Tatizo kwenye ada za mafunzo ualimu

Tatizo kwenye ada za mafunzo ualimu

Korozoni

JF-Expert Member
Joined
Oct 24, 2016
Posts
264
Reaction score
106
Hivi karibuni wizara ilitangaza kufuta mafunzo ya Ualimu Elimu ya Msingi ngazi ya Stashahada na kurudisha mfumo wa Astashahada ambao ulikuwapo zamani.


Ikumbukwe kuwa kipindi cha nyuma Ada ya mafunzo ngazi ya Astashahada ilikuwa Tsh.400,000 na Stashahada Tsh.600,000.


Cha ajabu baada ya Astashahada kurudishwa Ada imebaki kuwa Tsh.600,000 kwa vyuo vya Serikali ambayo ni ya Stashahada.


Je,waziri Ndalichako kipindi unatoa tamko la kufuta Stashahada hukukumbuka kwamba kuna tofauti ya malipo katika ngazi hizo mbili?Mbona umekaa kimya na wananchi wakiendelea kunyonywa?

Hii ni kwa sababu wanafunzi walioomba udahili katika mafunzo hayo mwezi Novemba wameendelea kuona Ada ya mafunzo hayo ikiwa ni Tsh.600,000!
 
Mmmh hii nchi ni yamatajiri tu masikini hana chake ww unafikri Mtoto wa masikini anaweza pata wapi laki NNE ? Au sita ya chuo si karo wangerudisha kama ya advance shule za serikali ikawa elfu sabini tu
 
Mmmh hii nchi ni yamatajiri tu masikini hana chake ww unafikri Mtoto wa masikini anaweza pata wapi laki NNE ? Au sita ya chuo si karo wangerudisha kama ya advance shule za serikali ikawa elfu sabini tu
Yaani hii nchi imejaa mambo ya ajabu sana!ukiangalia kwa umakini mwanafunzi huyo aliyeomba kwenda chuo alishindwa kulipa ada ya sekondari kwa wakati mmoja ambayo ni kati ya 20,000 na 70,000,leo hii unamuambia alipe laki sita au nne na michango isiyopungua laki moja!atazitoa wapi?
 
Back
Top Bottom