Tanzia: Msanii mkongwe, mzee Kankaa afariki dunia

Tanzia: Msanii mkongwe, mzee Kankaa afariki dunia

suat

Member
Joined
Jun 8, 2015
Posts
14
Reaction score
5

10444571_818457911565361_1385541165369148380_n.jpg

Marehemu Juma Ally Salim ‘Mzee Kankaa' enzi za uhai wake

MSANII mkongwe wa filamu nchini, Juma Ally Salim ‘Mzee Kankaa' amefariki dunia leo alfajiri akiwa nyumbani kwake Tandale jijini Dar es Salaam baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi kwa muda mrefu.

Mwili wa Mzee Kankaa unatarajiwa kuzikwa leo saa 10 jioni katika makaburi ya Ali Maua jijini Dar es Salaam.

Marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi kwa zaidi ya miaka mitatu. Msiba upo nyumbani kwa marehemu eneo la Tandale-Chama jijini Dar.


ANGALIA PICHA NA MAELEZO ZAIDI JUU YA KIFO CHAKE HAPA

 
Si Vibaya Nikisema Pole Japo Simjui. Tafadhalini Tuwekeeni Basi Maelezo Yake Ya Kutosha Ili Tuweze Kumfahamu Vizuri Marehemu Mzee Wetu.
 
Bwana alitoa na sasa ametwaa jina lake lihimidiwe!
 
alikuwa anaigiza vizuri sana huyu MZEE Jana tu nimetoka kuangalia picha moja aliyoshirikishwa kaekti kama baba mwenye nyumba. inaitwa Veneranda, pia nilisha wahi kuona picha moja ameekti kama Fataki, sikumbuki vyema kama ni picha au Igizo kwenye TV yaani Tamthiliya. poleni sana wafiwa.
 
Kwa wasiomjua huyu mzee alifahamika zaidi katika tamthilia ya jumba la dhahabu iliyokua inarushwa tbc 1 kuanzia 2006 to 2007
 
Si Vibaya Nikisema Pole Japo Simjui. Tafadhalini Tuwekeeni Basi Maelezo Yake Ya Kutosha Ili Tuweze Kumfahamu Vizuri Marehemu Mzee Wetu.
Aliigiza kwenye ile tamthilia ya Chusi, Jumba la Dhahabu.
 
Back
Top Bottom