Tanzania: The Legacy of President Jakaya Kikwete (2005-2015)

Buchanan

JF-Expert Member
May 19, 2009
13,199
1,969
Wakati wa mdahalo jana ITV, JK amedai akumbukwe baada ya 2015 kwa mambo ya Elimu, Afya, nk!

Kwa mambo hayo mawili nitamkumbuka kwa shule za sekondari za kata kuongoza kufelisha na kujenga ukabila nchini.

Kwa upande wa afya nitamkumbuka kwa kukwepa hospitali zetu, kwa kuwa hazina kiwango, na kukimbilia kutibiwa nje ya nchi!

Wewe utamkumbuka JK kwa lipi baada ya 2015?
 
Mpaka sasa tayari imekwisha dhihirika kwamba top hot issues of national concern and interest kwa watanzania wote bila kujali vyama, imani nk katika awamu hii yako ya mwisho ni Tume Huru ya Kuchunguza Matokeo ya Uchaguzi ; Katiba Mpya, iliyosheheni Tume Huru ya Uchaguzi; kirahisi sana na bila kuangalia uso wa mtu; fanya haya yafuatayo na Watanzania watakukumbuka kama hero!!!!! second to Mwl- Mwl alileta uhuru; wewe utakuwa umeboresha uhuru huo!

Pokonya haraka mikononi mwa wapinzani na kukimbiza mjengoni hoja hizo bila kujali sisiemu na serikali yake wanasema nini?
(1) Uundwaji wa Tume Huru ya Kuchunguza Matokeo ya Uchaguzi wa 31.10.2010 ( Hapa watose kweli kweli Makame na Kiravu-maana hao ndiyo waliokaidi karipio la Dr PhD alipowataka waache kusoma matokeo feki)
(2) Kuandikwa kwa Katiba Mpya ya Watanzania wote-na Tume yake Huru ya Uchaguzi kama ile ya Kibaki/Raila (hapa kwa ujasiri tosa sisiemu-maana watanzania wana shauku kubwa ya kupata kipya kinyemi!!! at the end)
(3) Kuhusu viporo vya EPA, Richmond nk. (bila woga kabisa watose maswahiba wote ambao kamati ya Mwakyembe iliwa-condem!!!!! fumba macho!!; mpe Sadi Mwema naye aambulie ka-legacy japo kadogo kwa hawa jamaa-wewe watakupata wapi tena?)

At the end utakuwa nyota bara la Afrika second to Mwl, and by far above Kibaki/Raila, and by farthest, above Mugabe/Tvangirai legacies! Hii ni golden chance kwako. Ukipoteza hii chance, very sorry, you will be forgotten by history ya Tz!
 
HISTORIA (LEGACY) YA KIONGOZI HUANDIKWA NA KIONGOZI MHUSIKA MWENYEWE KWA JINSI ANAVYOWIWA KATIKA KIZAZI FULALI:

Ni kweli kuwa watu wengi sana duniani huzaliwa, huishi na mwisho wa siku huondoka usoni mwa ulimwengu kama vile hawakuwahi kwepo kabisa mahali hapa.

Kwangu mimi, jambo kama hili linasikitisha MNO kwangu inapotokeaa. Hata hivyo, historia nayo huwafunika kiurahisi mno sisi watu wadogo wadogo pindi tunapoondoka usoni mwa ulimwengu kana kwamba hatuwahi kabisa kuzuru katika sayari hizi za 'EARTH' au Dunia. Lakini, historia hiyo hiyo kamwe haiwatendei haki watu wakubwa kama WATAWALA pindi wanapoongoza na kuondoka kana kwamba hawakuwahi kwepo. Kwao viongozi historia huwahukumu vibaya sana tena bila huruma pindi wanapochezea hasa mambo yanayohusu MASLAHI YA UMMA.

Sasa basi, ni juu yao viongozi wetu wa leo wa kutuongoza 'Tupende Tusipende' wakajichagulia njia SAHIHI ya kufuata katika kujiandikia historia zao wao wenyewe leo hii. Sisi hata na vizazi vijavyo kazi yetu itakua tu ni kuzikumbuka historia hizo na kuendelea kusimuliana sawa sawa na jinsi watakavyoamua kujiandikia wenyewe.

Daftari langu la kunakilia historia za viongozi mbalimbali duniani akiwemo JK tayari ishafunguliwa hadi dakika hii hapa ...
 
Mtu wa Mungu

Hilo ndugu yangu sahau. Yaani achunguze mchakato uliomwezesha kurejea ikulu!!!! Kwa JK hiyo sahau, haitakuja itokee na wala hata chembe ya wazo hilo haimo moyoni. Legacy atakayoiacha ni ya rais mpenda watu, hana complication na ndiyo maana inafika mahali kijana anasafiri kutoka geita (bagamoyo??) hadi ikulu Dar kwenda kumshika mkono rais na kumpogeza kwa kuchaguliwa kuongoza nchi tena. Hiyo ni bonge ya 'legacy'.

Mtu kusafiri kwa baiskeli kutoka Geita, sengerema, mwanza, shinyanga, nzega, igunga, shelui, singida, manyoni, dodoma, morogoro, chalinze, mlandizi, kibaha, ubungo, magomeni hadi ikulu (siyo kupanda basi kutoka bagamoyo, tegeta, mwenge hadi msasani na kisha kuchukua baiskeli hadi ikulu???) siyo mchezo jamani. Inahitaji ujasiri tena basi bila hata kufuatiliwa na chombo chochote cha habari.
 
