Tanzania ya Sasa: Jamii, siasa na wanasiasa

Tanzania ya Sasa: Jamii, siasa na wanasiasa

KENZY

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2015
Posts
35,744
Reaction score
86,370
Sote twafahamu msingi wa taifa hili toka hapo awali nisingependa sana kugusia mambo ya kale japo vya kale ni dhahabu lakini kwa muktadha wa mada hii nitaangazia mambo ya sasa..

Si jambo geni ama la ajabu kuona migomo na maandamano katika taifa lolote lile lakini sikuzote jamii ndio hushawishi waongozwe vipi.! Ndio na wala si ajabu maana kuongoza watu hutegemea wana elimu kiasi gani, utendaji, umoja na ustaarabu wao upo katika stage gani.

Kwa uchache tu na ufupi jamii yetu ipo katika stage ya uchangamano!, yani kuna kizazi kinachohitaji mabadiliko na kile ambacho hakihitaji!.

Hivi vizazi vyote vipo sahihi aidha kutokana na uzoefu wa maisha,matarajio na vilevile kuridhika ama kutoridhika!.

Ila moja ya kitu ambacho saikolojia ya binadamu huwa inaogopa ni mabadiliko. Kuubadilisha mfumo uliopo huwa inawapa tabu sana hususani watu wenye hulka ya hofu na uoga!.

Jamii hii ndio ileile iliyoona na kuishi mabadiliko toka enzi za awamu ya kwanza mpaka hivi sasa, na jamii nyingine ni imeona nakuishi awamu kadhaa hapo nyuma.

Mitazamo ya hizi jamii lazima itakinzana katika namna moja ama nyingine kutokana na vile mahitaji ya wakati huu yanahitaji nini na nani hayahitaji!.

Wapo wanaomini kilimo ni bora na wapo wanaomini usanii, ama uanamitindo ama kuwa mwana Mitandao ni bora zaidi!.

Hawa wote wapo sahihi maana wapo katika wakati sahihi na vyote vinaweza kupatikana kwa wakati sahihi!.

Shida ya haya yanakuja hapa: SIASA na Wanasiasa ndio wanaweza kuyafanya haya yakawa matunda matamu ama machungu!.

Bila kuremba muandiko, taifa hili limekosa wanasiasa wenye maono na wanaoogopa mabadiliko!, wanaogopa aidha kwa tamaa ama ileile hulka ya kibinadamu ya uoga wa mabadiliko lakini kwenye hili hata mtoto anaweza kung'amua uoga wao ni juu ya nini!.

Kwani nani yupo tayari kuliachia pande la keki liende kwa mwingine..?

Hii imekuwa ni ndoto kwa wanaharakati kuona uongozi ukigawa keki ya taifa ipasavyo lakini si malaika ama shetani ameweza kuruhusu hilo!.

Kiongozi mwenye maono anafahamika na hupimwa kwa matendo yake!, ila huu mzani uliolegalega bado hausomi vyema ila nimegundua tatizo lilipo na wapi pakutatua!.

Jamii imekosa sauti moja hii ni kutokana na mkanganyiko ya wanaofaidi na wasiofaidi, wanaoiba na wasioiba n.k

Hoja dhaifu za kukimbilia zinaonyesha ufupi ama uhafifu wa akili za watu fulani fulani!..

Hoja haiwezi kuwa Dini ama muungano au kabila maana wanufaika wa maendeleo nchi huwa ni ya wote pasipo kuangalia tofauti yoyote ile, ila kwasababu wanajua mkikimbiziwa huko mtaogopa na kuifyata mikia yenu kama mbwa koko basi hiyo ndio fimbo yakuichalaza!.

Nanyi nani aliwaambia kwa vurugu nakuharibu vitu vya watu wakusadikika ndio mtapata haki yenu..?

Hii ni akili finyu ila ni alama ya utambulisho inayoitwa "kuchoka!".

Japo hii vita haikupaswa kuwa hivi hapo awali ila sauti tu ya umoja inaweza kutosha na kubadili historia! Ni zwazwa pekee anaeweza kuiamini katiba ya nchi yakusadikika!, lakini vipi ndugu zangu ndio huwa inaombwa hivyo...?

