Tariffs za TANESCO zipoje?

Tariffs za TANESCO zipoje?

NileSat

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2015
Posts
340
Reaction score
182
Wakuu scale ya malipo ya hili shirika letu la umeme lipo vipi? Naelewa Wateja Wa D1 ni wale wanaotumia chini ya unit 75 kwa mwezi na wanauziwa unit 100 je nini tofauti ya T1 na T2 customers? na bei za unit kwa T1 na T2 zipoje? na hawa wanaochukua 11KV au 132KV wao wapo kundi gani na wanauziwaje unit?
 
Wakuu scale ya malipo ya hili shirika letu la umeme lipo vipi? Naelewa Wateja Wa D1 ni wale wanaotumia chini ya unit 75 kwa mwezi na wanauziwa unit 100 je nini tofauti ya T1 na T2 customers? na bei za unit kwa T1 na T2 zipoje? na hawa wanaochukua 11KV au 132KV wao wapo kundi gani na wanauziwaje unit?


Asante sana kwa swali, Kuna tariff T1 ambayo ni kwa ajiri ya wateja wa kawaida (Normal use category) hawa ni wateja wanao tumia umeme kuanzia unit 0 - na kuendelea haina mwisho. Gharama ya umeme kwa wateja hawa ni Tsh. 298 kwa Unit na wanalipia service charge 5520+ 22% ( 22% ni VAT = 18, EWURA - 1% na REA-3%)

Tariff 4 ni kwa ajiri ya low usage customers, hawa matumizi yao kwa mwezi kuanzia unit 0-75. Gharama ya umeme ni Tsh 100 kwa unit bila service charge. Ukiwa upo tariff 4 ukatumia unit zaidi ya 75 zile unit zilizozidi utalipia Tsh 350 + 22% ya VAT.
 
Asante sana kwa swali, Kuna tariff T1 ambayo ni kwa ajiri ya wateja wa kawaida (Normal use category) hawa ni wateja wanao tumia umeme kuanzia unit 0 - na kuendelea haina mwisho. Gharama ya umeme kwa wateja hawa ni Tsh. 298 kwa Unit na wanalipia service charge 5520+ 22% ( 22% ni VAT = 18, EWURA - 1% na REA-3%)

Tariff 4 ni kwa ajiri ya low usage customers, hawa matumizi yao kwa mwezi kuanzia unit 0-75. Gharama ya umeme ni Tsh 100 kwa unit bila service charge. Ukiwa upo tariff 4 ukatumia unit zaidi ya 75 zile unit zilizozidi utalipia Tsh 350 + 22% ya VAT.

nashukuru sana kaka
 
Aksante sana kwa muuliza swali na mtoa jibu, hii ndiyo tunayoihitaji kwa Forum hii, maana maswali yapo clere na jibu ni sahihi na kujitosheleza kwa ufupi, natumai hata majibu kuhusu utofauti wa T1,T2 na wanaotumia 11KV & 132KV utadadavua vizuri kwa faida ya wengi na general gharama zake. Na utusaidie ni taratibu zipi zitumiwe kwa mtu kuhama Tariff, maana ukienda kuunganisha umeme kwa mara ya kwanza hope unapewa T1, Sasa unajikuta matumizi ni ya kawaida so ufanyeje? Otherwise thanks mjibu maswali@ Koleba
 
Baada ya ufafanuzi wa lugha na mizani, tutaenda sasa kwa watungaji utaratibu ili tupate scientific justification ya rationality and fairness ya hizi rates.
 
Asante sana kwa swali, Kuna tariff T1 ambayo ni kwa ajiri ya wateja wa kawaida (Normal use category) hawa ni wateja wanao tumia umeme kuanzia unit 0 - na kuendelea haina mwisho. Gharama ya umeme kwa wateja hawa ni Tsh. 298 kwa Unit na wanalipia service charge 5520+ 22% ( 22% ni VAT = 18, EWURA - 1% na REA-3%)

