Tatizo kwa Waislamu si Mahakama ya Kadhi, ni AJIRA!

Status
Not open for further replies.
a) Leta data na research inayoonyesha kwamba waislamu wanahitaji ajira zaidi kuliko wakristo?
b) Wewe ambaye si muislamu unajuaje umuhimu wa mahakama kama siyo ubinafsi na chuki zako..
c) Gharama ngapi serikali ime-finance miradi ambayo inahudumia dini moja (wakristo) waislamu hawakuja na hoja za kipuuzi kama hizi
d) You can postpnent the issue lakini lazima itakuwepo wakati huo itakuwa too late kujadili kwa busara kama sasa

Tumain
Mbona na wewe hutuwekei data za miradi ya wakristo wanaofadhiliwa na serikali.Chuki naiona kwako kwa jinsi ulivyoleta hoja yako.watanzania wote wawe waislamu au wakristo wanahitaji ajira hilo halina swali.
Katika hali ya jaziba unayoionyesha nina wasiwai kwamba huwezi kujenga hoja yoyote,tulia utafakari ujibu kwa hoja badala ya kujibu kwa jazba.
watu wengi hasa ambao si waislamu wangependa kujua faida na hasara za kuanzishwa mahakama hiyo.
Ikumbukwe kwamba tulifika mahala ambapo swala la udini halikuwapo,ninapoandika hivi ninaushahidi wa marafiki zangu na baadhi ya ndugu ambao wameoana wakiwa dini tofauti,hapa na maanisha dini siyo dhehebu,yaani mmoja mkristo na mwingine mwisilamu. Hata wengine walifikia mahala ambapo kila mmoja anabakia na dini yake je ikifikia mgogoro hao wataamuliwa na sheria gani? hayo ndo mambo tunatopenda kuyajadili,tuyajue kabla hatujajutia uamzi wetu kama wahenga walivyosema kuwa "majuto ni mjukuu".
Nina jua ndugu zangu tulivyo na msimamo tunapo shupalia jambo
hata ikibidi bila kulitafakari,lakini kuna busara pia kukaa chini na kutafakari
serikali haitawaliwi na wakristo tu wamo waislamu pia ambao wanaunga msimamo huo wa serikali, sasa basi hii mbinde inatokana na nini ndo maana wengine wanaanza kuwa na wasiwasi kuwa kuna ajenda ya siri ndani yake.
mnataka muanze kukatana mikono kama sharia inavyoagiza?angalieni mtapoteza waumini wakishaona sharia zingine za ajabuajabu,
 
Hata hivyo mkae mkijua kuwa suala hili ni sera rasmi ya CCM. Kwa wale wanachama wa CCM nashangaa mnabishania humu, hamkubishana wakati inaingizwa kwenye sera rasmi za chama chenu.

Vile vile CCM imeamua kuvizuia vyama vingine visiwe na sera za kidini. Hii sera ya kuwaletea waislam mahakama zao, kama CUF wangeibeba tokea mwanzo ingewasaidia sana. Sasa CUF kikasemwa sana ooo ni chama cha kidini. Sasa CCM wameweka sera hii rasmi kwenye sera zao. Sidhani kama itakuwa kosa vikitokea vyama vya kutetea haki za wasiokuwa waislam maadam CCM imeshajiweka kwa waislam.
 
Kuna baadhi ya tips kuhusu kadhi's court kwenye hii discussion ya wenzetu hapo kenya nimezisoma hapa http://www.constitutionnet.org/files/KERE02-535.pdf.
Nimekatakata ili kuweka issues za kadhi's court tu. mjaribu kuogelea hapo mnaweza kupata chochote

Let us then move to Article 192, the High Court; Mahakama kuu na inasema hivi: "Mahakama Kuu inajumuhisha
(a) Jaji kiongozi wa Mahakama
(b) Idadi ya Majaji wasiopungua hamsini kama itakavyoelezwa na sheria ya Bunge.
2. Jaji Kiongozi anaweza, kwa kushauriana na Jaji Mkuu, kuunda vitengo vya Mahakama kuu na kufafanua mamlaka ya kisheria ya vitengo hivyo." Hapo chini kuna mamlaka ya kisheria ya mahakama kuu na mnaweza kusoma. ………………………………………………..
I want now to take you to the Kadhi's Court and that is in Article 199 na inasema hivi; Mahakama za Kadhi "Kuna mahakama za Kadhi, ofisi ya Kadhi Mkuu, ofisi ya Kadhi mwandamizi na ofisi ya Kadhi.
Kutakuwa na idadi isiyopungua thelathini ya Makadhi wengine kama itakavyofafanuliwa na sheria za Bunge.
Kadhi amewezeshwa kushikilia Mahakama ya Kadhi inayojulikana kama Mahakama ya Kadhi ya wilaya akiwa na uwezo wa kisheria katika wilaya moja au wilaya nyingi kama inavyofafanuliwa chini ya au na sheria ya Bunge.
Then we have qualifications but before I go to qualifications of Kadhis, I want to take you to qualifications for appointment of Judges, Article 195 page 24. If you read the qualification for the appointment of Judges, just go to article 195 b and c and you will find some conditions, which the new Constitution is recommending for the
………………………………………….
………………………..
2. On attaining the retirement age, a Judge of the Superior Courts of record may continue in office for a period not exceeding six order to enable the Judge to deliver judgement or perform any other functions related to proceedings that were commenced before the judge prior to attaining the age of retirement. So that is about the age of retirement na ukiwa una maoni fulani, you are free to give it.
The kadhi's courts that I have read to you, our brothers of the Muslim community felt that their interests also need to be catered for in terms of Islamic or Muslim interpretation and therefore we have decided to level the courts up to the level of the high court but I would like to read qualification for appointment of Kadhis in Article 202, for the interest of the Muslim community. We are recommending the following
1. A person is qualified to be appointed as Chief Kadhi if that person
(a) is a Muslim of not less than thirty-five years of age
(b) is an advocate of the high court of Kenya of at least ten years experience as a legal practitioner and has attended and obtained a recognized qualification in Muslim Personal Law application to any sect or sects of Islam from a recognized University.
(c) has obtained a degree in Islamic Law from a recognized University and has not less than 10 years in the practice of Islamic law or has held the office of a Kadhi for a similar period.
………………………………………………….
……………………………………………………..
The High Court Kadhi: The Muslims have been given the power to have a High Court. Now, you know the rules of Muslims are able to sentence somebody got in illegal sex, someone gets buried while standing to the head and the Constitution is saying there is no difference. How are we going to do it if the High Court and Chief Kadhi are able to profer their laws?
They will actually seal the sentence. Thank you very much, that is my contribution.

unaweza fungua link hapo juu upate zaidi

Hiyo habari ya Wakenya wapelekee wao. Juzijuzi waislamu wa Kenya walitaka mambo ya Kadhi yaingizwe kwenye Katiba ya Kenya! Unafikiri ukiwapa mahakama za kadhi ndio wataridhika? That will not be the end of the story. Mwisho wa siku watakuambia nchi ni ya kiislamu tunataka kuweka sharia!
 
hapo kwenye ushauri ndo kabisa wanafunga macho na masikio!
Kodi yangu haiwezi tumika kuhudumia mahakama kama hii.Kama vp ndg zangu waislam mjichangishe wenyewe au mtafute mfadhili wa kugaramia/kuendesha mahakama yenu.
 
wakuu,
kikubwa ambacho wasialam wanagangania kuhusu uanzishwaji wa mahjakama ya kadhi ni upanuzi wa ajira kwao kwa sababu ikianzishwa ni kama mfumo wa mahakama ya sasa ulivyo kwa maana ya mbali na kushugulikia masuala ya kiroho kama wanavyodai lakini hawasemi ni jinsi gani zinavyoendeshwa.

kama baadhi hamjui ngoja niwajulishe.
Kadhi mkuu atakuwa na wasaidizi kwa nchi nzima,watalipwa mishahara na serikali,watakuwa na ofisi,magari na kuingizwa katika ajira rasmi a serikali na taarifa nilizonazo kutoka kwa baadhi ya nchi ambazo utataribu huu upo ni kuwa hakuna mtu nje ya dini hiyo atakayeruhusiwa kuajira katika makakama za kadhi kuanzia kadhi mkuu hadi wa wilaya,Mwanzo.

kwa ufupi ni kuwa ikianzishwa kwa kodi ya waumini wa dini zote itakuwa bonge la ulaji kiajira kwa waislamu ndiyo maana wanakomaa nayo.

USHAURI:Kama wanaona ni muhimu kwa nini wasiaziashe wao wenyewe kwa gharama zao badala ya kugangania kugharamia na serikali

kazi kwenu.

Na wanasheria tayari wanaandaliwa Pale MUM
 
Mkuu hawajaificha, kwani jana wamesema wazi John hawezi kufanya ibada ya muislamu, wakimaanisha hawezi kuwa hakimu wa mahakama hiyo!

Mkuu unacho sahau, baada ya hiyo wataomba wtaalamu pia, hapo wataitaka serikali ianzishe chuo cha kutoa mfunzo kwa mahakimu wa mahakama hizo, ama iwapeleke sauidia? maka? irani? wakajifunze jinsi ya uendeshaji wa mahakama hizo na sheria zake.. yote hiyo hela ya mlipa kodi!

Halafu wanakomaa kweli, nadhani kuna shida sehemu, mtu huwezi dai upendeleo, inadaiwa haki!

Mkuu chuo kipo tayari na watu wanasoma mpaka Sasa Bachelor of Law with Shariah pale Muslim University Morogoro.Kwa hiyo hapo soko la ajira nje nje kwao
 
a) Leta data na research inayoonyesha kwamba waislamu wanahitaji ajira zaidi kuliko wakristo?
b) Wewe ambaye si muislamu unajuaje umuhimu wa mahakama kama siyo ubinafsi na chuki zako..
c) Gharama ngapi serikali ime-finance miradi ambayo inahudumia dini moja (wakristo) waislamu hawakuja na hoja za kipuuzi kama hizi
d) You can postpnent the issue lakini lazima itakuwepo wakati huo itakuwa too late kujadili kwa busara kama sasa

Ni vizuri ukaorodhesha miradi inayohudumia Wakristo tu kuliko kuongelea tu kiujumla
 
Akumbuke kuna memorandum baina ya serekali na makanisa humo serekali inajicoment itasaidi makanisa na mashule hospitali na vyuo vikuu vya makanisa na hauna kikomo ulisainiwa na lowasa
 
huna ukijuacho NAKUHURUMIA.
wakuu, kikubwa ambacho wasialam wanagangania kuhusu uanzishwaji wa mahjakama ya kadhi ni upanuzi wa ajira kwao kwa sababu ikianzishwa ni kama mfumo wa mahakama ya sasa ulivyo kwa maana ya mbali na kushugulikia masuala ya kiroho kama wanavyodai lakini hawasemi ni jinsi gani zinavyoendeshwa.kama baadhi hamjui ngoja niwajulishe. Kadhi mkuu atakuwa na wasaidizi kwa nchi nzima,watalipwa mishahara na serikali,watakuwa na ofisi,magari na kuingizwa katika ajira rasmi a serikali na taarifa nilizonazo kutoka kwa baadhi ya nchi ambazo utataribu huu upo ni kuwa hakuna mtu nje ya dini hiyo atakayeruhusiwa kuajira katika makakama za kadhi kuanzia kadhi mkuu hadi wa wilaya,Mwanzo.kwa ufupi ni kuwa ikianzishwa kwa kodi ya waumini wa dini zote itakuwa bonge la ulaji kiajira kwa waislamu ndiyo maana wanakomaa nayo.USHAURI:Kama wanaona ni muhimu kwa nini wasiaziashe wao wenyewe kwa gharama zao badala ya kugangania kugharamia na serikalikazi kwenu.
 
audhubilah.........!!! je kama hoja yako ni fedha za uendeshwaji hizo mahakama,ndio tatizo ,kwa msemo wako wakristo hawataki fedha zao ziendeshe mahakama hizo.je ule mkataba wa hiyari alioufunga bw E Lowasa kwa na kanisa katoliki, na kufanya serikali mkutoa fungu kubwa la fedha kuhudumia hospitali za kanisa ,mule k zile fedha hakuna fungu la waislamu...?
KHIDMAT DWAAT LISIAMIYAT CENTRE REGISTERED TRUSTEESP. O. BOX 16106, MOB. 0713-290272, 0784-403020.1. Uanzishaji wa Mahakama ya Kadhi utaleta madahara makubwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa vile Wakristo hawagawanyiki katika suala la kuipinga, lakini sisi Waislamu tunagawanyika katika suala hilo. Kwa taarifa yako napenda nikuhakikishie kuwa Waislamu wa Madhehebu ya AnsarSunna HAWAIKUBALI Mahakama hiyo kwa vile wanaelewa kuwa itakuwa chini ya BAKWATA. 2. Pia wanaelewa kuwa miongoni mwa mamlaka ya Kadhi ni kutangaza mwezi wa Ramadhani kufunga na kufungua na wao wanaye Amir wao ambaye hutangaza mwezi kwa kufuata mwezi unaoandama Saudia (Saud Arabia). Kwa maana hiyo katika nchi yenye Kadhi kutokea mtu mwingine nje ya Kadhi kutangaza mwezi ni kosa la jinai.3. Kitu ambacho kitaleta madhara makubwa kuliko mafanikio ingawa AnsarSunna ni kundi dogo lakini wanaburuza kundi kubwa sana la Waislamu, kuliko Taasisi yoyote ya Kiislamu hapa Tanzania kwa vile ushawishi wao ni mkubwa sana katika jamii ya Kiislamu.4. ANSAR SUNNA ndio wanaoendesha Shuura ya Maimam, GAZETI LA AN-NUUR, AL-HUDA, NASAHA na RADIO IMANI. Pia wana ushawishi mkubwa TIMES FM. Je, BAKWATA wana uwezo wa kupambana na vyombo hivyo?5. Je, Serikali inaweza kukabidhi Mahakama ya Kadhi kwa wanaharakati wa Kiislamu? Nina hakika haiwezi kufanya jambo hilo na kama haitofanya hivyo Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinaweza kupata hasara zifuatazo:(a) Wakristo wote wanaweza kujitoa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujiunga katika chama cha CHADEMA ambacho hakina Mahakama ya Kadhi katika Ilani yake.(b) Waislamu wote walioko chini ya Shuura ya Maimamu ambayo ni Mpinzani Mkuu wa BAKWATA wataendelea kuipinga Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kuikumbatia BAKWATA na huku wakiendelea kuiunga mkono CUF, hivyo CCM itajikuta imebakia na Waislamu wanaoiunga mkono BAKWATA tu. Suala la wanaharakati kuipinga Mahakama ya Kadhi ni jambo rahisi sana kwa vile Mahakama ya Kadhi sio madai yao ya msingi.6. Waislamu (wanaharakati) dai lao la msingi ni MGAWANYO SAWA WA MADARAKA. Hivyo Serikali inapounda Wizara, wao hutizama Baraza la Mawaziri, WAISLAMU NI WANGAPI NA WAKRISTO NI WANGAPI NDIO MAANA WANAIUNGA MKONO CUF, KWA VILE CUF IMEELEWA TATIZO LAO NA WAO WAKAJA NA KAULIMBIU YA HAKI SAWA KWA WOTE, yaani kwa Wakristo na Waislamu, wala Ilani ya Uchaguzi ya CUF haisemi lolote kuhusu Mahakama ya Kadhi WALA HAITOSEMA!!7. Pia Waislamu wanaharakati wanaelewa kuwa Mahakama ya Kadhi haina manufaa yoyote kwa Waislamu, kwa vile Zanzibar ipo na WAISLAMU WA ZANZIBAR HAWANA MAENDELEO YOYOTE KUWAPITA WALE WA BARA, NA UISLAMU SI NDOA NA MIRATHI TU WALA MUNGU HASEMI "SOMETHING IS BETTER THAN NOTHING." Huu ni msemo wa Wazungu.8. Mwenyezi Mungu anasema: INGIENI KATIKA UISLAMU WOTE NA MSIFE BALI MMEKUWA WAISLAMU KAMILI (Surat Baqarah ya 2 aya ya 208). Kwa hiyo mimi nikiwa kama Mwislamu nashauri kuwa Mahakama hiyo ISIWEPO kwani haitakuwa na manufaa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) na italeta mgawanyiko miongoni mwa wanachama wako, chukulia mfano Zanzibar, Mufti na Kadhi wanavyopingwa na wanauamsho ambao wanaongozwa na Sheikh Farid hali wanauamsho ndio Shura ya Maimam na Shuura ya Maimam ndiyo Uamsho.KWANINI MASHEIKH WA BAKWATA WANAITAKA?9. Wanaelewa wanachokifanya, wao wanajua fika kuwa Serikali itakapoanzisha Mahakama ya Kadhi watakuwa wamepata AJIRA, kwa hiyo wao wanapigania maslahi yao tu, hawawezi kuangalia madhara yatakayokikumba Chama Cha Mapinduzi (CCM) na huku wakijua kuwa ushawishi wao ni mdogo katika Jamii ya Kiislamu na hawana hata Miundumbinu ya kuwashawishi Waislamu wote waweze kumkubali Mufti, na hali ya Mufti ameshaweka wazi milango kwa Taasisi zote za Kiislamu na Waislamu waje washirikiane naye.10. Masheikhe hawa wanaelewa kuwa hakuna Hakimu anayehukumu makosa mawili tu, yaani NDOA na MIRATHI, ukiletewa mzinifu huruhusiwi kumhukumu, ukiletewa mwizi huruhusiwi, nk. lakini wanang'ang'ania hivyo hivyo kwa ajili ya mishahara tu na hiyo ni hatari.11. Hujaribu kutoa hata mifano ya Serikali ya Uingereza kwamba mwaka 1920 iliweka Mahakama hizo, ukweli ni kwamba Serikali ya Uingereza haikuweka Mahakama za Kadhi tu bali za Maakida na Maliwali, lakini pia sababu ya kuziweka Mahakama hizo siyo kwa ajili ya kuutunza Uislamu au uliwali bali ilikuwa ni mbinu ya kuwatuliza Viongozi hao ili waweze kuwatawala bila vurugu kwani mkoloni aligundua kuwa ni watu wenye ushawishi katika jamii kwa hiyo ile ilikuwa ni mbinu ya kiutawala ili Masheikhe, Maliwali na Maakida wajione kuwa na wao ni sehemu ya Serikali ya Muingereza, kumbe ni watawaliwa, hivyo bado hoja hiyo haina msingi wowote wala haina maana kwamba Serikali ya Mkoloni ilikuwa nzuri kwa Waislamu kuliko hii ya CCM, na huku tukiambiwa kuwa Waislamu ndiyo walioanzisha harakati za kudai Uhuru, kama walikuwa wazuri kwa nini tuliwaondoa.12. CCM inayo mambo mengi ya kujivunia kwa Waislamu kama vile kuwapatia Chuo Kikuu, na hilo ni jambo muhimu na la msingi kwa maendeleo ya Uislamu na Waislamu, kwa hiyo JAMBO HILO LA MAHAKAMA YA KADHI mnapaswa kuliangalia kwa umakini ijapokuwa limo ndani ya Ilani yenu. Lakini si kila jambo lililomo ndani ya Ilani litekelezwe, mengine yanaweza kushindikana kwa matatizo mbalimbali na hili ni tatizo kubwa KWANI LINAWEZA KUZAA MGOGORO WA KIDINI!!WAKRISTO WANA HAKI YA KUPINGA MAHAKAMA YA KADHI13. Sehemu kama Zanzibar ni rahisi kuweka Mahakama ya Kadhi kwa vile Waislamu kule ni asilimia 99.99 hali kama hiyo Wakristo kule ni kama hawapo wamemezwa kwa uchache wao. Lakini BARA NI PAGUMU kwa vile HUENDA WAKRISTO NI WENGI KULIKO WAISLAMU. KWA VILE WAISLAMU KWA UHAKIKA HUPATIKANA MIKOA ISIYOZIDI SITA AMBAYO NI DAR ES SALAAM, LINDI, TANGA, MTWARA, KIGOMA NA TABORA, pia katika mikoa hiyo siyo Wilaya zote, kwa mfano Mkoa wa Kigoma ni Ujiji na Kigoma Mjini tu.14. Pamoja na hayo Masheikhe wa BAKWATA wanaoshikilia suala la kuwepo kwa Mahakama ya Kadhi bado hawajafahamu nini tatizo la Wakristo, hata hawakubali kuwepo kwa Mahakama hiyo, siyo kweli kabisa kwamba Wakristo hudhani Mahakama hizo zitawahukumu wao, la hasha na Masheikhe hutumia muda mwingi kuwaelimisha juu ya hilo, wakati hilo sio tatizo lao, na ni udhaifu wa kutokujua madai au matatizo ya mpinzani wako, ni nini tatizo la Wakristo ni hili:(a) Mkumbuke kwamba mwaka 1993 hapa Tanzania kulikuwa na mgogoro wa bucha za nguruwe, mgogoro huo ulizaa harakati kubwa za Waislamu ambazo makao yake makuu yalikuwa msikiti wa Mtoro na kiongozi mkuu alikuwa marehemu Kasim bin Juma. Waislamu walipinga kuwepo Ubalozi wa Vatican hapa Tanzania na bado wanaendelea na msimamo huo hadi leo, wakati ubalozi huo hauendeshwi kwa Fedha za walipa kodi wa Tanzania bali ni Vatican yenyewe. JE, ITAKUWAJE LEO WAKRISTO WAKUBALI ZIWEPO MAHAKAMA AMBAZO ZITATOA AJIRA KWA WAISLAMU, KUANZIA MTAA, KATA, TARAFA, WILAYA, MKOA HADI TAIFA, TENA KWA FEDHA ZA WALIPA KODI WA TANZANIA WAKIWAMO NA WAO WAKRISTO? Hilo ndilo tatizo lao na hapo ndipo BAKWATA wanatakiwa wapatolee maelezo.(b) Kwamba, mabilioni ya Watanzania yatakayowalipa Masheikhe kila mwezi nao wao watanufaikaje? Huo ndio mgogoro uliotengenezwa na Ilani yenu na ambao unaweza kuwagharimu katika uchaguzi ujao wa mwaka 2010 ENDAPO WAKRISTO WAKIIGA MFANO WA WAISLAMU WA MSIKITI WA MTORO walipoamua kukusanya Kadi za CCM mwaka 1993 ingawa jaribio hilo lilizimwa na Viongozi wa CCM.HOJA ZA SHEIKH BASALEH15. Sheikh Ali Basaleh ndiye ambaye amelielewa tatizo la Maaskofu ingawa ametoa mfano mzuri wa kuwatuliza katika kipeperushi chake cha Wito cha tarehe18/08/2006. Ijumaa kuwa kama mtu ana watoto wawili mmoja anakula sana na mwingine hali sana, Je, baba atamzuia yule anayekula sana ili alingane na yule asiyekula sana? Mfano wake ni mzuri lakini haufanani na tatizo lililopo kwani fedha za baba hazichangiwi na watoto wake, bali baba huzitafuta yeye mwenyewe kwa nguvu zake, LAKINI FEDHA ZA BABA SERIKALI ZINATOKANA NA KODI YA WAISLAMU NA WAKRISTO, HIVYO SERIKALI HAIPASWI KUTUMIA FEDHA NYINGI KWA DINI MOJA LAZIMA ITALETA MGOGORO NA NDIYO MAANA SISI WAISLAMU TUMEKUWA TUKIDAI HAKI SAWA!16. Katibu Mkuu ni matumaini yangu kuwa hekima itatumika katika kulitatua tatizo hilo kwani ni rahisi kuziba ufa kuliko gharama za kujenga ukuta mwisho nakutakia kazi njema pamoja na afya njema.WABILAH TAUFIQ,ASANTE.USTADH A. S. MKAMBAKU,KATIBU MKUU.
 
Mkuu chuo kipo tayari na watu wanasoma mpaka Sasa Bachelor of Law with Shariah pale Muslim University Morogoro.Kwa hiyo hapo soko la ajira nje nje kwao

hao ndiyo waliopiga kambi Dodoma Bungeni
 
audhubilah.........!!! je kama hoja yako ni fedha za uendeshwaji hizo mahakama,ndio tatizo ,kwa msemo wako wakristo hawataki fedha zao ziendeshe mahakama hizo.je ule mkataba wa hiyari alioufunga bw E Lowasa kwa na kanisa katoliki, na kufanya serikali mkutoa fungu kubwa la fedha kuhudumia hospitali za kanisa ,mule k zile fedha hakuna fungu la waislamu...?
wewe mbulula, tatizo ninyi huwa hamuwajui wakristo, mnafikiri kila mkristo ni MKATOLIKI. zaidi ya wakristo milioni 10 Tanzania sio wakatoliki. hivyo kama kuna mkataba ulishafanywa na katoliki, ujue kuna wakristo wengine wengi sana hawajapata kama msivyopata ninyi, na zaidi ya yote, hospitali za katoliki ninyi huwa mnatibiwa, (mahakama zenu hazituhusu hivyo msitumie pesa zetu) hospitali mnatibiwa kila siku na mkiumwa haya maswali huwezi kuuliza hadi upone. NINYI HAMNA HOSPITALI NYINGI NA BORA, serikali yenu pia haina ndio maana inaomba msaada tu kwa wakatoliki kuzifanya hospitali zao kuwa designated walau ziwafaidishe hata ninyi. kwenye hospitali za kikristo na mashule ya kikristo tungeingia kwa vitambulisho kukagua dini ninyi wote mngetegemea waganga wa kienyeji na mashehe wauza majini na wapunga upepo kina sheh yahya kwasababu hamna hospitali na uwezo huo hamna. kama mnao prove it basi, anyeni kazi. nchi hii tumeishi kwa kuchukuliana siku zote na wakristo huwa hawawabagui waislam, tatizo ninyi malalamishi sasa...kumbe uvivu wa kufikiri na kufanya kazi.
 
Ukweli kinachotafutwa ni ajira. Hivi vijana wanaohitimu chuo chao cha Morogoro haswa Sheria za Kiislam huwa wanaenda wapi?
 
Ukweli ajira ndiyo inayotafutwa. Wahitimu wa Sharia chuo chao cha Morogoro huwa wanapotelea wapi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom