Tanzania yanunua tena 35% ya TTCL

Tanzania yanunua tena 35% ya TTCL

bukoba boy

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2015
Posts
5,374
Reaction score
3,972
Serikali ya Tanzania imeamua kuzirudisha hisa 35% za TTCL kutoka kampuni ya simu za mkononi kutoka India Bharti kwa gharama ya $7.07m.
Serikali imesema inataka umiliki wa 100% kwenye shirika hilo la umma iki kuliokoa kutoka uhaba wa fedha unaolikabili.

Nini madhara ya uamuzi huu wa serikali kwenye moja ya sekta ambayo inaongoza kwa ukuaji?

====================================
DAR ES SALAAM: Tanzania's government has agreed a deal to buy back a 35 per cent stake in a state-run telecoms company from the local subsidiary of India's top mobile carrier Bharti Airtel for 14.6 billion shillings ($7.07 million), a senior official said.

The east African nation says it wants to regain 100 per cent ownership of the Tanzania Telecommunications Corp (TTCL) to recapitalise the cash-strapped firm, which provides mobile voice, data and fixed-line services.

Source: Indiatime
 
Tunapongeza serikali kwa kurejesha umiliki wa TTCL mikononi mwa Watanzania, lakini tunailaumu kwani ni tamaa ya utajiri, waliokua nayo baadhi ya viongozi wa serikali kipindi kile ndio ilisababisha waibinafsishe TTCL, hakukuwa na haja hiyo.

Kama alivyowahi kusema hayati J K Nyerere, hana shida sera ya ubinafsishaji bali alitoa angalizo serikali iangalie yale mashirika yaliyoshindwa kujiendesha ndio yafanyiwe hiyo kitu mbaya. na yale yanayojiendesha na kodi yanalipa yaachwe.

Na hata ukiangalia huo ubinafsishsji wa TTCL ni wizi wa mchana kweupe tu ulifanyika, hao watu hawakuja na sent tano walikuja na brifcase ambazo walipewa viongozi wa umma baadhi yao , huku serikali ikiambulia patupu, ukitaka kuliona hilo jiulize inakuwaje aliye na hisa chache amiliki kila kitu?

Kama haitoshi ikaanzishwa celtel kwa mtaji toka TTCL wakitumia license ya TTCL, ikisikika ni kampuni tanzu .mara imekuwa ndio kila kitu na muamuzi wa maisha ta TTCL, haikutosha. Muda si muda ikamegwa na kuwa kampuni huru.

Nchi hii wacha wang'ang'anie madaraka maana zimwi likujualo halikuli likakwisha. Ingelikuwa China tumeshawasahau baadhi yao. Nampongeza sana rais Jakaya Kikwete kurekebisha kasoro hii iliyofanywa na waliomtangulia kwa faida ya Watanzania wote.
 
Ubadhirifu huu sijui ni maandalizi ya uchaguzi ? waziri anaeshughulika na simu sio yule yule anaegombea urais ambae juzi juzi aliisamehe vodacom mabilioni ya shilingi kama ruzuku. Hajaingia Ikulu, ndio hivi akiingiaje ?
 
Nasikiaga ni Baba yake Nape ndiyo aliliuza shirika la TTCL?
 
Wanamlipa hela za umma huyo mwekezaji wao ambaye hajatia hata shilingi?kweli serikali hii tatizo
 
Jambo la kwanza tunatakiwa kujua ziliuzwa bei gani ili tuone kiasi ambacho serikali ilipoteza.
Pili wale wote walioingiza hasara hiyo wanatakiwa waondolewe serikalini na ikiwezekana wafunguliwe mashtaka au waadhibiwe kwa kuwanyima nafasi za kugombea uongozi.
 
Na wale wafanyakazi waliopunguzwa kazini wakati shirika linabinafsishwa mpaka sasa wanazungushwa,kuna wakandarasi,wanasheria na wengine wengi tu...wameendesha kesi ya madai tangu 1994 walipwe halali yao.wamechoka
 
Si lilikuwa la Serikali 100%?

Litakufa tena likirudi 100% kwa serikali. No doubt.
 
Suala hapa ni tuliliuza bei gani na tunalipa bei gani kulinunua.
Tuliwapa bure tunanunua kwa hela.
 
bukoba boy

Hilo dili hela za uchaguzi. Marekani njooni huku mfanye yale ya FIFA hapa Bongo.
 
Last edited by a moderator:
Hawa wahindi walilipa kiasi gani ili kununua hizo 35% of the shares from the government?
 
Na hapo umejionesha jinsi ulivyo finyu kwa kutokuweza kujibu maswali simpo kabisa.

We ndo uko finyu, kwani umejionyesha jinsi serikali yako ya CCM unayoishabikia ilivyo mbovu kusimamia mashirika ya umma.
 
We ndo uko finyu, kwani umejionyesha jinsi serikali yako ya CCM unayoishabikia ilivyo mbovu kusimamia mashirika ya umma.

Waliokuwa wanasimamia mashirika ya umma ni wale waliopewa upendeleao wa kusomeshwa na wakayaua yote. Na unawajuwa ni akina nani.
 
Waliokuwa wanasimamia mashirika ya umma ni wale waliopewa upendeleao wa kusomeshwa na wakayaua yote. Na unawajuwa ni akina nani.

Tunawajua kina Joseph Makamba, Joseph Kighoma, Mbaruk Mwandoro, Juma Mwapachu na kaka yake etc
 
Back
Top Bottom