Tariffs za TANESCO zipoje?

Tariffs za TANESCO zipoje?

Asante sana kwa swali, Kuna tariff T1 ambayo ni kwa ajiri ya wateja wa kawaida (Normal use category) hawa ni wateja wanao tumia umeme kuanzia unit 0 - na kuendelea haina mwisho. Gharama ya umeme kwa wateja hawa ni Tsh. 298 kwa Unit na wanalipia service charge 5520+ 22% ( 22% ni VAT = 18, EWURA - 1% na REA-3%)

Tariff 4 ni kwa ajiri ya low usage customers, hawa matumizi yao kwa mwezi kuanzia unit 0-75. Gharama ya umeme ni Tsh 100 kwa unit bila service charge. Ukiwa upo tariff 4 ukatumia unit zaidi ya 75 zile unit zilizozidi utalipia Tsh 350 + 22% ya VAT.

Mh. Koleba naona kama upo jikoni kutokana na majibu yako mazuri.Nilikuwa sijui kitu. Nakugongea like za mafuriko 😎
 
Shurani sana wadau Koleba na wengineo tungeomba Charges kwa T2 na T3 kwa unit mana sijaona jibu hili Asante

Bei ya mahitaji ya juu msongo mdogo (T2)
Gharama ya huduma kwa mwezi Tzs 14,233.00.
Gharama ya mahitaji ya juu kwa kVA Tzs 15,004.00.
Gharama ya umeme kwa kWh Tzs 205.00.

Bei ya mahitaji ya juu ya msongo wa Kati (T3-MV)
Gharama ya huduma kwa mwezi Tzs 16,769.00
Gharama ya mahitaji ya juu kwa kVA Tzs 13,200.00
Gharama ya umeme kwa kWh Tzs 163.00

Bei ya mahitaji ya juu ya msongo mkubwa (T3-HV)
Gharama ya huduma kwa mwezi hakuna
Gharama ya nahitaji ya juu kwa kVA Tzs 16,559.00
Gharama ya umeme kwa kWh Tzs 159.00
 
Last edited by a moderator:
mimi nalia na tanesco magomeni, yaani hapo prof.muhongo timua timua au wahamishe wapeleke kijijini kigoma huko baadhi ya wafanyakazi wa hapo, watu tumepeleka tatizo but hadi leo wanaleta uzushi uzushi, ikiwezekana wapige chini.

Mkuu Nando ni pm namba yako tuongee zaidi utaweza kusaidiwa.
 
Mkuu Nando ni pm namba yako tuongee zaidi utaweza kusaidiwa.

Mkuu ww ni jembe. Tatizo langu limekwisha mkuu.Big up sana, TANESCO inahitaji vichwa kama ww mnaejua kudili na wateja. Naomba ujitambulishe kabisha Prof. Mhongo afanye kazi na ww kwani naamini unaweza kumsaidia ipasavyo. Bravoo Mkuu
 
Asante sana kwa swali, Kuna tariff T1 ambayo ni kwa ajiri ya wateja wa kawaida (Normal use category) hawa ni wateja wanao tumia umeme kuanzia unit 0 - na kuendelea haina mwisho. Gharama ya umeme kwa wateja hawa ni Tsh. 298 kwa Unit na wanalipia service charge 5520+ 22% ( 22% ni VAT = 18, EWURA - 1% na REA-3%)

Tariff 4 ni kwa ajiri ya low usage customers, hawa matumizi yao kwa mwezi kuanzia unit 0-75. Gharama ya umeme ni Tsh 100 kwa unit bila service charge. Ukiwa upo tariff 4 ukatumia unit zaidi ya 75 zile unit zilizozidi utalipia Tsh 350 + 22% ya VAT.
Ila kwa kweli miye bado napinga kuwaunganisha wateja wanaotumia chini ya unit 500 kwa mwezi kwa hali hii ya umeme tuliyo kuwa nayo, Ni kujibebesha mzigo mzito mwenyewe. Kwanini usiwe na chanzo chako mwenyewe? Gharama utakayo tumia kuweka vifaa vya umeme jua haifiki kiasi unachokamuliwa na Tanesco kwa mwaka. Ukifungua macho utaliona hili 😎
 
Mkuu Koleba na wengine wenye ufahamu;
Juzi juzi hapa nilinunua units kadhaa za umeme wa Luku. Nilipotaka kuingiza namba husika kwenye mita ni namba mbili tu za mwanzo zilizokubali kuingia (inakuwa ina beep) lakini namba zilizofuatia ziligoma kabisa. Nilirudia mara nyingi bila mafanikio. Je ni sababu zipi zinaweza kusababisha namba zigome kuingia au ni mita ime jam? Na kama mita ni mbovu na inatakiwa kubadilishwa mimi mteja nitatakiwa kuilipia hiyo mita mpya itakayofungwa?

