Si hilo tu.
Njaa nchi nzima, chakula hakuna. Mafuta ya magari foleni. Jumapili hakuna kunedesha gari, Watanzania wanavaa matairi ndiyo viatu hata kadambili hakuna. Foleni ya chakula, foleni ya nguo, foleni ya nyama na ng'ombe wote tulionao. Fikiri.
Halafu leo mtu ankuja kuponda utawala wa Kikwete? unakwenda dukani unachaguwa unataka kula mchele wa wapi, sembe ya wapi, kiatu kipi uvae. Una fedha za kigeni benki za kukutosha kununuwa chochote ukitakacho kwa miezi minne ijayo bila kuingiza hata senti tano. Leo unakopesheka kuliko wakati wowote ule.
Leo miaka 9 ya Kikwete unaweza kwenda kufanyiwa upasuaji wa moyo Muhimbili bila kupasuliwa kifua chote.
Watu hawayaoni yote hayo.
Bado watu wanakuja na habari za kufikirika.
Siwashangai, hata kitabu chao hao hao wanashindwa kukifata.
Utawaona ni wepi. Tazama.