Mgonjwa jumlisha Mgonjwa jibu ni MahututiKama wana haraka ya kuungana waache waungane, mwisho wa siku bomu likilupuka ni wao watakao umia. Kama wanaona maswala ya kuungana ni ya mzaha mzaha na Tanzania ina wachelewwsha basi haiko waendelee na mikakati yao.
Ukweli unabaki kwamba Tanzania ina uzoefu ya mambo haya kutokana na muungano wa Tanganyika na Zanzibar ndio maana tuna sita. Pili nchi zote za Afrika Mashariki zina matatizo ya ndani ambayo mkiungana nchi zote shiriki mtarithi. Kenya kuna ukabila, Uganda kuna ukabila na Museveni yeye anataka kuwa raisi wa nchi itakayo kuwa East Africa, Rwanda nao ukabila nk. Kweli shirikisho lita fanikiwa kwa hali hiyo?
kitendo cha kufukuza raia wao kama wanyama kimewauzi sana,moyoni kimewauma sana,na uwezi kushirikiana na mtu aliofukuza ndugu zako
tofauti ya Tanzania na nchi nyingine wanachama ilianzia kwenye suala la ardhi miaka mitatu iliyopita. nchi 4 zilipendekeza kuwa wananchi wa EAC wawe huru kununua na kumiliki ardhi ktk nchi yoyote ile mwanachama. Tanzania ndiyo nchi kubwa kuliko zote na ndiyo iliyo na angalau ardhi ambayo haijawahi kanyagwa na binadamu. Tanzania iliogopa pendekezo hili kwa kuamini kuwa raia wa nchi nyingine zitavamia ardhi na kuinunua kwa pupa! jambo hili liliwakera wanachama wengine na ndiyo chanzo cha kuiona Tanzania kama kikwazo kwa umoja wa EAC. je kuhusu hili la Tanzania iko sahihi au la?
Wamejiunga kwenye nini hasa? Hapo kila mmoja ana ajenda yake: Kenya ni kimaslahi zaidi i.e biashara specifically bandari ya M'SA : Uganda- M7 alisha sema siku nyingi kwamba anataka kuwa Rais wa kwanza wa Est Africa na ndie alikuwa anampigia debe PK (Rwanda) ajiunge na Shirikisho, lakini hao wawili i.e PK na M7 wana ajenda zao za siri zaidi kuhusu East Africa: Rwanda, inacho tafuta zaidi pale ni kutaka ahungwe mkono na nchi hizi kama usalama wa nchi yake utakuwa mashakani, he (PK) knows suala la Wahutu kutaka kuchukuwa tena madaraka nchini mwake (Rwanda) alijafa, wapinzani wake watajipanga kurudi Rwanda kwa style ile ile aliyo itumia PK kuingia madarakani: Burundi - kisakolojia sioni Burundi kama inachangamkia sana suala hili la kutenga nchi mwanachama, wanaudhulia mikutano kama geresha tu hawana interest sana na jambo hili, Mh.Nkuruzinza inajua yaliyo wapata Marais wenzake Wahutu walio mtangulia na anajua wahusika wakuu walikuwa wakina nani - sio mjinga. Kwa kifupi: Kenya - biashara: Uganda - Urais wa East Africa na kuendeleza ndoto za HIMA Empire wakishirikiana na PK. : Rwanda - ina nia ya kuhungwa mkono kijeshi just in case, wako paranoid wanafikili WATAVAMIWA na wapinzani wa regime ya Kagame, PK anajua fika wapinzani wake wengi wao ni Wahutu na moderate TUTSIS wapenda amani, anajua vile vile kwamba historia inaonyesha hakuna nchi yoyote duniani ambayo Minority walifanikiwa kuwatawala majority 4 ever - Demise of Omnipotent Apartheid South Africa should serve as awake up call 4 PK and his regime.nakumbuka wananchi walikataa na walisema ni mapema mno lakin mchakato wa kuwaweka ukaenda fasta fasta wakajiunga
kitendo cha kufukuza raia wao kama wanyama kimewauzi sana,moyoni kimewauma sana,na uwezi kushirikiana na mtu aliofukuza ndugu zako
Mimi nafikiri MMEPANIC kusikia wenzetu wanatumwaga!Ukweli ni kwamba Tanzania ndio imekuwa kikwazo kikubwa kwa kuharakisha soko la pamoja la shirikisho la Africa mashariki.Kulikuwa na sababu kadhaa zilizosababisha kutokuharakisha huko ikiwemo elimu kuwa watanzania wengi hawana elimu hivyo watakuwa manamba wa wageni.Pia kulikuwa na hoja ya ardhi kuwa wenzetu wanahitaji ardhi yetu.Na pia kulikuwa na hoja ya ukabila kuwa wenzetu ni wakabila sana kuliko sisi hivyo kuungana nao ni kujifunza Yao.
Kiukweli watanzania tuna USHAMBA na UBINAFSI Fulani hvi,ambao unasababisha watu wadumae kifikra.Sasa kama watu hamsomi na kuzingatia elimu wakenya wakija Tanzania si ndo watawa-mobilize msome?Au kama mataifa mengine Yana ukabila si ndio tutaupunguza huo ukabila kwa kuchangamana nao(refer hotuba za Nyerere),au kama ni issue ya ardhi si ndio tutakuwa makini na kuchangamkia fursa za kumiliki ardhi na kuacha kushinda vijiweni kunywa ghahawa na kucheza draft huku tukiacha ardhi kubwa bila matumizi?
Kwanza hata yale yote tuliokuwa tunajivunia yote tulishayaacha,sasa hivi watanzania ni WADINI,WAKABILA na WABAGUZI kupita maelezo.Ni mara ngapi humu ndani tunapost thread za kibaguzi za KIDINI na KIKABILA?
Mie naona ni wakati wa kuwa waungwana na kuwaomba radhi wenzetu ili tujenge shirikisho letu vyema!Haiwezekani tunahubiri shirikisho wakati huo huo tunawafukuza nchini wenzetu na kuwaita wakimbizi na kuwaacha raia wa Oman,Syria na Egypt wamejazana pale kariakoo wakiwa n pasipoti feki!
TUACHE UNAFIKI!
kwa nini tulaumiane na kuilaumu Ccm hata katika swala ambalo hawapaswi kulaumiwa? ni tangu lini Tanzania ama Ccm walikataa kushiriki katika jumuiya ambayo Tanzania ndo ilikuwa kinara wa kuanzishwa kwake hiyo jumuiya? hapa kunayo vita ya kiuchumi kati ya Tanzania na kenya hilo ni moja na la pili kunayo vita Kati ya Rwanda na Tanzania kwa habari ya Ardhi Rwanda inaunyemelea sana Ardhi ya Tanzania ndiyo maana walikuwa wanataka maswala ya umiliki wa Ardhi kwa raia wanaotoka Ktk nchi jumuiya yawe ni yawekwe free raia wa nchi mwanachama amiliki ardhi kwa nchi yeyote bila kuweka mpaka serikali ya Tanzania ni makini ilikataa kuuweka huo mkataba saini kwa maana ya kwamba mtanzania hatafaidika na mkataba huo bali nchi kama Rwanda ambayo ardhi yake ni ndogo sana ndo watakaofaidika.jambo hili lilizusha hasira sana kwa serikali ya Rwanda na hata Uganda hivyo wakawa wanalalamika ya kuwa Tanzania itengwe nao hao wamepiga kampeni kwa misingi hiyo.kw upande wa kenya ilionekana kuwa Tanzania itampa upinzani kwenye maswala ya bandari na usafirishaji kwani nchi za Rwanda,Burundi na Uganda hazina bandari na zitahitaji kutumia mojawapo Kati ya bandari ya Mombasa ama Dar es salaam na kwa uwezekano mkubwa Dar ndo bandari ambayo ingekuwa na nafasi nzuri zaidi ukizingati ya kuwa bandari hiyo ndiyo iliyopo karibu zaidi na nchi hizi kwa hapo ndipo kenya nayo ikafanya fitna ili nchi ya Tanzania iwekwe kando kwenye jumuiya na hivyo iwe rahisi kwa kenya kufanya biashara na nchi hizo kwa maana ya kuwa ni jumuiya . hizo ndo sababu za hayo yaliyotokea.sasa kwa hapa sioni sababu ya kuilaumu serikali yetu katika hili maana wangeingia kichwakichwa wakati Ardhi ingepokonywa tungewalaumu ya kuwa serikali imeshindwa kuwalinda watanzania kwa kutokujali maslahi yaoKuna principle ya UMOJA NI NGUVU, UTENGANO NI UDHAIFU. Mwalimu Nyerere alikuwa tayari kuchelewesha Uhuru wa Tanganyika ili Afrika Mashariki tupate Uhuru pamoja na kuwa nchi moja.
Kuogopa kuungana kwa sababu una ardhi ni mediocrity; kwani ukiwa na kitu ukaungana kinaacha kuwa chako? Kama kuna mtu au kijiji chenye ardhi ekari elfu moja sasa hivi, tukiungana hizo ekari elfu zinaacha kuwa mali ya hicho kijiji? Au kijiji hicho kitalazimishwa kuiuza hiyo ardhi? Kuna mediocrity hapo.
Serikali ya CCM imeshindwa vibaya kudumisha hali nzuri kati yetu na majirani zetu wa Malawi, Rwanda na hata Kenya na Uganda. Ila kuna tumaini: wakiingia wapinzani serikalini 2015, watazawasisha hii hali. Wataaminiwa na majirani zetu.
Ile kanuni ya mwasisi wa CCM kwamba "Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja" imekufa naye?