Unatumia aina gani ya mita? Kama huifahamu aina dondosha mita namba hapa.

Kama mita ikionekana mbovu unabadilishiwa free of charge ndio maana service charge ikawepo( nafikiri utakuwa mmoja wa watu watakao ona umuhimu wa service charge)
 
Mkuu ww ni jembe. Tatizo langu limekwisha mkuu.Big up sana, TANESCO inahitaji vichwa kama ww mnaejua kudili na wateja. Naomba ujitambulishe kabisha Prof. Mhongo afanye kazi na ww kwani naamini unaweza kumsaidia ipasavyo. Bravoo Mkuu

Asante Mkuu, nashukuru sana. Nilikuwa na mpango wa kukupigia leo.

Nikisema mteja wangu aneenda kimoja
 
Asante Mkuu, nashukuru sana. Nilikuwa na mpango wa kukupigia leo.

Nikisema mteja wangu aneenda kimoja

Mkuu jitambulishe usiwe mwoga, kamata fursa; hunijui lakini umeniudumia ipasavyo; naamini ww ukipewa ofisi utamsaidia mzee (Prof. Mhongo) kwa kasi ya ajabu, JITAMBULISHE Mkuu usiogope......
 
Mkuu jitambulishe usiwe mwoga, kamata fursa; hunijui lakini umeniudumia ipasavyo; naamini ww ukipewa ofisi utamsaidia mzee (Prof. Mhongo) kwa kasi ya ajabu, JITAMBULISHE Mkuu usiogope......

Mkuu asante, nitachukua hatua kaka
 
Hahaha hakuna tatizo kaka nipo kwa ajiri ya kuhudumia wateja

Unaitwa Henry nadhani utakuwa makao makuu huduma za wateja TANESCO. cc Prof. Mhongo; mpe kijana ofisi naona atakufaa kutuhudumia sio "Miungu watu" walijaa kwenye ofisi za TANESCO na njaa kali ya virushwa vya kiajabu ajabu.... Bravoo Henry
 
Last edited by a moderator:
Unaitwa Henry nadhani utakuwa makao makuu huduma za wateja TANESCO. cc Prof. Mhongo; mpe kijana ofisi naona atakufaa kutuhudumia sio "Miungu watu" walijaa kwenye ofisi za TANESCO na njaa kali ya virushwa vya kiajabu ajabu.... Bravoo Henry

Mkuu Ntu nipo Kitengo cha Uhusiano
 
Last edited by a moderator:
Aksante sana kwa muuliza swali na mtoa jibu, hii ndiyo tunayoihitaji kwa Forum hii, maana maswali yapo clere na jibu ni sahihi na kujitosheleza kwa ufupi, natumai hata majibu kuhusu utofauti wa T1,T2 na wanaotumia 11KV & 132KV utadadavua vizuri kwa faida ya wengi na general gharama zake. Na utusaidie ni taratibu zipi zitumiwe kwa mtu kuhama Tariff, maana ukienda kuunganisha umeme kwa mara ya kwanza hope unapewa T1, Sasa unajikuta matumizi ni ya kawaida so ufanyeje? Otherwise thanks mjibu maswali@ Koleba
Unaandika barua kwa Meneja wa Tanesco ya kuomba kubadilishiwa tarrif,ukifanya ivyo utabadilishiwa
 
Unatumia aina gani ya mita? Kama huifahamu aina dondosha mita namba hapa.

Kama mita ikionekana mbovu unabadilishiwa free of charge ndio maana service charge ikawepo( nafikiri utakuwa mmoja wa watu watakao ona umuhimu wa service charge)
Ahsante sana mkuu. Ni kweli kwa maelezo yako nimeweza kujua umuhimu wa service charges. Kuhusu mita yangu maelezo yake ni: CASHPOWER, Manufactured 2006, Type 10-SA018, Landis Gyrt+. Nadhani kwa maelezo hayo utaweza kujua aina ya mita hata nisipoweka namba ya mita mkuu.
 
Ahsante sana mkuu. Ni kweli kwa maelezo yako nimeweza kujua umuhimu wa service charges. Kuhusu mita yangu maelezo yake ni: CASHPOWER, Manufactured 2006, Type 10-SA018, Landis Gyrt+. Nadhani kwa maelezo hayo utaweza kujua aina ya mita hata nisipoweka namba ya mita mkuu.

Mkuu hiyo mita imeharibika, toa taarifa ofisi ya TANESCO iliyokaribu nawe ili ibadilishwe.

Ukitoa taarifa hakikisha umepewa TB number kwa ajiri ya kufuatilia.
 
Koleba nakushukuru sana kwa majibu yako ambayo yamekuwa msaada mkubwa kwangu.
 
Back
Top Bottom