Tariff 4 ni kwa ajiri ya low usage customers, hawa matumizi yao kwa mwezi kuanzia unit 0-75. Gharama ya umeme ni Tsh 100 kwa unit bila service charge. Ukiwa upo tariff 4 ukatumia unit zaidi ya 75 zile unit zilizozidi utalipia Tsh 350 + 22% ya VAT.
Hapo kidogo nachanganyikiwa kuna site yangu moja nimefunga mita tangu mwezi wa 7 na umeme tunatuumia kwa mwezi unit 55-62 lakini mbona bado kila nlinunua umeme nakatwa service charge??? Wakati sifikishi hizo unit 75 na unit zenyewe naona bado nauziwa kwenye bei ya 300+ kwa unit nifanye nn ili niingizwe kwenye kundi hilo la watumiaji chin ya unit 75??? Na sijawahuhi vuka zaid ya unit 70 tangu mita ifungwe msaada hapo jaman??
 
Aksante sana kwa muuliza swali na mtoa jibu, hii ndiyo tunayoihitaji kwa Forum hii, maana maswali yapo clere na jibu ni sahihi na kujitosheleza kwa ufupi, Na utusaidie ni taratibu zipi zitumiwe kwa mtu kuhama Tariff, maana ukienda kuunganisha umeme kwa mara ya kwanza hope unapewa T1, Sasa unajikuta matumizi ni ya kawaida so ufanyeje? Otherwise thanks mjibu maswali@ Koleba
Koleba Mkuu saidia na hilo swali kwani hata mm linanihusu
nimefungiwa meter za LUKU (Wasion ya China) ikinisomea kwa T1 Novemba 2015
mwezi Disemba nikasoma ni Unit45
nikajaza Unit 62 nimeambia nika miezi mitatu ndio niende kulalamika
  • Mm nilikuwa T4 ni kwanini nikalalamike tena wakatu situmii frji nk
  • hicho kiremote kinasoma Error 77 na hakioneshi zimebaki au maandishi yoyote je kitakata au nikaripoti?
 
Aksante sana kwa muuliza swali na mtoa jibu, hii ndiyo tunayoihitaji kwa Forum hii, maana maswali yapo clere na jibu ni sahihi na kujitosheleza kwa ufupi, natumai hata majibu kuhusu utofauti wa T1,T2 na wanaotumia 11KV & 132KV utadadavua vizuri kwa faida ya wengi na general gharama zake. Na utusaidie ni taratibu zipi zitumiwe kwa mtu kuhama Tariff, maana ukienda kuunganisha umeme kwa mara ya kwanza hope unapewa T1, Sasa unajikuta matumizi ni ya kawaida so ufanyeje? Otherwise thanks mjibu maswali@ Koleba


T1 hili hujumuisha wateja wadogo wenye matumizi ya kawaida ndio Kama nilivyoeleza (tariff 1)

T2 kundi hili linahusu wateja wenye matumizi ya kawaida ambapo umeme hupimwa kwa msongo wa 400V na matumizi ya wastani ni 7500kWh kwa mwezi. Mahitaji hayazidi 500kVA kwa kipindi cha mwezi mmoja.

T3 kuna medium Voltage na High Voltage, T3 Medium Voltage inatumika kwa wateja waliounganishwa kwenye msongo wa Kati na umeme unapinwa kwa KV11 na zaidi. T3 high Voltage inatumika kwa wateja waliounganishwa kwenye msongo mkubwa, umeme unapimwa kwa KV132 na zaidi.

T2 na T3 ni kwa ajiri ya wateja wakubwa (viwanda) na mita wanazotumia ni AMR mita.

D1 ndio T1(tariff 4) na T1 ndio (tariff 1). Hizo zipo kwa ajiri ya wateja wa majumbani.

Kubadilisha tariff kuna vigezo vyake. Ili uende tariff 4 ni lazima uhakikishe matumizi yako hayazidi unit 75 kwa mwezi sababu hiyo ni kwa watumiaji wadogo yakizidi utatozwa Tsh 350 kwa unti badala ya Tsh 100 kwa unit
 
Hapo kidogo nachanganyikiwa kuna site yangu moja nimefunga mita tangu mwezi wa 7 na umeme tunatuumia kwa mwezi unit 55-62 lakini mbona bado kila nlinunua umeme nakatwa service charge??? Wakati sifikishi hizo unit 75 na unit zenyewe naona bado nauziwa kwenye bei ya 300+ kwa unit nifanye nn ili niingizwe kwenye kundi hilo la watumiaji chin ya unit 75??? Na sijawahuhi vuka zaid ya unit 70 tangu mita ifungwe msaada hapo jaman??

Unapo unganishiwa umeme automatic unakuwa upo tariff 1 ambayo unakatwa service charge. Kama unauhakika huvuki unit 75 kwa mwezi unaandika barua una iadress kwa Meneja wa TANESCO wa ofisi uliyokaribu nayo ya kuomba kubadilishiwa tariff, kutoka tariff 1 kwenda tariff 4.

Ila iwapomatumizi yatazid itakula kwako
 
Hapo kidogo nachanganyikiwa kuna site yangu moja nimefunga mita tangu mwezi wa 7 na umeme tunatuumia kwa mwezi unit 55-62 lakini mbona bado kila nlinunua umeme nakatwa service charge??? Wakati sifikishi hizo unit 75 na unit zenyewe naona bado nauziwa kwenye bei ya 300+ kwa unit nifanye nn ili niingizwe kwenye kundi hilo la watumiaji chin ya unit 75??? Na sijawahuhi vuka zaid ya unit 70 tangu mita ifungwe msaada hapo jaman??

Wewe andika barua kwa meneja wa tanesco ukiomba kuondolewa service charge ukieleza kuwa matumizi yako ni chini ya unit 75 kwa mwenzi na utasaidiwa
 
Naomba kuuliza wadau. Ninatumia hizi mita mpya za kama remote control inayochomeka waya ktk socket kuingiza umeme. Nataka kufahamu records za umeme ulioingia atlest the last 5.
Koleba msaada mkuu
 
Last edited by a moderator:
Koleba Mkuu saidia na hilo swali kwani hata mm linanihusu
nimefungiwa meter za LUKU (Wasion ya China) ikinisomea kwa T1 Novemba 2015
mwezi Disemba nikasoma ni Unit45
nikajaza Unit 62 nimeambia nika miezi mitatu ndio niende kulalamika
  • Mm nilikuwa T4 ni kwanini nikalalamike tena wakatu situmii frji nk
  • hicho kiremote kinasoma Error 77 na hakioneshi zimebaki au maandishi yoyote je kitakata au nikaripoti?


Unapofungiwa mita ya umeme, automatic unakuwa tariff 1, kwa taratibu za TANESCO unatakiwa kukaa miezi 6 ndio ubadilii tariff kwenda tariff 4.

Error 77 fanya yafuatayo
a) swichi kuu (main swich) na kikata umeme (circuit Breaker) vimewashwa ili kuwezesha Kati ya kipima umeme (mita) na kiwasilianishi (CIU)
b)Betri zimewashwa sawa sawa ndani ya kiwasilishi(CIU)
c)Angalia Kama betri za kiwasilianishi bado nzima na zinafanya kazi vizuri, Kama betri ni mbovu badilisha
d) Thibitisha namba ya mita kwa kuingiza namba 000 na kisha bonyeza ya kukubali.
e)Kama namba ya mita inaonekana kwenye kiwasilianishi inatofautiana na namba iliyopo kwenye kadi, fuata hatua zifuatazo
1) Bonyeza 0 kisha andika namba ya mita mara mbili kisha bonyeza accept au ok

Iwapo umekamilisha hatua nilizozitaja hapo juu kwa usahihii mita yako itafanya kazi Kama kawaida.

Tatizo likiendelea kujitokeza hata baada ya kufuata hatua hizo , tafadhari wasiliana na ofisi za TANESCO zilizokaribu na wewe
 
nafanyaje ili kuhamia T4?
Asante sana kwa swali, Kuna tariff T1 ambayo ni kwa ajiri ya wateja wa kawaida (Normal use category) hawa ni wateja wanao tumia umeme kuanzia unit 0 - na kuendelea haina mwisho. Gharama ya umeme kwa wateja hawa ni Tsh. 298 kwa Unit na wanalipia service charge 5520+ 22% ( 22% ni VAT = 18, EWURA - 1% na REA-3%)

Tariff 4 ni kwa ajiri ya low usage customers, hawa matumizi yao kwa mwezi kuanzia unit 0-75. Gharama ya umeme ni Tsh 100 kwa unit bila service charge. Ukiwa upo tariff 4 ukatumia unit zaidi ya 75 zile unit zilizozidi utalipia Tsh 350 + 22% ya VAT.
 
