Tatizo la CRDB Simbanking

Tuache ulalamishi usio na mashiko, mimi naitumia huduma hiyo mwaka wa sita sasa na taizo la namna hiyo limenitokea mara tatu tu. Ni vyema ukaelewa kuwa changamoto za namna hiyo huwa zinajitokeza kutokana na matatizo mbalimbali na mengi zaidi yakisababishwa na mtandao kuwa chini. Huduma za mtandao hazitolewi na CRDB bali wao huwategemea Service Providers wengine. Sio jambo zuri sana kuchafua biashara za watu kwa tatizo dogo lililokukuta mara moja.
 
voda kidg wapo slow n hudum hii ila tigo ni fasta tu hela yako uki transfer kwa simbanking..
 
Issue ya nauli ni kama unaishi mbali sana na zilipo hizo mashine,but kama ni around the town ATM better.But why hizi comm companies zi charge kiwango kikubwa hivyo? Bila shaka ni KODI na gharama za uendeshaji,so lawama hapa ziende Serikalini! Waangalie set up ya uchumi wa nchi,kuepuka wananchi kulaumiana
 
Ni natumia simbanking mara nyingi sana haijaniletea tatizo lolote.nimetoka kununua LUKU sasa hivi na nimefanikiwa.kumbuka muamala ukigoma inawezekana link ya huo mtandao wa simu ilikuwa down na sio simbanking.
 

Kitu chochote duniani kinachotumia computer system kweny emergency ujue umeliwa ...... DUNIANI............. Shateseka Las Vegas balaa na CC then wakati narudi LA - LAX ikakubali....
 
Umeongea bila kufikiria other factors...mfano muda,usafiri,usalama nk...kama ATM ipo nyumba ya pili hapo sawa lakini kama lazima uchukue usafiri ni sawa sawa na pengine nafuu kuliko hiyo 2100 ulioitaja...hapo bado hujaangalia usalama wa kutembea na fedha njiani na pia muda utaotumia kufika kwa ATM.viwango na gharama benki zote wanachaji pesa hiyo hiyo..NMB wanachaji pesa hiyo hiyo Exim benk ndo wanakata zaidi.
 


Acha kubwatuka wewe.....
Sasa umenipinga ama umeni sapoti????

Case study:
Naishi Mwananyamala, ATM ziko zimejaa kibao karibu kila kona siku hizi....
CRDB wamesambaza ATM katika centres zote muhim mjini....
Naweza kwenda pale Mwananyamala Hospital, nikiona vipi nasogea pale Makumbusho stand...

Mambo ya Simbanking bakini nayo nyie wa Vijijini mpigwe pesa za kijinga...


[HASHTAG]#Chief[/HASHTAG] Eng
 
Umesahau na gharama za nauli na usumbufu kuzifikia hizo ATM


Acha kubwatuka wewe.....

Case study:
Naishi Mwananyamala, ATM ziko zimejaa kibao karibu kila kona siku hizi....
CRDB wamesambaza ATM katika centres zote muhim mjini....
Naweza kwenda pale Mwananyamala Hospital, nikiona vipi nasogea pale Makumbusho stand...

Mambo ya Simbanking bakini nayo nyie wa Vijijini mpigwe pesa za kijinga...


[HASHTAG]#Chief[/HASHTAG] Eng
 


Acha kubwatuka wewe.....

Simbanking ni Huduma expensive sana, inakutia umasikini kama hujui...

Mfano :
Kuhamisha tuu 10,000 kutoka Simbanking kwenda Mpesa /Tigopesa unakatwa 2130.
Wakat kama unngeenda ATM makato ni 944.

Twende :
Kuhamisha 500,000 kutoka Simbanking kwenda Mpesa/Tigopesa unakatwa 6000.
Wakati kama ungeenda ATM makato ni 1888.

Conclusion:
Tuache tabia za Uvivu, kupenda shortcut.
Kama unaweza kwenda ATM ni bora mara 100% kuliko kutumia Simbanking.
Simbanking ni gharama sana, unganisha na changamoto kama hizo juu za Wadau wanatoa hela, hawazioni mpaka wasubiri masaa 24.

Kama hiyo haitoshi:
Kumbuka kuna gharama za kutoka Simbanking kwenda Mpesa/Tigopesa, jumlisha na gharama za kutoa hela Mpesa/Tigopesa kwenda mkononi.

Simbanking ni Huduma ya kifala, hasa kwa sisi tulioko Dar sababu ATM zimejaa kila kona.

[HASHTAG]#Chief[/HASHTAG] Eng.
 
Ni natumia simbanking mara nyingi sana haijaniletea tatizo lolote.nimetoka kununua LUKU sasa hivi na nimefanikiwa.kumbuka muamala ukigoma inawezekana link ya huo mtandao wa simu ilikuwa down na sio simbanking.


Acha kubwatuka wewe...

Tunaongelea kufanya miamala kutoka Simbanking kwenda Tigopesa/Mpesa..
Achana na hivyo vi LUKU vyako vya buku buku....

Simbanking ni Huduma expensive sana, inakutia umasikini kama hujui...

Mfano :
Kuhamisha tuu 10,000 kutoka Simbanking kwenda Mpesa /Tigopesa unakatwa 2130.
Wakat kama unngeenda ATM makato ni 944.

Twende :
Kuhamisha 500,000 kutoka Simbanking kwenda Mpesa/Tigopesa unakatwa 6000.
Wakati kama ungeenda ATM makato ni 1888.

Kama hiyo haitoshi:
Kumbuka kuna gharama za kutoka Simbanking kwenda Mpesa/Tigopesa, jumlisha na gharama za kutoa hela Mpesa/Tigopesa kwenda mkononi.

Simbanking ni Huduma ya kifala, hasa kwa sisi tulioko Dar sababu ATM zimesambaa kila kona

[HASHTAG]#Chief[/HASHTAG] Eng
 
Wewe umefanya muamala lini?Mie pesa yangu ilikwama na ndani ya masaa 24 pesa iliingia!tembelea page zao utapata msaada wa haraka zaidi
 

Mimi binafsi ni huduma hii ya Sim banking inanisaidia sana. Sijawahi kwama. Inawezekana kwako imekuwa ni bahati mbaya tu. Pole sana.
 
NMB Mobile haijawahi kuniangusha ... Malipo yangu yote nafanyia hiyo kitu. Na kama kuna shida ya mtandao wana kua alert mapema ili usiingize kichwa..!
 
Simbanking inarahisisha kwenye kufanya malipo mbalimbali. Ikitokea muamala umekwama Naamini hizi ni changa moto tu ambazo zinaweza kutokea kwenye Kampuni yoyote siyo CRDB tu. Hakuna biashara bila changamoto, na kupitia changamoto hizo ,kampuni au Biashara inaweza kufanya vizuri zaidi. Bigup CRDB. keep it up.
 
CRDB ndio maana nimehama huduma zao mbovu sana mpaka ATM muda wote hazifanyi kazi
 
Mimi siku wakiniletea huo uhuni nitawatukana sana hapana chezea hela yangu tena na hiki kipindi cha Magufuri.
 
Changamoto zakimtandao zipo sana hata kwenye makampuni ya simu hiyo hali huwa inatokea, mimi ni mdau ninaetumia sana sana simbanking na ninatumia Mpesa na tigo pesa kwenye akaunti tofauti za Crdb bank kwangu imekuwa msaada mkubwa kunirahisishia maisha pale ninapokuwa na huitaji wa pesa na nipo mbali na ATM mashine, napia inanipunguzi cost kama kulipa nauli kwenda kwenye ATM, na pia Muda sipotezi, kukwama kwamiamali nijambo la kimtandao ambalo halikwepeki na isitoshe Crdb bank katika huduma ya simbanking nafanya kazi pamoja na mitandao ya simu, kwahiyo hapo inategemeana kwakiwango kikubwa, yawezekana na mtandao wasimu hauko vizuri au pia kwa upande wa bank pia hauko vizuri, sasa tusiilalamikie tu Crdb bank ila tuangalie pande zote mbili swala la mitandao kufail nichangamoto sana, minatumia simbanking na kwangu iko super, minawapongeza sana Crdb bank kwa huduma ya simbanking upatikanaji wa pesa umekuwa rahisi sana.
 
Mi nilikaa wiki 3, tena nilikua safarini, nilipoenda benk wananiambia niandike barua, ilhali sina hela yeyote ya kwenda kula huku nikisubiria barua amabayo ilikaa wiki 3.
 

Mkuu nadhani si vyema kuiita ya kifala bali tuseme tu ni huduma nzuri lakini itumie tu pale ambapo huna suruhisho lingine,mfano binafsi huwa inanisaidia sana nikiwa vijiji vya mbali kusiko na ATMs bali kuna MPESA na TigoPesa.

Kila kizuri hakikosi kasoro.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…