Mengi mtasikia, mtaona na kuyaishi lakini mchezo unaoitwa siasa unatakiwa uwe na akili ya moja kwenda na mbili!, hesabu hupigwa na kuchezewa; hivi ni vipaji vya watu japo kwa sasa ni vipaji vilivyochacha!.

Hivyo basi, badiliko la kweli litakuja pale mtakapokuwa na sauti moja, vilevile kubadili mifumo katika njia sahihi lakini kama mtakuwa na sauti kila mtu anaongea lakwakwe hapo hakuna kusikilizana!, ni kutoana meno na manundu tu!.

Hata hivyo nanyi upande wapili mmeshakuwa wazee wapeni vijana nafasi wasimamie mambo!, ushamba wakukatiana umeme, internet na kuchukuana bila ridhaa hizo ni karne za zamani. Watu hivi sasa hawahitaji tu barabara bali barabara bora, sio tu umeme bali wa uhakika maisha yasasa umeme ni uchumi, sio tu internet bali ya uhakika.

Msiwe waoga wa mabadiliko.
 
Umenena vyema. Lakini namna ya kutoka hapa tulipo lazima utaifa ndio utumike vinginevyo tutarudi kule kule Kwa muamba ngoma.

Au tusubiri wazee wastaafu wafe kwanza maana waliyoyafanya ndio huwafanya waogope mabadiliko.
 
Umenena vyema. Lakini namna ya kutoka hapa tulipo lazima utaifa ndio utumike vinginevyo tutarudi kule kule Kwa muamba ngoma.

Au tusubiri wazee wastaafu wafe kwanza maana waliyoyafanya ndio huwafanya waogope mabadiliko.
ni aibu kuogopa mabadiliko Tena mabadiliko Chanya.. Muda ufike kama in kamba waachie tu mbona wao wanaweka watoto wao
 
Umenena vyema. Lakini namna ya kutoka hapa tulipo lazima utaifa ndio utumike vinginevyo tutarudi kule kule Kwa muamba ngoma.

Au tusubiri wazee wastaafu wafe kwanza maana waliyoyafanya ndio huwafanya waogope mabadiliko.
Kama wanaingiza watoto wao sahau mabadiliko kwa ridhaa yao, maana watoto wao watafanya kama wazazi wao ili kulinda kosa la kimfumo. Ni machafuko tu yatatuoa hapa.
 
ni aibu kuogopa mabadiliko Tena mabadiliko Chanya.. Muda ufike kama in kamba waachie tu mbona wao wanaweka watoto wao
Zungumza tu mkuu maneno yote unayotaka, lakini bila machafuko hatuwezi kupata mabadiliko ya kweli. Lakini hizo unazoita njia za amani zimeshatumika sana na hazijaa matunda. Kibaya zaidi imefikia mahali uchaguzi ni kutimiza wajibu tu, lakini washindi wanapatikana kwa njia tofaufi kabisa. Ni bora tufe nusu ya watanzania, nadhani watakaobaki wataelewa maana ya kuheshimu matakwa ya wananchi.
 
Umenena vyema. Lakini namna ya kutoka hapa tulipo lazima utaifa ndio utumike vinginevyo tutarudi kule kule Kwa muamba ngoma.

Au tusubiri wazee wastaafu wafe kwanza maana waliyoyafanya ndio huwafanya waogope mabadiliko.
Huoni kwamba wanapambana kurithisha 'ya kwao' kwa watoto wao?
 