Tariff 4 ni kwa ajiri ya low usage customers, hawa matumizi yao kwa mwezi kuanzia unit 0-75. Gharama ya umeme ni Tsh 100 kwa unit bila service charge. Ukiwa upo tariff 4 ukatumia unit zaidi ya 75 zile unit zilizozidi utalipia Tsh 350 + 22% ya VAT.
Mkuu Koleba nakushukuru kwa ufafanuzi na hasa huu wa Error 77 umekubali kuzima na kuwaka vizuri
ila nimeshtuka hii ya kujinyima kutumia T1 nikitaka nihamishiwe T4
  • kumbe nikiirudisha friji heater na pasi ni lazima nitavuka unit 75 nazo nitatozwa zaidi kwa Tsh 52 yaani kutoka 298/ hadi 350/
  • bado Tanesco wanaumiza naona km umeme umepanda kwani matumizi yangu halali kwenye mita ya kizamani yalukuwa hayazidi 40,000/= unit km 120 kwa mwezi
swali lingine la kifizikia nikizimam Friji kutwa nzima ninapokuja kuiwasha naona inachukua muda mrefu kupata ubarudu na kugandisha nishauri nifanyeje ili isile umeme na ina thermostart 9umeme wa tz umeshakuwa shida )
 
mimi nalia na tanesco magomeni, yaani hapo prof.muhongo timua timua au wahamishe wapeleke kijijini kigoma huko baadhi ya wafanyakazi wa hapo, watu tumepeleka tatizo but hadi leo wanaleta uzushi uzushi, ikiwezekana wapige chini.
 
mimi nalia na tanesco magomeni, yaani hapo prof.muhongo timua timua au wahamishe wapeleke kijijini kigoma huko baadhi ya wafanyakazi wa hapo, watu tumepeleka tatizo but hadi leo wanaleta uzushi uzushi, ikiwezekana wapige chini.

Mpuuzi mkubwa wewe,, tuliopo Kigoma unatuzidi nini ? Acha dharau makota wewe
 
Koleba Mkuu saidia na hilo swali kwani hata mm linanihusu
nimefungiwa meter za LUKU (Wasion ya China) ikinisomea kwa T1 Novemba 2015
mwezi Disemba nikasoma ni Unit45
nikajaza Unit 62 nimeambia nika miezi mitatu ndio niende kulalamika
  • Mm nilikuwa T4 ni kwanini nikalalamike tena wakatu situmii frji nk
  • hicho kiremote kinasoma Error 77 na hakioneshi zimebaki au maandishi yoyote je kitakata au nikaripoti?

ukiona erro77 kanakuwa kamepoteza programu! hawa jamaa wameacha mita za sauzi wameenda chna dah!

sasa ili programu irudi inabid ubonyeze sifuri then ingiza mita namba halafu weka tena sifuri halafu mita namba tena!

halafu bonyeza mshale ulopinda ule! fanya hvo wakat umechomeka kwenye socket yoyote ambayo inaunganisha mpaka kwenye mita yako ya nje
 
Shurani sana wadau Koleba na wengineo tungeomba Charges kwa T2 na T3 kwa unit mana sijaona jibu hili Asante
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Koleba na wengine wenye ufahamu;
Juzi juzi hapa nilinunua units kadhaa za umeme wa Luku. Nilipotaka kuingiza namba husika kwenye mita ni namba mbili tu za mwanzo zilizokubali kuingia (inakuwa ina beep) lakini namba zilizofuatia ziligoma kabisa. Nilirudia mara nyingi bila mafanikio. Je ni sababu zipi zinaweza kusababisha namba zigome kuingia au ni mita ime jam? Na kama mita ni mbovu na inatakiwa kubadilishwa mimi mteja nitatakiwa kuilipia hiyo mita mpya itakayofungwa?
 
Back
Top Bottom