TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
TATHMINI; siku 10 za Kampeni ya Dr John Magufuli.
Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dr John Pombe Magufuli amehitimisha mzunguko wa Kwanza wa Kampeni yake kwa mikoa 6 ya kanda ya Nyanda za Juu Kusini na Kanda ya Kusini ambayo ni KATAVI, RUKWA, MBEYA, NJOMBE, RUVUMA na MTWARA.
Katika kampeni zake Dr Magufuli amefanya mikutano ya hadhara takribani 49 pamoja na mikutano midogo ya kusalimia wananchi zaidi ya 126 ambapo katika mikutano yote wananchi walijitokeza kwa Maelfu kumsikiliza akiwasilisha Ilani ya CCM ya 2015-2020.
Dr Magufuli ametembea takribani Kilometa 5,900 kwa kutumia gari na maeneo mengine akitembea kwa miguu ili kukutana na Wananchi wa Makundi mbalimbali akinadi sera za CCM.
Tafiti za awali za Mashirika mbalimbali ya nje na ndani ya nchi yalionyesha kuwa CCM itashinda uchaguzi wa mwaka 2015 kwa zaidi ya asilimia 60, lakini baada ya kuanza kwa Kampeni na mgombea kuzunguka akifanya mikutano mikubwa ya hadhara ambayo imekuwa ikirushwa moja kwa moja (live) kupitia vituo mbalimbali vya televisheni, magazeti, redio pamoja na mitandao ya kijamii na kuwafikia watanzania takribani milioni 30, Umaarufu wa CCM na uwezekano wa kushinda umeongezeka kufikia asilimia 85 (tafiti za ndani)
Mambo yaliyopelekea CCM kuongeza umaarufu wake ni pamoja na rekodi nzuri ya uadilifu na uchapakazi aliyonayo mgombea wake, pamoja na uwezo mkubwa wa mgombea (Dr Magufuli) katika kutambua na kutoa suluhu ya matatizo yanayowakabili wananchi wa kada zote na maeneo yote ya Mijini na Vijijini.
Ilani ya CCM na namna mgombea anavyoinadi (Body language) imeongeza imani ya wananchi kwa CCM, mfano Dr Magufuli akisema anaichukia rushwa, mwili, haiba na sura yake vinaonyesha kuwa anamaanisha anachokizungumza. Ilani ya CCM imejikita katika kuleta mabadiliko kwa kuondoa Umasikini na kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira hasa kwa Vijana, kuendeleza Vita dhidi ya Rushwa na Ubadhirifu, Kuboresha huduma za jamii na kuendeleza Umoja wa Kitaifa pamoja na kudumisha Ulinzi na usalama.
Wakati Umaarufu na kukubalika kwa CCM kunaongezeka, bado inapata upinzani hafifu ktk kampeni zake. Rekodi zenye mashaka za wagombea wao zinazohusisha kashfa za rushwa, ufisadi, utendaji mbovu na uzembe. Hali tete na migogoro ya ndani ya vyama vya Upinzani ambayo imeshika kasi ktk kipindi hiki hasa kuhusu wagombea kwa nafasi ya Urais na baadhi ya majimbo. Hali ya Afya za wagombea wao ambazo zimewafanya kutoweza kufika katika baadhi ya maeneo waliyopanga kufanya mikutano mfano Ludewa na Tunduru ambapo wananchi walishakusanyika na mgombea akashindwa kutokea. Vyama vya upinzani kukosa Ilani madhubuti na hivyo wananchi kupunguza imani yao kwao.
NB;
Katika moja ya utaratibu bora kabisa wa Chama Cha Mapinduzi ni ule wa kujifanyia tathmini katika kila hatua ya mpango ama jambo lake lolote, utaratibu huu umeiwezesha CCM kubaki kuwa relevant na kuendelea kuaminiwa na kupendwa na watanzania walio wengi.