Tarehe ya uchaguzi Igunga kujulikana kesho

EasyFit

JF-Expert Member
Jul 4, 2011
1,269
1,082
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imesema tarehe rasmi ya kufanyika uchaguzi mdogo wa marudio katika Jimbo la Igunga, mkoani Tabora, itatangazwa kesho.
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imesema tarehe rasmi ya kufanyika uchaguzi mdogo wa marudio katika Jimbo la Igunga, mkoani Tabora, itatangazwa leo. Kaimu Mkurugenzi wa NEC, Dk. Sist Cariah, amesema kuwa kufikia leo watakuwa wamekwishakujua tarehe rasmi ya kufanyika uchaguzi huo jimboni humo.
 
Hivi ni akina nani wana possibility kubwa ya kushinda?? Thru the fukuto ya huko?
 
Tendwa keshakutana na waandishi jamani mlioko karibu mtujuze.
 
CCM wameshaanza usanii kule bungeni wakulaghai wana Igunga, Jana nilimsikia mbunge msanii mmoja waTabora akiigiza (Nkumba) kuwasemea/kuuliza kuwa kwenye Bajeti hii mbona hajaona mahali palipotengwa pesa kwa ajili ya daraja la Mbutu? Msanii mwenzie Mwakyembe akasimama kwa madoido yote na kumjibu kuwa "ukiangalia kitabu hiki cha bajeti ukurasa.....(siukumbuki) basi utaona hizo fedha...(hakuzitaja) ambazo zimetengwa kwa ajili ya daraja hilo na fedha hii isipotosha basi tutaangalia kwingine ili kumaliza tatizo hilo", nilichoshangaa daraja hilo analolizungumzia halipo kwenye Trunk Roads ambazo wizara ndio inayohusika kutengeneza kwani hata Magufuri alikuwa anasisitiza kuwa barabara zote zilizo chini ya halmashauri ni juu yao kuzitengeneza wakishirikiana na Tanroads ya mkoa husika, ni wazi kuwa hili ni changa la macho kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa Igunga kwani kwa mtu yeyote anayeijua vizuri barabara hiyo ya Igunga Mbutu ataona kwamba haiwezekani ukajenga daraja pekee ktk mto Mbutu then ukasema umemaliza tatizo, ili njia hiyo ipitike inahitaji kunyanyuliwa juu na chini yawepo makaravati yasiyopungua 20-30 ili maji wakati wa mvua yasiende kubomoa daraja na pia yasibomoe njia, hivyo ujenzi wa daraja pekee sio kweli na bora angesema tunajenga barabara ya Igunga Mbutu pamoja na madaraja mawili kwani hivi sasa tayari kuna mto mkubwa na mto mdogo pembeni yake hapo kidogo tungemwamini..

Uzuri nimepita huko na kukuta percent kubwa wanaikubali CDM, wanajua uongo wa CCM, Taabu wamezichoka na sasa wanachotaka ni kutoa adhabu stahiki kwa waliowafikisha hapo walipo,

Naomba mwenye kitabu cha bajeti ya Magufuri/ Mwakyembe aiweke hapa or through PM
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom