Maisha ya mwanadamu ni kama maua, yachanua yapendeza mwisho wake hunyauka zaburi 103:15, 1 Petro 1:24. Eee binadamu, mbona unakuwa na kiburi sana, mbona unaringa na kudharau wengine, mbona unaringia hiyo afya yako utadhani ni juhudi zako mwenyewe? Hujui afya ni zawadi kutoka kwa Mungu? Waweza kujiona mzima, ukatukana wengine, Kumbuka kwa kufanya hivyo unaangilia kazi ya MUNGU. Waweza kuijiona una nguvu, hata kuweza kukumbia marathon, kupiga pushup mia moja, kwenda gym daily, saa usiyodhani Mungu anakuambia eee mpumbavu, usiku huu wanaitaka roho yako.