Zanzibar 2020 Tathmini fupi mara Baada ya uteuzi wa Dkt Hussein Mwinyi huko NEC ya CCM

Nchi ni moja, Chama ni kimoja, Halmashauri kuu ya Taifa ni moja, kama Bunge lilivyo moja! huwezi kusema leo tunajadili issue ya Zanzibar wengine wote msiotoka Zanzibar tokeni mtupishe! Naomba uzoefu wa vyama vingine kama Chadema, CUF ,NCCR , ADC ,Jahazi Asili vyote hivyo vilifasimamisha wagombe urais Zanzibar , je ukifika wakati wa maamuzi huwa wanafakuza wajumbe wa vikao vya maamuzi wabaki wa Zanzibar tu?!
Mnakosea sn......rais wa Zanzibar ilitakiwa wamteue wenyewe wazanzibari tena hukohuko kwao Zanzibar.........

Ona sasa mwinyi kateuliwa na wabara lkn kuanzia viongozi hadi wananchi hawataki kusikia kitu kinachoitwa mwinyi.........
 
Si kweli. Majina yote yamependekezwa na Kamati Maalum ya NEC. Hao ni Wazanzibari watupu. Majina hayakubuniwa Dodoma! Hata hivyo hakuna chama makini cha siasa ulimwenguni kinachoachia sehemu ya nchi imteue mwakilishi wake muhimu bila kuhusisha ngazi ya taifa. Inatokea sasa hivi chaguzi za Amerika kwa maseneta wa majimbo (states).
Hapana mkuu mnakosea sn na mnawanyanyasa sana wazanzibari......
Rais wa Zanzibar inatakiwa wachague wenyewe wazenji tena huko huko kwao labda huku wangemwalika tu mwenyekiti wa ccm kushuhudia Basi inatosha.....

Unaona sasa watanganyika mmewalazimishia mwinyi ambaye hakuna mzamzibari anamtaka?
 
Mimi iki kitu ndio huwa sielewi mgombea wa uraisi zanzibar anapitishwa na nec bara ..kwa nini nec zanzibar wasikae wakapitisha mtu wao huko ndio aje bara wasalimu
Kamati Maalum ya CC ya CCM Zanzibar ndio humaliza kazi na kuleta majina yasiyopungua matatu kwenye Halmashauri ya Taifa ya CCM. Humowamo wote wa Bara na wa Visiwani, na kwa kuwa wa Visiwani wameshaleta hayo majin, ambayo kimsingi ni chaguo lao, basi huku NEC na kwenye Mktano Mkuu ni kupitisha jina moja ambalo halileti tafrani kwa wahusika - yaani Wazanzibari ila ninyi ndio mnaona tofauti. Huu ni utaratibu wa miaka yote na wanaoupinga ni wahafidhina wachache amabao hawamzuii mwenye nyumba kupata usingizi!
 
Mnakosea sn......rais wa Zanzibar ilitakiwa wamteue wenyewe wazanzibari tena hukohuko kwao Zanzibar.........

Ona sasa mwinyi kateuliwa na wabara lkn kuanzia viongozi hadi wananchi hawataki kusikia kitu kinachoitwa mwinyi.........
Kakwambaia nani au umetumwa kutaka kuwachanganya wana Zanzibar au unawasemea wale ambao tayariwameshindwa kwa kusikia tu, kateuliwa Dr. Mwinyi kupeperusha bendera ya CCM Zanzibar?
 
Hata ukiingia ndani Unguja Kusini kwa mfano, utakuta bado wanabaguana kati ya Makunduchi, Jambiani na Dimbani
Hata bara hayo kaleta yesu wa chato! Msukuma ni daraja la kwanza, Mnyamwezi daraja la pili, wote wanaotoka kanda ya ziwa ni kuondoa wasukuma na wanyamwezi ni daraja la tatu,
Wengine wote hawana daraja!
Wengine siyo binadamu hasa kaskazini. "msiwabolee nyumba kwa sababu walinipigia kura".
October tuunganishe nchi yetu!
 
Kakwambaia nani au umetumwa kutaka kuwachanganya wana Zanzibar au unawasemea wale ambao tayariwameshindwa kwa kusikia tu, kateuliwa Dr. Mwinyi kupeperusha bendera ya CCM Zanzibar?
Ccm ina mwenyewe mkuu ujue hilo......lkn tuyaache tu kwanza
 
Ccm ina mwenyewe mkuu ujue hilo......lkn tuyaache tu kwanza
Huo ni usemi mfu, ulizikwa with the entry of the current CCM Chairperson, Dr. Magufuli, the President of the United Republic of Tanzania. Wenye CCM ni wanachama hai, wapenzi na wakereketwa wake wote Tanzania nzima.
 
Huo ni usemi mfu, ulizikwa with the entry of the current CCM Chairperson, Dr. Magufuli, the President of the United Republic of Tanzania. Wenye CCM ni wanachama hai, wapenzi na wakereketwa wake wote Tanzania nzima.
Hakuna kitu km hicho......maamuzi yote saaizi ni ya mtu mmoja mengine ni maigizo tu......

Ccm ina mwenyeweeee.....
 
Back
Top Bottom