Tanzia: Ustadh Ilunga afariki dunia

Tanzia: Ustadh Ilunga afariki dunia

Status
Not open for further replies.

KIM KARDASH

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
5,139
Reaction score
1,149
Habari nilizozipata punde ni kwamba ustadh Ilunga Hassan Kapungu muasisi wa maneno mfumo kristo Tanzania amefariki dunia kwa ugonjwa wa kisukari na baadae figo zake kushindwa kufanya kazi.

Swala ya maiti itaswaliwa msikitini wa Kichangani-Magomeni na atazikwa Leo.

Innalilahi waina Ilaihi Rajiuun.

attachment.php


Sheikh alikuwa mgonjwa kitambo tu. Msiba upo Mbezi, atazikwa leo mida ya saa 10 jioni makaburi ya Mwinyimkuu, hatosafirishwa kupelekwa Mwanza!

===============
UPDATE:

Sheikh Ilunga aliyefariki Dar es Salaam, anatarajiwa kuzikwa leo katika Makaburi ya Mwinyimkuu yaliyoko Magomeni Mapipa.

Maiti yake itasaliwa katika msikiti wa Kichangani, Magomeni - Dar es Salaam katika sala ya Alasiri saa kumi jioni.

Sheikh Ilunga ambaye alikwenda nchini India kwa matibabu, aliwahi kukamatwa na Polisi na kufunguliwa mashtaka kwa tuhuma za kutoa mahubiri ya uchochezi.

Msiba wake upo Mbezi - Goigi, jijini Dar es Salaam.
 
Tupe maelezo kamili mkuu nini kimemsibu hadi mauti kumkuta.Inna-lillahi wainna ilaihi raaajiun

1.jpg
 
Nini chanzo cha kifo chake?

Poleni wafiwa.
 
Jaman tunaomba chanzo cha kifo chake ..vyanzo vingine vinadai kauwawa na watu wasiojulikana
 
Innallillahi Wainna Lilah Rajuulun. Poleni wafiwa.
 
Sheikh alikuwa mgonjwa kitambo tu. Msiba upo Mbezi, atazikwa leo mida ya saa 10 jioni makaburi ya Mwinyimkuu, hatosafirishwa kupelekwa Mwanza!
 
Ni yupi huyu, tafadhali picha kama iko maana wengine hatumfaham! Poleni sana wafiwa, Mungu awatie nguvu
 

Attachments

  • 1399260061122.jpg
    1399260061122.jpg
    18.5 KB · Views: 2,428
  • 1399260080542.jpg
    1399260080542.jpg
    15.3 KB · Views: 13,734
Apumzishwe mahala panastahili pema peponi.... amen
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom