisha ngozi.

kilo 60-70 ideally but 90kg it’s a bit too much.
Sababu ya huo unene,

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom