Tathmini: Lowassa amemfunika Dr. Slaa



Mzee tupatupa, kuna mahali padogo tu umesahau. Mwaka 2010 Dr. Slaa alipata 27 point somethimg percent, lakini kumbuka wakati ule alisimama peke yake sio kama ilivyokuwa kwa lowassa mwaka huu Lowassa amechukua kura za vyama vinne. prof Lipumba naye alikuwa na asilimia zake kupitia CUF 2010 na Hashim Sipunda naye alikuwa na asilimia zake kupitia NCCR. Ukichanganya za hao wote mwaka 2010 utapata ukweli na hesabu halisi iliyoongezeka kwa lowassa. Lakini vilevile usisahau za NLD.

Lakini kumbuka watu walianza kuiona chadema imeanza kuonyesha upinzani wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2014. na hii nayo hujaiweka kwenye tathimini yako, ukifanya mahesabu sahihi, utagundua kwamba Lowassa amevuruga mwenendo mzuri wa chadema uliokuwepo na hakuna alichoongeza
 
Hivi mamlaka ya Kikwete mwaka huu haujayaona kwenye uchaguzi huu?
 
Hii hoja haiwezekani. Ni kitu gani kinakuaminisha kwamba wapenzi wa Lipumba na Slaa walimpigia Kura Lowassa hasa baada ya Slaa na Lipumba wenyewe kujitokeza hadharani kumpinga Lowassa na, especially Dr. Slaa kuwashawishi wapenzi wake wamchague Magufuli?
 

Ok, kama ni nguvu ya pesa wewe ulipewa kiasi gani?.....ni kampeni gani tanzania utafanya bila kuwa na pesa?....kama ni nguvu ya ukawa unajua 2010 Prof. Lipumba alikiri kumsadia Rais Kikwete?
 

Huyo Prof. Lipumba aliwahi kukili kwa 2010 alimsaidi Kikwete
 
Ok, kama ni nguvu ya pesa wewe ulipewa kiasi gani?.....ni kampeni gani tanzania utafanya bila kuwa na pesa?....kama ni nguvu ya ukawa unajua 2010 Prof. Lipumba alikiri kumsadia Rais Kikwete?

Ndugu yangu hanunuliwi kila mtu "Wananunuliwa watu wenye ushawishi kwenye jamii".Mfano Mbowe na Gwajima.Ukishamnunua Gwajima umenunua waumini wake wote maana wanamwamini balaa.Ukishamnunua Mbowe umenunua wafuasi wake wote.Ndivyo Ilivyo.Hapa sizungumzii fedha za kampeni nazungumzia fedha za kuwalipa WAPAMBE na TEAM.
 
Hahaha...watu wanasahau mizizi iliyojengwa na Slaa kwa kuzunguka nchi nzima kila kata ....Lowasa kakuta taasisi ingawa tayari ilikuwa vipande baada ya kuona misingi inakiukwa na baadhi ya viongozi walioaminika ...Bila kusahau Slaa alisimama bila kuungana na chama chochote ....na mchango wa mitandao ya kijamii ktk uchaguzi huu ...
 
wewe lala mbele,kumbuka enzi zile hakukuwa na ukawa,nakuambia kwa mwamvuli wa ukawa Dr Slaa ndo ANGESHINDA uRAIS WA NCHI HII,
 

Mkuu tunapozungumzia dr slaa na lipumba maana yake tunazungumzia cuf na chadema na ndio maana tunasema lowassa alisimama kwa mwamvuli wa ukawa kwa mantiki hiyo lazima utambue kuwa mtaji alioingia nao lowassa ni mtaji unaojumlisha vyama vyote vilivyokwenye muungano na si chadema peke yako hivyo wapenzi, washabiki na wanachama wote kwa umoja wao walimpa kura lowassa wakiwa na imani watavuna kikubwa zaidi sasa chakujiuliza hicho kilichopatika kina tija kiasi cha kufanya kubadilisha gea juu kwa juu na kwa mtazamo wako hapo tumepata au tumepatikana kwa jinsi matokeo yalivyo mpaka sasa?
 
Angalia uwiano wa kura, siyo idadi ya kura...maana yake linganisha 26.34% za Slaa dhidi ya 39.97% za Lowassa.

Usijumlishe % za slaa tu jumlisha za lipumba na za nccr jumla kuu ni % ngapi ndio ulinganishe na za lowassa hapo ndio utapata jibu kama lowassa amefanya vizuri au laa!!
 
Ni kura za Urais Mkuu. Mwaka huu, viti maalum vitapatikana kwa CCM na CHADEMA tu.

Mzee Tupatupa

Sio kweli, viti maalum vinaangalia kura za ubunge, kasome katiba, hata hivyo chadema bado itaongeza viti kwani wamepata kura nyingi za wabunge pia
 
Usijumlishe % za slaa tu jumlisha za lipumba na za nccr jumla kuu ni % ngapi ndio ulinganishe na za lowassa hapo ndio utapata jibu kama lowassa amefanya vizuri au laa!!
Na unaonaje tukiweka factor ambayo ita-estimate kura zilizopungua kutokana na Dr. Slaa kuwaambia wale wanaomkubali wampigie kura magufuli? Plus za wapenzi wa Lipumba ambao kwa kuona mtu wao 'ameonewa' waliamua kutopiga kura kabisa au kumpigia kura magufuli?
 
Saluteeeee!!!!mkuu, kweli maendeleo yanakuja kama tutakuwa tunawaza positivity kama wewe, mawazo murua kabisa na mm mwana ccm lakin jana sikushangilia kabisa ikitegemea napenda fair play, naomba Rais wangu alete mabadilko ndani ya ccm ili tusije kutapatapa tena kama mwaka huu huko mbele, rasilimali kubwa tumetumia mavuno kidogo, upuuzi kabaisa
 

Kwa hiyo tunakubaliana kuwa dr na lipumba walikuwa na ushawishi mkubwa na tulifanya kosa kubwa kubadili gea juu kwa juu na madhara yake ndio haya tunayoanza kuyaona sasa?
 
hili lingejadiriwa na wapinzani nadhani lingekuwa na tija lkn kama fisiem afu unaanza kufanya tasmini ya kushinda au kushindwa kwa ukawa sikuelewi kabisaaaaa
faida ya slaa vs lowassa ni sisi ukawa tunajua plus kuanza kutufundisha namna ya kuendesha chama /ukawa wetu nakushangaaa sana ?????????does make sense to train your enemies??????
 
Kwa hiyo tunakubaliana kuwa dr na lipumba walikuwa na ushawishi mkubwa na tulifanya kosa kubwa kubadili gea juu kwa juu na madhara yake ndio haya tunayoanza kuyaona sasa?
Kila mmoja anao ushawishi, hapa suala ni nani mwenye ushawishi zaidi. In this case bado naona Lowassa alikuwa na ushawishi zaidi maana pamoja na Lipumba na Slaa kuhamishia kura za wapenzi wao CCM na ACT, bado Lowassa ameweza kupata 40% (assuming hizo ndizo alizopata kweli).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…