TANZIA: Aliyewahi kuwa Rais wa pili wa Zanzibar, Mzee Aboud Jumbe afariki dunia

Nadhani kunajambo alisahau yakuwa alikuwa kiongoz na aliapa kuzikubali sheria na katiba huku akiwa ameshika Quran sasa nilazima ajuwe atazikwa kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi zakuwazika viongozi. RIP mzee

Death is a private matter and it's between the deceased and his/her family. Serikali huwasiliana na familia/wafiwa kabla hawajafanya chochote na serikali hueshimu uamuzi wa familia.
 
Siasa za nchi hii zimesababisha watu muwe wanafiki sana. Sasa ndiyo nini kusababishiana malumbano yasiyo na tija humu? Marehemu ameshafariki muombeeni tu na siyo kufyatuka fyatuka.
 
Mzee Jumbe ausia asizikwe kiserikali - Islam Tanzania

====

Huu wosia wake utafanziwa kazi??

"MIMI Aboud Jumbe Mwinyi, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunibariki kuzaliwa ndani ya Uislamu na namuomba aniruzuku kufa na kufufuliwa ndani ya Uislamu".

Hayo ni sehemu ya yaliyomo katika Wasia wa Rais Mstaafu wa wa Zanzibar Alhaj Aboud Jumbe ambaye hivi sasa ametimiza umri wa miaka 80.

Akiwa na akili timamu kabisa Mzee Jumbe ameandika wasia huo wiki hii ambao nakala zake zimesambazwa kwa watu mbalimbali likiwemo gazeti hili.

Wasia huo wenye kuashiria kutahadharisha juu ya yale yanayoweza kuja kufanywa kinyume na ridhaa yake, umekuja siku chache baada ya kifo cha Rais mwingine Mstaafu wa Zanzibar Sheikh Idris Abdul Wakil.

"Ni matumaini yangu kwamba kama Mwenye Enzi Mungu alivyonirehemu kuwa Muislamu, atanijaalia nikifa kukoshwa, kuvishwa sanda, kutiwa katika jeneza, kusaliwa na kuzikwa kwa mujibu wa sunna ya Mtume Muhammad (sa.w.)", umeagiza wasia huo uliosainiwa kwa niaba

yake na Msaidizi wake Bwana Abubakar.

Agizo hilo linahusisha pia jeneza lake kutofunikwa bendera ya Taifa au ya CCM, kuwepo na utabaka katika kubeba jeneza na ufukiaji wa kaburi.

Akiwashuhudisha Mufti wa Zanzibar, Kadhi Mkuu wa Zanzibar, Naibu Kadhi Mkuu, Mwanasheria Mkuu, Sharrif Juneid, Masheikh wengine na wanawe, Alhaj Jumbe amesisitiza kuwa kufanyiwa si ombi bali ni haki yake kama binadamu, kama Muislamu na kama Mtanzania.

Amesema haki ya uhuru wa kuabudu imeelezwa katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kifungu cha 19 (1) na (2).

Kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu mtu anapokufa ni haramu kwa ndugu au jamaa zake kuomboleza kwa nyimbo, kunyoa vipara, kuvaa vitambaa au nguo nyeusi wala kulia kupita kiasi.

Aidha, imesuniwa kuwafariji (taa'zia) wafiwa kwa muda wa siku mbili tu.

"Atta'azia marrataan" ameagiza Mtume (s.a.w) akiwa maana ya kuwafariji wafiwa ni mara (siku) mbili.

Katika wasia wake Alhaj Jumbe amesema maana ya kuumbwa mauti na uhai sababu na lengo lake ni kuwafanyia wanaadamu mtihani kupimwa miongoni mwao mwenye vitendo vizuri.

"Nikiwa hai, dhamana ya vitendo vyangu inaniangukia mimi mwenyewe, nikifa dhamana ikiwa vitendo vyema au vibaya nitakavyofanyiwa itawaangukia waandalizi, watendaji na wenye kushiriki katika vitendo hivyo", amesisitiza mzee huyo aliyekuwa pia Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akimshudisha Mwenyezi Mungu katika wasia huo amekataa maziko yake kufanywa kinyume na taratibu za Kiislamu.

"Sitaki bendi, sitaki mizinga, sitaki maombolezo wala lolote lingine lenye hata chembe ya kufuru", ameandika kwa mkazo mzee huyo.

Aidha, amewaapiza kwa kumshuhudia Mwenyezi Mungu wale watakaojaribu kufanya kinyume na anavyoagiza.

"Sitaki hivyo nikiwa hai, nitakapoondoka katika dunia Mwenye Enzi Mungu anatosheka kuwa shahidi wangu, duniani na akhera", mzee Jumbe amemaliza wasia wake alioutanguliza aya ya Qur'an isemayo "Enyi wenye kuamini, mcheni Mwenyezi Mungu vile ipasavyo waja kumcha, wala msife ila Ilhali ni miongoni mwa Waislamu. (3:101)
R. I. P
 
Apart from udini kuna upuuzi mwingi tu aliufanya...! Just imagine alivyoharibu historia ya Tanganyika na hatimaye Tanzania as if huo uhuru aliuleta single handedly!!!

sio yeye tu jamani, au hamjawahi kufika huko bara nyieeeeeeeee? bora mwenzenu amegundua kuwa Dar sio bara ipo ndani ya maili 10 ameamua kusogeza nchi kwao
 
Na aliefanya mpaka mzee Jumbe akateseka namna ile kwa kifungo kile cha dhuluma,huyo mtu atalipa na atapata adhabu kali kwa MUNGU.

adhabu alianza kuionja hapahapa duniani kabla hajafika kwa hakimu wa mahakimu, alinyofolewa roho na 'saratani ya damu' akiwa 'amedhofu kwa ghafla sana' si maneno yangu, nikatika hotuba ya aliyekuwa mkuu wa nchi kipindi hicho
 
Kwani Magufuli yeye ni MUNGU?

hahahahahaa. eti Magufuli anaweza kumpoteza mtu, Tanzania kwa unafiki ni hatari, hakuna kitakachobaki juu mgongo wa ardhi hata kimoja, vile uonavyo mtu anashikwa na haja ndogo akasahau kila kitu kinachomzunguka hadi haja ndogo itoke, basi ujue hana anachoweza bila kwa idhini yake Muumba, likikufika ni Qadar yake na mtihani kwako
 
Mkuu dangadunguri..
Sijakuelewa apo naomba unipe shule kidogo

escotter
kuna uzi unazungumzia kifo cha mzee mtukufu, inasemekana kuwa 'saratani ya damu' ndiyo iliyomdhoofisha 'ghafla' huko UK ilhali hapa aliondoka buheri wa afya. inasemekana kuwa jinamizi la ubinafsishaji alioutaka 'mtoto mwema' halikumpendeza mzee wetu, sasa itakuwaje 'saratani ya damu' ilimuondoa duniani, akamtangulia jumbe miaka 15 mbele
 
Muongo xana wewe! Udini ulitoka wapi wakati Mwl.Nyerere amefariki akiwa mpingaji mkubwa wa udini na ukabila nchi hii! Mbona huzungumzii ya marais wengine waislamu waliofuatia,ambao ndio waliohamasisha udini hata mashuleni school uniform zilibadilishwa ili ku reflect wanafunzi na dini zao! Ama hayo huyaoni.Hapa tuna discuss political issues we unaanza udini?

taratibu ngomeu, hapa hapahitaji hasira saaana manake hutaelewa kitu, vuta subra utajibiwa kwa hoja madhubuti juu ya UDINI wa Nyerere, tuliza munkari hutaweza kujifunza
 
Wanafiki wanaomboleza ....ooh Chama kitamuenzi ....Wakati huyu alikuwa anatumikia Kifungo cha maisha ...kizuizini...,pale MJIMWEMA ilikuwa jela unajua rais akifungwa...anazuiliwa KWENYE Jumba ....
MFUNGWA KAFARIKI
Familia yake iwafukuze hao wapuuzi!Jumbe kafa akiwa kama mhaini ingawa ndiye Rais aliyeifanyia mema sana ZNZ kuliko Rais yyt yule

Hata hii Baraza la Wawakilishi ni yy alilianzisha mwaka 1980!Kabla ya hapo Jeshi ZNZ chini ya Kanal Bakar na baadae Brigedier Himid Mansour liikuwa linakugongea mlango na wakikuchukua huonekani tena!

Vigogo kama Dr Hanga;Dr Sherif,Mdungi Ussi,Ubwa Halj na wengineo hadi leo hawajulikani walipo presumed died!Prof Abdulrahman Babu yy alikuwa na bahati ya kutorokea Uingereza

Jumbe ndiye alianzisha utawala wa kisheria ZNZ
 
Gwama, issue ya huyu Mzee ni ndogo tuu, baada ya kuona Zanzibar inabanwa, akautumia Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Mgoa Wolfgang Dourado kuandaa hati za kisheria za serikali tatu, ziende BMW, Zanzibar iwe na mamlaka yake kamili. Wakamshirikisha Maalim Seif wakati huo kijana kada maarufu wa CCM, toka UV-CCM. Seif akapanda boat usiku usiku na kuzikabidhi hizo documents kwa Mwalimu, Mwalimu akaitisha kikao cha NEC cha dharura Dodoma, kwenye kikao Jumbe akaenda kama rais wa Zanzibar, akaonyeshwa document, kimya, akavuliwa nyadhifa zote na kurejea kama mfungwa, akutupwa kizuizini cha nyumbani kwake mpaka umauti ulipomkuta. Dourado yeye aliozea jela kwa muda mrefu, kisha akaachiliwa na kujifia!.

Tangu pale alikuwa kifungoni cha nyumbani kwake mpaka Mungu alipomuita. Hata hivyo, wakati wa kifungo hicho, serikali iliendelea kumhudumia kwa kumpatia stahiki zake zote kama rais mstaafu wa Zanzibar!.

Huyu Maalim Seif wa leo ambaye ni mpinzani Mkuu wa CCM Zanzibar, alikuwa ni CCM, and was once a snitch! . Once a snitch, always a snitch!, naye siku zake zinahesabika, what goes around, comes around! .

RIP Alhaj Aboud Jumbe, wengine soon watafuatia na wote mtakutana huko mbinguni na mtayamaliza kiutu uzima hukohuko mliko! .

Pasco
Huyu Maalim Sief huyu,
Mwenye kelele tele, anayeandamanisha watu kwa kudai mamlaka kamili za Zanzibar, hali yeye ndo "alimtia ndani" Mzee Jumbe kwa jambo hilo hilo?
Ama kweli dunia hadaa.......na kuishi kwingi ni kuona mengi.
 
Back
Top Bottom