Tanzia: Ben Kiko afariki dunia

Tanzia: Ben Kiko afariki dunia

Poleni sana.

Mbele yake, nyuma yetu.

Hakika kila nafsi itaonja umauti
 
R.I.P Ben kiko.Nakumbuka habari ulizokuwa ukitupatia wakati wa vita vya kagera
 
Tanzia
Aliekuwa Mtangazaji maarufu wa radio Tanzania (TBC) mzee BEN KIKO amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo 31/10/2014 kwenye hospital ya jeshi mirambo Tabora.

R.I.P Mzee wetu....nakumbuka zamani mwanaume aliekuwa 'mmbeammbea' kama warumi tulikuwa tukimuita Ben Kiko....kitambo sana!
 
Last edited by a moderator:
Tanzia
Aliekuwa Mtangazaji maarufu wa radio Tanzania (TBC) mzee BEN KIKO amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo 31/10/2014 kwenye hospital ya jeshi mirambo Tabora.

R.I.P Mzee wetu....nakumbuka zamani mwanaume aliekuwa 'mmbeammbea' kama warumi tulikuwa tukimuita Ben Kiko....kitambo sana!


JAMAn i wish ningemjua huyo mzee, R.IP
 
Last edited by a moderator:
Nasikia huyu mtangazaji alikuwa anatangaza vita vya kagera... akawa anasema naona risasi zinauwa waganda watano hapo, vifaru vinavurumisha makombora ...yaani eti alikuwa anatangaza kama mpira, R.I.P Ben Kiko
 
Huyu mzee alikuwa wa ukweli sana,hapo alipoti tukio fulani la kusikitisha kuhusu ushirikina au jambo la ajabu kwenye kipindi cha majira we utampenda.....na kuna kipindi alitangazia RFA baadae sikumsikia tena mpaka leo natapa taarifa za mauti yake R.I.P BEN KIKO!
 
RIP Ben Kiko nilianza kusikiliza habari zake pale alipokuwa Dodoma na kutoa ile habari ya yule kijana Makomeo (kipofu) ambaye alikuwa mahabusu gereza la Isanga
 
"NIKIRIPOTI KUTOKA KANDA YA KATI MKOANI DODOMA,MIMI NI BEN KIKOO WA RTD"...

Itaendelea kubaki sauti tamu zaidi kuwahi kusikiwa na masikio yangu katika Radio za hapa nchini!

Sauti ambayo haikumfanya msikilizaji achoke kuisikiliza..ni sauti yenye Mamlaka na sauti yenye Mvuto.

Sauti ambayo ikisikika tu basi tunafahamu huyu ni Ben Kiko,kinyume na sasa watangazaji wengi wanaigana kila kitu kiasi ni ngumu kumtofautisha yule wa Mawingu Radio na hata ile Radio ya Wakati...swaga zile zile
"ama niniiii"
"aje aje jombaaa"
NI UJINGA....
R.I.P BEN KIKO

Nyuma yako mbele yetu umeacha tasnia ya habari ikizidi kupoteza mvuto kila siku,waandishi makanjanja wanazidi uwingi wa wale wenye weledi.
Umeondoka KIKO ukiacha ma PRESENTER ni wengi zaidi kwasasa kuliko WANAHABARI..

Umeondoka ukiacha watu wanaojiita waandishi wa habari wa sasa hawajui hata bei ya gazeti, hawajaui hata majina ya mawaziri wao, hawajui hata idadi ya mikoa yao...yan hawajui tu!! Hata huo muziki wanaoutaka bado hawaujui.

Kuna wakati natamani ningekuwa MWANAHABARI katika kipindi chenu.

Kapumzike KIKO.!!
 
Tanzia
Aliekuwa Mtangazaji maarufu wa radio Tanzania (TBC) mzee BEN KIKO amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo 31/10/2014 kwenye hospital ya jeshi mirambo Tabora.

benKiko.jpg

R.I.P BEN


Uki angalia vizuri hiyo picha jicho la upande wa kulia utagundua Ben K alipigwa au kukoswa na stock na ndio maana hiyo tuzo kashika kwa mkono wa kushoto.....R.I.P "Mwana kipindi cha majira"
 
Uki angalia vizuri hiyo picha jicho la upande wa kulia utagundua Ben K alipigwa au kukoswa na stock na ndio maana hiyo tuzo kashika kwa mkono wa kushoto.....R.I.P "Mwana kipindi cha majira"

Na Wewe kwa umbea, stock ni nini? Sasa hapo Mkuu angeishika kwa mkono gani? Maana kama angeweka mkono Wa kulia picha ingeharibika!!
 
Back
Top Bottom