Zungumza tu mkuu maneno yote unayotaka, lakini bila machafuko hatuwezi kupata mabadiliko ya kweli. Lakini hizo unazoita njia za amani zimeshatumika sana na hazijaa matunda. Kibaya zaidi imefikia mahali uchaguzi ni kutimiza wajibu tu, lakini washindi wanapatikana kwa njia tofaufi kabisa. Ni bora tufe nusu ya watanzania, nadhani watakaobaki wataelewa maana ya kuheshimu matakwa ya wananchi.
Nakinzana na wewe kwani maandamano yenye tija sio lazima mfanye vurugu na watu mtoke damu ama mpoteze maisha!, mkiweza kuwa na sauti moja na kubalio moja hakuna anaeweza kukaa mbele yenu ipo migomo isiyoleta shida kwa wasiohusika na inaweza kuleta tetemeko kwa wahusika!, kama mkiigomea serikali mambo yake unafikiria nani ataweza kusimama katikati..?
hata wazee wetu waliwafanyia wakoroni migomo baridi na ilifanya kazi shida ni umoja tu!, yani bado tuna makundi wapo wanaoridhika na kidogo wanachopata japokuwa wanaumia!.
hakuna anaeweza kushindana na nguvu ya umma kama wakiamua kusimama kwa umoja.
 
Sote twafahamu msingi wa taifa hili toka hapo awali nisingependa sana kugusia mambo ya kale japo vya kale ni dhahabu lakini kwa muktadha wa mada hii nitaangazia mambo ya sasa..

Si jambo geni ama la ajabu kuona migomo na maandamano katika taifa lolote lile lakini sikuzote jamii ndio hushawishi waongozwe vipi.! Ndio na wala si ajabu maana kuongoza watu hutegemea wana elimu kiasi gani, utendaji, umoja na ustaarabu wao upo katika stage gani.

Kwa uchache tu na ufupi jamii yetu ipo katika stage ya uchangamano!, yani kuna kizazi kinachohitaji mabadiliko na kile ambacho hakihitaji!.

Hivi vizazi vyote vipo sahihi aidha kutokana na uzoefu wa maisha,matarajio na vilevile kuridhika ama kutoridhika!.

Ila moja ya kitu ambacho saikolojia ya binadamu huwa inaogopa ni mabadiliko. Kuubadilisha mfumo uliopo huwa inawapa tabu sana hususani watu wenye hulka ya hofu na uoga!.

Jamii hii ndio ileile iliyoona na kuishi mabadiliko toka enzi za awamu ya kwanza mpaka hivi sasa, na jamii nyingine ni imeona nakuishi awamu kadhaa hapo nyuma.

Mitazamo ya hizi jamii lazima itakinzana katika namna moja ama nyingine kutokana na vile mahitaji ya wakati huu yanahitaji nini na nani hayahitaji!.

Wapo wanaomini kilimo ni bora na wapo wanaomini usanii, ama uanamitindo ama kuwa mwana Mitandao ni bora zaidi!.

Hawa wote wapo sahihi maana wapo katika wakati sahihi na vyote vinaweza kupatikana kwa wakati sahihi!.

Shida ya haya yanakuja hapa: SIASA na Wanasiasa ndio wanaweza kuyafanya haya yakawa matunda matamu ama machungu!.

Bila kuremba muandiko, taifa hili limekosa wanasiasa wenye maono na wanaoogopa mabadiliko!, wanaogopa aidha kwa tamaa ama ileile hulka ya kibinadamu ya uoga wa mabadiliko lakini kwenye hili hata mtoto anaweza kung'amua uoga wao ni juu ya nini!.

Kwani nani yupo tayari kuliachia pande la keki liende kwa mwingine..?

Hii imekuwa ni ndoto kwa wanaharakati kuona uongozi ukigawa keki ya taifa ipasavyo lakini si malaika ama shetani ameweza kuruhusu hilo!.

Kiongozi mwenye maono anafahamika na hupimwa kwa matendo yake!, ila huu mzani uliolegalega bado hausomi vyema ila nimegundua tatizo lilipo na wapi pakutatua!.

Jamii imekosa sauti moja hii ni kutokana na mkanganyiko ya wanaofaidi na wasiofaidi, wanaoiba na wasioiba n.k

Hoja dhaifu za kukimbilia zinaonyesha ufupi ama uhafifu wa akili za watu fulani fulani!..

Hoja haiwezi kuwa Dini ama muungano au kabila maana wanufaika wa maendeleo nchi huwa ni ya wote pasipo kuangalia tofauti yoyote ile, ila kwasababu wanajua mkikimbiziwa huko mtaogopa na kuifyata mikia yenu kama mbwa koko basi hiyo ndio fimbo yakuichalaza!.

