SDP_TZ_Mpya
Senior Member
- Jun 21, 2013
- 166
- 77
Taarifa za kwenye CCM zilithibisha kuwa Wassira yuko 'very serious' kwenye kusaka Urais 2015. Hoja yake ni kuwa yeye ni msafi kuliko akina Lowassa. Kura alizopata NEC na kumfanya aongoze zinamtia wazimu. Anadai Ikulu ya sasa inamkubali na anaweza kutumika ku-neutralise uhasama wa akina Sitta, Membe na Lowassa.
Hata hivyo, imefahamika kuwa kwa sasa ameamua kuikumbatia TASAF iliyo chini ya uratibu wake kuhakikisha inamwingiza Ikulu. Ikumbukwe kuwa TASAF imefika kila kona ya nchi na mbunge na mjumbe wa CCM wilaya lazima ajitahidi kumuunga mkono ndipo mradi wa TASAF uje kwenye eneo lake. Na yeye baadae hutembelea miradi hiyo huku akipokea kiapo cha mpokea mradi cha kumuunga mkono yeye Wassira 2015.
Inajulikana wazi kuwa ni mtindo huu ndio uliompa Wassira kura nyingi wakati wa uchaguzi wa NEC mwaka jana Dodoma. Ukiangalia kutoka pembeni, hakuna tofauti na ufisadi mwingine wowote.
Hata hivyo, imefahamika kuwa kwa sasa ameamua kuikumbatia TASAF iliyo chini ya uratibu wake kuhakikisha inamwingiza Ikulu. Ikumbukwe kuwa TASAF imefika kila kona ya nchi na mbunge na mjumbe wa CCM wilaya lazima ajitahidi kumuunga mkono ndipo mradi wa TASAF uje kwenye eneo lake. Na yeye baadae hutembelea miradi hiyo huku akipokea kiapo cha mpokea mradi cha kumuunga mkono yeye Wassira 2015.
Inajulikana wazi kuwa ni mtindo huu ndio uliompa Wassira kura nyingi wakati wa uchaguzi wa NEC mwaka jana Dodoma. Ukiangalia kutoka pembeni, hakuna tofauti na ufisadi mwingine wowote.