PreGE2025 Tarimba ataka CCM kumchukulia hatua Askofu Gwajima

PreGE2025 Tarimba ataka CCM kumchukulia hatua Askofu Gwajima

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
20,725
Reaction score
31,305
Ameongea kwa uchungu mkubwa sana leo Bungeni. Na mimi naunga mkono. CCM Kinondoni iandae kongamano la kumlaani Gwajima, hata mimi ntachangia gharama za mkutano huo.

Ajibiwe na ngazi ya wilaya na mkoa tu ili ajue hiyo ni level yake, akiwa anataka ajibiwe na ngazi ya taifa. CCM Wilaya inamtosha huyo

Mimi chiembe napendekeza afukuzwe uanachama wa CCM, na kanisa lake lililojengwa eneo la wazi libomolewe akatafute eneo nje ya mji
================
Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Mhe. Abbas Tarimba, amekitaka Chama cha Mapinduzi (CCM) kumchukulia hatua za Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima, kupitia Kamati ya Maadili ya chama hicho, kufuatia kauli alizotoa dhidi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2025/2026, leo Mei 26, 2025, bungeni jijini Dodoma, Mhe. Tarimba amesema kauli za Gwajima kuhusu madai ya utekaji ni za kudhalilisha na hazikubaliki, hasa pale zinapogusa familia ya Rais.

Soma Pia: Askofu Gwajima: Wakuu wa Vyombo vya Usalama wasiondolewe kwenye nafasi zao kwa mapenzi ya mwanasiasa aliyewaweka

"Naiuliza CCM, huyu mtu bado ana kadi ya chama chetu, kwa nini awe huru kuendelea kutoa maneno ya fedheha kwa Rais wetu? Anatoa mifano ya kutisha, ya kumkosea heshima Rais na familia yake. Unamtaja mtoto wa Rais, ukisema atobolewe macho, hivi kweli unaelewa uchungu wa mzazi?" amehoji Tarimba.

 
Ameongea kwa uchungu mkubwa sana leo Bungeni. Na mimi naunga mkono. CCM Kinondoni iandae kongamano la kumlaani Tarimba, hata mimi ntachangia gharama za mkutano huo.

Napendekeza afukuzwe uanachama wa CCM, na kanisa lake lililojengwa eneo la wazi libomolewe akatafute eneo nje ya mji
Wewe nawe unaunga mkono watu kufukuzwa kwenye chama? Si wafanye watakavyo kwakuwa ccm kuna demokrasia? Unayakumbuka matamshi na uchonganishi wako dhidi ya KINA MCHOME na chama chao?
Gwajima amelonga asikilizwe, aeleweke AJIBIWE Kwa hoja siyo viroja!
Kanisa lake linahusu nn hapa?
 
Ameongea kwa uchungu mkubwa sana leo Bungeni. Na mimi naunga mkono. CCM Kinondoni iandae kongamano la kumlaani Gwajima, hata mimi ntachangia gharama za mkutano huo.

Napendekeza afukuzwe uanachama wa CCM, na kanisa lake lililojengwa eneo la wazi libomolewe akatafute eneo nje ya mji
Watafuna nchi ndio wenye uchungu kuhatarishwa kwa daraka zao.
 
Bibie aache kutumatuma machawa apande jukwaani atueleze ni kwanini anauwa Watanzania.
Wanasema anatumia vijana wa KZMKZ
 
Back
Top Bottom