FisadiKuu
JF-Expert Member
- Nov 19, 2015
- 8,108
- 13,346
Habarini za Asubuhi wanabodi..
Uzi huu niuandika baada ya kusikiliza kupindi cha Straight Talk Afrika cha Shaka. Jana walikuwa wanaongelea siasa za Afrika Kusini na Cyril Ramaphosa. Binafsi sikuwa namjua Cyril vizuri mpaka alipokwaa madaraka kutoka kwa Zuma. Hapo ndipo nilishawishika kutafuta na kuusoma wasifu wake. Ukiacha mengine mengi, he is a purely businessman.
Tanzania tuna mipango na matazamio mengi mbeleni, tunaitaka Tanzania ya viwanda na ifikapo 2025 tunatazamiwa kuwa nchi yenye uchumi wa kati (Second world country).
Binafsi siamini kama hawa walioko madarakani sasahivi watatufikisha kwenye hata moja kati ya hayo mawili. Kufika huko hatuhitaji kauli za kibabe, sera zisizoeleweka za kuwakandamiza wawekezaji, kujifungia ndani tukiwasubiri mpaka wao waje.
Serikali yetu ya sasa labda inafanya mazuri kwenye baadhi ya mambo ambayo kiukweli ni machache na yanahesabika. Serikali ya sasa imejaa wanataaluma ambao kiukweli hawana background yeyote kiuongozi hasahasa kibiashara zaidi ya kuwa wakufunzi tu.
Mambo mengi yanakwama, viwanda tulivyohaidiwa hatuvioni vinavyofunguliwa vingi kama sio vyote vilikuwa initiated wakati wa Kikwete, wakati huo ilikuwa rahisi kushawishi wawekezaji sababu purchasing power ilikuwepo, hali ya fedha kwenye mzunguko ilikuwa nzuri. Ila sasa, ni wenyewe tu ndio wanajua wanachofanya.
Tukirudi kwenye mada kuu, Je, kwa hapa tulipo na huu mkwamo tunaoupitia bila shaka kwanza tunahitaji Rais msomi lakini pia Rais ambaye amebobea kwenye masuala ya kibiashara.
Hapa haraka lilinijia jina la ALI MAFURUKI. Kwa kiasi kikubwa naona Mtanzania huyu anaweza kutupeleka kule tunakotaka kwenda. Huyu amekulia kwenye buashara na anajua biashara haitaki ubabe, biashara yeyote duniani inataka NEGOTIATIONS, biashara haitaki two faced people. Kwamba leo tunaongea hiki alafu kesho tunageuka.
Kwa mtizamo wako; nani unaona atafaa kuwa mrithi wa JPM?
Uzi huu niuandika baada ya kusikiliza kupindi cha Straight Talk Afrika cha Shaka. Jana walikuwa wanaongelea siasa za Afrika Kusini na Cyril Ramaphosa. Binafsi sikuwa namjua Cyril vizuri mpaka alipokwaa madaraka kutoka kwa Zuma. Hapo ndipo nilishawishika kutafuta na kuusoma wasifu wake. Ukiacha mengine mengi, he is a purely businessman.
Tanzania tuna mipango na matazamio mengi mbeleni, tunaitaka Tanzania ya viwanda na ifikapo 2025 tunatazamiwa kuwa nchi yenye uchumi wa kati (Second world country).
Binafsi siamini kama hawa walioko madarakani sasahivi watatufikisha kwenye hata moja kati ya hayo mawili. Kufika huko hatuhitaji kauli za kibabe, sera zisizoeleweka za kuwakandamiza wawekezaji, kujifungia ndani tukiwasubiri mpaka wao waje.
Serikali yetu ya sasa labda inafanya mazuri kwenye baadhi ya mambo ambayo kiukweli ni machache na yanahesabika. Serikali ya sasa imejaa wanataaluma ambao kiukweli hawana background yeyote kiuongozi hasahasa kibiashara zaidi ya kuwa wakufunzi tu.
Mambo mengi yanakwama, viwanda tulivyohaidiwa hatuvioni vinavyofunguliwa vingi kama sio vyote vilikuwa initiated wakati wa Kikwete, wakati huo ilikuwa rahisi kushawishi wawekezaji sababu purchasing power ilikuwepo, hali ya fedha kwenye mzunguko ilikuwa nzuri. Ila sasa, ni wenyewe tu ndio wanajua wanachofanya.
Tukirudi kwenye mada kuu, Je, kwa hapa tulipo na huu mkwamo tunaoupitia bila shaka kwanza tunahitaji Rais msomi lakini pia Rais ambaye amebobea kwenye masuala ya kibiashara.
Hapa haraka lilinijia jina la ALI MAFURUKI. Kwa kiasi kikubwa naona Mtanzania huyu anaweza kutupeleka kule tunakotaka kwenda. Huyu amekulia kwenye buashara na anajua biashara haitaki ubabe, biashara yeyote duniani inataka NEGOTIATIONS, biashara haitaki two faced people. Kwamba leo tunaongea hiki alafu kesho tunageuka.
Kwa mtizamo wako; nani unaona atafaa kuwa mrithi wa JPM?