Nanyi nani aliwaambia kwa vurugu nakuharibu vitu vya watu wakusadikika ndio mtapata haki yenu..?

Hii ni akili finyu ila ni alama ya utambulisho inayoitwa "kuchoka!".

Japo hii vita haikupaswa kuwa hivi hapo awali ila sauti tu ya umoja inaweza kutosha na kubadili historia! Ni zwazwa pekee anaeweza kuiamini katiba ya nchi yakusadikika!, lakini vipi ndugu zangu ndio huwa inaombwa hivyo...?

Mengi mtasikia, mtaona na kuyaishi lakini mchezo unaoitwa siasa unatakiwa uwe na akili ya moja kwenda na mbili!, hesabu hupigwa na kuchezewa; hivi ni vipaji vya watu japo kwa sasa ni vipaji vilivyochacha!.

Hivyo basi, badiliko la kweli litakuja pale mtakapokuwa na sauti moja, vilevile kubadili mifumo katika njia sahihi lakini kama mtakuwa na sauti kila mtu anaongea lakwakwe hapo hakuna kusikilizana!, ni kutoana meno na manundu tu!.

Hata hivyo nanyi upande wapili mmeshakuwa wazee wapeni vijana nafasi wasimamie mambo!, ushamba wakukatiana umeme, internet na kuchukuana bila ridhaa hizo ni karne za zamani. Watu hivi sasa hawahitaji tu barabara bali barabara bora, sio tu umeme bali wa uhakika maisha yasasa umeme ni uchumi, sio tu internet bali ya uhakika.

Msiwe waoga wa mabadiliko.
Kumbe ua na point
 
Nakinzana na wewe kwani maandamano yenye tija sio lazima mfanye vurugu na watu mtoke damu ama mpoteze maisha!, mkiweza kuwa na sauti moja na kubalio moja hakuna anaeweza kukaa mbele yenu ipo migomo isiyoleta shida kwa wasiohusika na inaweza kuleta tetemeko kwa wahusika!, kama mkiigomea serikali mambo yake unafikiria nani ataweza kusimama katikati..?
hata wazee wetu waliwafanyia wakoroni migomo baridi na ilifanya kazi shida ni umoja tu!, yani bado tuna makundi wapo wanaoridhika na kidogo wanachopata japokuwa wanaumia!.
hakuna anaeweza kushindana na nguvu ya umma kama wakiamua kusimama kwa umoja.
Kwahiyo tukae tusubiri kupata mabadiliko baada ya watu wote kuwa na hiyo lugha moja? Toka lini mabadiliko yakasubiri watu wote kuongea lugha moja ndio yadaiwe? Punguza nadharia boss. Ni mabadiliko yapi hayajawahi kudaiwa kwa njia ya kistaarabu na yakapuuzwa? Mfano halisi, huu uchaguzi wa juzi watu hawakutaka hadi usogezwe mbele ili ufanyike kwa haki, je maombi yale yalikubaliwa? Ni hivi, watawala walioziba masikio huwa hawaelewi chochote kwenye njia za kistaarabu, machafuko pekee ndio huwa lugha wanayoielewa zaidi.

Mfano wa machafuko hadi kuleta mabadiliko ni huko Africa Kusini kwenye mfumo wa ubaguzi wa rangi. Na Nyerere aliwasupport weusi kwa machafuko yale waliyokuwa wanayafanya dhidi ya weupe waliokuwa wanaleta maendeleo ndani ya nchi ile.
 
Kwahiyo tukae tusubiri kupata mabadiliko baada ya watu wote kuwa na hiyo lugha moja? Toka lini mabadiliko yakasubiri watu wote kuongea lugha moja ndio yadaiwe? Punguza nadharia boss. Ni mabadiliko yapi hayajawahi kudaiwa kwa njia ya kistaarabu na yakapuuzwa? Mfano halisi, huu uchaguzi wa juzi watu hawakutaka hadi usogezwe mbele ili ufanyike kwa haki, je maombi yale yalikubaliwa? Ni hivi, watawala walioziba masikio huwa hawaelewi chochote kwenye njia za kistaarabu, machafuko pekee ndio huwa lugha wanayoielewa zaidi.

Mfano wa machafuko hadi kuleta mabadiliko ni huko Africa Kusini kwenye mfumo wa ubaguzi wa rangi. Na Nyerere aliwasupport weusi kwa machafuko yale waliyokuwa wanayafanya dhidi ya weupe waliokuwa wanaleta maendeleo ndani ya nchi ile.
Hujaelewa vurugu ama maandamano yaliyofanyika tarehe 29, watu waliharibu zaidi miundombinu ya watu binafsi huku kukiwa na tetesi tu kuwa miundombinu hiyo ikiwa ni yawatawala baadhi!. hili sidhani kama lilikuwa jambo sahihi kulifanya maana ni kama nadharia ilitakiwa kama ni mgomo watu wakaiguse serikali moja kwa moja!. na sio kugusagusa vitu vya watu kwakusadikika!.

Mkuu ipo migomo baridi inayoweza kuwa na athari moja kwa moja tena ikawa athari kali haswa!, mfano tu kutoshirikiana na viongozi wa serikali katika mambo yao hata kidogo hapo watajiona wamekaa katika hizo nafasi haafu hakuna wanaemfanyia kazi!. hata watu wakikaa bungeni utaona kama wanaweza kufanya mjadala wowote!.

Mkuu mi nafikiri zipo njia effective mkikaa nakufikiria vipo vitu mkigomea serikali moja kwa moja lazima ihahe na hizi njia zinahitaji umoja hata nusu ama robo ya watu wote wakiyafanya hayo basi inatosha!.
 
Umenena vyema. Lakini namna ya kutoka hapa tulipo lazima utaifa ndio utumike vinginevyo tutarudi kule kule Kwa muamba ngoma.

Au tusubiri wazee wastaafu wafe kwanza maana waliyoyafanya ndio huwafanya waogope mabadiliko.
Wastaafu wakati wewe bado kijana tu! Wao miaka inaenda yenu imesimama?
 
Ogopa sana jamii inayotegemea mtu mmoja awabadilishie maisha, hii inauwa Hari ya kujituma,uwezo wa kufikiri kwa kifupi inaongeza uvivu
Pili uongozi umekuwa aina ingine ya biashara, kila anayejishika kwenye mfumo anawaza kupiga tuu ndio sababu miradi inatekelezwa kwa mabilioni na kukamilika ni bado
Ogopa jamii inayoamua kitu kishabiki nasio kiuhalisia, yaani unakuta natetea jambo baya kisa chama cha siasa,dini, timu n.k
Ngumu sana kuendelea kwa jamii ambayo inatumia busara kupindisha sheria/kuepa makali ya sheria baada ya kuikiuka badala ya kutumia busara kufuata sheria na taratibu

Adios Amigo
 
Hujaelewa vurugu ama maandamano yaliyofanyika tarehe 29, watu waliharibu zaidi miundombinu ya watu binafsi huku kukiwa na tetesi tu kuwa miundombinu hiyo ikiwa ni yawatawala baadhi!. hili sidhani kama lilikuwa jambo sahihi kulifanya maana ni kama nadharia ilitakiwa kama ni mgomo watu wakaiguse serikali moja kwa moja!. na sio kugusagusa vitu vya watu kwakusadikika!.

Mkuu ipo migomo baridi inayoweza kuwa na athari moja kwa moja tena ikawa athari kali haswa!, mfano tu kutoshirikiana na viongozi wa serikali katika mambo yao hata kidogo hapo watajiona wamekaa katika hizo nafasi haafu hakuna wanaemfanyia kazi!. hata watu wakikaa bungeni utaona kama wanaweza kufanya mjadala wowote!.

Mkuu mi nafikiri zipo njia effective mkikaa nakufikiria vipo vitu mkigomea serikali moja kwa moja lazima ihahe na hizi njia zinahitaji umoja hata nusu ama robo ya watu wote wakiyafanya hayo basi inatosha!.
Hizo njia nyingine zitumie ww, sisi tumeamua kutumia hii na ina impact ya haraka kuliko hizo zako.
 
Back
Top Bottom