JF ni dhahiri kabisa JK anatafuta a trademark of Legacy in his existance as a president.... does JK deserve this hefty legacy in our country for a reborn of a new constitution

Je.... wadau gani mpaka imefikia 31/12/2010 wamekua mstari wa mbele kuhakikisha wanawakilisha matakwa ya wananchi kuhusu katiba mpya ili basi siku moja tuweze kuwapa stahi na heshima tukuku ya kutupatia katiba mpya

yaweza kuwa Mabere Marando.... pia Rev. Christopher Mtikila.., au James Mbatia..... pengine ni James Mapalala.... au Yusuf Makamba.... yupo Philip Marmo.... na Celina Kombani..... Wapo kina Ibrahim Lipumba na Mtatiro.... Usimsahau Mohamed Rashid..... Je pia Dr. Wilbroad Slaa au Freeman Mbowe na Zitto Kabwe...... NAE Augastine Mrema..... Wapo Kina Joseph Sinde Warioba na Frederick Werema......Usimsahau Dr.Azaveli Lwaitama na Yahya Mohamed au Rainfred Masaku... pia Askofu Laizer na Mokiwa.... au Kardinali Pengo na Askofu Kilaini..... yumo Mchungaji Zakaria Kakobe ..... na tena Mufti Gorogosi.... au Ali Hasan Mwinyi........ wapo kina Mzee Mwanakijiji.. na Raila Odinga....

Wapo wengi..... kwa kuwataja.... pia michango yao imekua chachu gani katika kutoa breakthrough towards coming draft new constitution.....
 
Legacy ya Katiba Mpya ni ya wale wote walio-campiagn kwenye uchaguzi mkuu wakiitaka katiba mpya...

wengine wote ni dandia dandia tu hakuna cha legacy wala nini... na wakiendelea dandia dandia hivyo bila kuwapa walio campaign kwamba ndio hoja yao kuu watoe mapendekezo zaidi ni wazi kwamba wataiharibu na ndio maana JK kasema inaweza kufanyiwa marekebisho mapema mara baada ya kuwa enacted...
 

mkuu.... nimekupata.... kwa hiyo JK amedandia hii ya kuandikwa katiba mpya... ninaweza kubali kwa sababu haikuwa kwenye sera (manifest) ya CCM......Nninakumbuka Dr. Slaa aliahidi kuandika katiba mpya ndani ya siku 100 kama angechaguliwa kuwa raisi..... je JK amemwiga (amedesa) Dr. Slaa kwa hili...? hivyo basi jibu lako ni wazi...JK does not deserve the legacy for the re writting of a new constitution
 
acheni ubinafsi, Katiba haijapatikana mnazungumzia sifa ziende kwa nani! Huu ni muda wa kujadili philosophies, values and issues ambazo zinapaswa kuwa reflected katika katiba. Halafu kwanza yaani mlitaka JK akatae katiba kuwe na confrontation, muandamane, watu wafe, image ya nchi iharibike, kisha katiba ipatikane.. ndo mfurahi. shenzi type.
 
None of the Above........ The time is right na Wananchi needs it. So if you force me. Ni legacy ya wananchi, bila kuidai hii haitapatikana na bila kuwa macho itakuwa ni changa la macho na viraka vya hapa na pale
 

mkuu.. hayo pia ni mawazo...yatapimwa hapa JF kama yana uelekeo hasi..... au...this is open forum.... and staged for great thinkers there is no way we could skip honouring the legacy to any one or any stakeholder for blowing whistle until the voice of the peoples power is now heard... call a spade.. spade JK jumped into this boat to fabricate legacy at his side
 
Katiba mpya ni hoja ya msingi ya Dr slaa ktk uchaguzi, alisema ndani ya siku 100 atakuwa ameanzisha mchakato wa kuunda katiba mpya, alikuwa haitaki hii iliyopo hata kidogo, akasema hata JK anafuata maelekezo yake, kuwa kweli ndani ya siku mia anataka kuanzisha, naamini maneno ya dr slaa yanatakiwa yawekwe ktk kumbukumbu. tHIS GOES TO DR SLAA
 

Alitoa ahadi mapema kuwa mengine mazuri ya wapinzani tutayachukuwa na kuyafanyia kazi.
 
Alitoa ahadi mapema kuwa mengine mazuri ya wapinzani tutayachukuwa na kuyafanyia kazi.

mkuu ahsante sana kwa umakini wako..... then the Legacy does not deserve him .... anabakia kuwa initiator and patriot of change ..... hilo nalikubali
 
jamani hilo swala la katiba lilikuwa linakera wengi sasa kama MH JK ameliona hilo na kulipa kipaumbele sioni kwanini asiheshimiwe kwa hilo kwani ni yeye aliyekuwa anasubiliwa atoe msimamo
 
suala la Katiba mpya kamwe haiendi kwa chadema, harakati ya kudai katiba mpya ni jambo liloanza tokea enzi za marehemu Chifu Fundikira

na kwa vyama vya siasa vilivyopambana na jambo hilo basi ni NCCR na CUF na sio hawa wapenda sifa na kurukia mambo juu kwa juu na kugeuza wao ati ndio walioanzisha mapambano
 

All in all , JK lazima apate Legacy kwani ndio kiongozi wa nchi aliye ruhusu wakati yupo madarakani kufanyika hicho kitu, hakuna jinsi ya kumkwepa. Hapa mtataja watu kibao ila mwisho wa siku ni yeye na serikali ndio watekelezaji wa hayo. Na hii huenda ikampatia Doctorate nyingine
 

Kwa hiyo akipewa doctorate nyingine ataitwa Penta-Dr. JK au?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…