Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Patashika ya Ligi Kuu Tanzania kuendelea tena leo Disemba 29, 2018 kwa michezo mitatu kupigwa katika viwanja tofauti. Gumzo ni Simba SC kuwakabili Singida United kwenye Dimba la Taifa jijini Dar es salaam.
Simba SC, Mnyama, Lunyasi ambao ni mabingwa watetezi wataingia katika uwanja wa Taifa wakihitaji alama tatu muhimu katika mchezo wa leo. Je Singida United wataweza kuwaruhusu kuvurumishwa na Simba SC?
Kumbuka mechi ni kuanzia saa 1:00 usiku. Usikose Ukaambiwa
Kikosi cha Simba SC dhidi ya Singida United kinachoanza leo hiki hapa..Jeshi la Patrick Aussems
Sent using Jamii Forums mobile app
Kabumbu liko katikati ya uwanja kuashiria kuanza kwa mchezo huu wa TPL
Naaam Mpira Umeanza Uwanja wa Taifa
Simba SC 0-0 Singida United
05' Bocco anamjaribu Ally Mustafa kwa shuti la umbali lakini anakaa vema na kudaka bila wasiwasi
Wanachukua Singida Utd kujaribu kupeleka mashambulizi, lakini wanapoteza mpira
07' Anakwenda Bocco lakini golikipa anatokea na kuharibu ile mipango yake
10' Hakuna timu imeona lango la mwezake uwanja wa Taifa TPL
Simba SC 0-0 Singida United
Singida Utd wanajaribu kupanga mashambulizi lakini, beki za Simba zinakaa imara.
15' Mpira unachezwa kwa pande zote kwa zamu ijapokuwa hakuna bao
17' Gooooooooooaaal Gooooooaaal
John Bocco anaandika bao la kwanza kufuatia pasi safi ya Kichuya ndani ya 18 za uwanja
Simba SC 1-0 Singida Utd
Simba wanazidi kuzidisha mashambulizi kuelekea Singida Utd huku wakitawala katikati
23' Goo la la laaaaaaa, Kichuya anashindwa kumalizia mpira uliorudi kufuatia shuti la Bocco. ilikuwa hatari
29' Go laaa laaa..Cleoutus Chama anapiga shuti la umbali mrefu na kupanguliwa na golikipa Ally na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda
30' Simba SC 1-0 Singida United
La la la Habib Kiyombo anashindwa kumalizia mpira wa Krosi ilikuwa nafasi nzuri kusawazisha bao
34' Singida Utd kwa mara nyingine wanakosa bao, baada ya shuti kupanguliwa na Ally Mustafa
35' John Bocco anapiga kichwa. Lakini mpira unatoka nje na kuwa gooal Kick
40' Kipute cha TPL uwanja wa Taifa Simba bado anaongoza bao moja
Singida Utd wanatengeneza mashambulizi lakini safu yao haijaleta matunda kuweza kusawazisha
Bocco anakosa bao lingine la wazi kwa shuti lake kutoka nje na kuwa gooal Kick, ilikuwa hatari lango la Singida Utd
45+2' Kuelekea kuwa mapumziko uwanja wa Taifa
Naaaaaaaam kipindi cha kwanza kimekamilika ambapo Simba wanatoka uwanjani wakiwa mbele ya goli moja bila dhidi ya Singida Utd
Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Taifa katika TPL, hakuna mabadilko kwa sasa kwa pande zote
Simba SC 1-0 Singida United
49' Gooooooooooaaal Gooooooooooaaal
Kichuya anaipatia Simba bao la pili ni pasi safi kutoka kwa Cleoutus Chota Chama
Simba SC 2-0 Singida Utd
Anakwenda kwa Obina upande wa Singida lakini wanashindwa kutulia eneo 18
55' Gooooooooooaaal kwa mara nyingine tena Shinza Ramadhan Kichuya anaandika bao la tatu..Kazi nzuri ya Cleoutus Chama 'Triple C'
Simba SC 3-0 Singida United
63' Simba wanakataliwa bao baada mpira kuingia wavuni. Mpira ulipigwa na Bocco
68' Anatoka Nicholas Cyan, anaingia Zana Coulibaly..Upande wa Simba
Kandanda safi linatandazwa hapa uwanja wa Taifa. Simba wanatakata
71' Simba SC 3-0 Singida Utd
Mpira unakwenda mbele ya lango Singida katikati uwanja Simba wanazidi kutawala mchezo
80' Singida wanacheza vizuri wakiwa na utulivu eneo kati
86' Okwi anakosa nafasi nzuri ya kuandika bao la nne hapa
Simba SC 3-0 Singida United
Kwa dakika hizi sidhani kama Singida wanaweza kufanya maajabu
90+3' Wakati wowote mpira utakuwa umemalizika
Naaaaaaaam mpira umekwisha uwanja wa Taifa katika TPL ambapo Simba SC wanaibuka kwa ushindi mnono wa mabao matatu bila majibu dhidi ya Singida United, Shiza Kichuya akifunga mabao mawili na kusaidia moja.
Simba SC 3-0 Singida United
Asanteni..
Ghazwat..
Simba SC, Mnyama, Lunyasi ambao ni mabingwa watetezi wataingia katika uwanja wa Taifa wakihitaji alama tatu muhimu katika mchezo wa leo. Je Singida United wataweza kuwaruhusu kuvurumishwa na Simba SC?
Kumbuka mechi ni kuanzia saa 1:00 usiku. Usikose Ukaambiwa
Sent using Jamii Forums mobile app
Kabumbu liko katikati ya uwanja kuashiria kuanza kwa mchezo huu wa TPL
Naaam Mpira Umeanza Uwanja wa Taifa
Simba SC 0-0 Singida United
05' Bocco anamjaribu Ally Mustafa kwa shuti la umbali lakini anakaa vema na kudaka bila wasiwasi
Wanachukua Singida Utd kujaribu kupeleka mashambulizi, lakini wanapoteza mpira
07' Anakwenda Bocco lakini golikipa anatokea na kuharibu ile mipango yake
10' Hakuna timu imeona lango la mwezake uwanja wa Taifa TPL
Simba SC 0-0 Singida United
Singida Utd wanajaribu kupanga mashambulizi lakini, beki za Simba zinakaa imara.
15' Mpira unachezwa kwa pande zote kwa zamu ijapokuwa hakuna bao
17' Gooooooooooaaal Gooooooaaal
John Bocco anaandika bao la kwanza kufuatia pasi safi ya Kichuya ndani ya 18 za uwanja
Simba SC 1-0 Singida Utd
Simba wanazidi kuzidisha mashambulizi kuelekea Singida Utd huku wakitawala katikati
23' Goo la la laaaaaaa, Kichuya anashindwa kumalizia mpira uliorudi kufuatia shuti la Bocco. ilikuwa hatari
29' Go laaa laaa..Cleoutus Chama anapiga shuti la umbali mrefu na kupanguliwa na golikipa Ally na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda
30' Simba SC 1-0 Singida United
La la la Habib Kiyombo anashindwa kumalizia mpira wa Krosi ilikuwa nafasi nzuri kusawazisha bao
34' Singida Utd kwa mara nyingine wanakosa bao, baada ya shuti kupanguliwa na Ally Mustafa
35' John Bocco anapiga kichwa. Lakini mpira unatoka nje na kuwa gooal Kick
40' Kipute cha TPL uwanja wa Taifa Simba bado anaongoza bao moja
Singida Utd wanatengeneza mashambulizi lakini safu yao haijaleta matunda kuweza kusawazisha
Bocco anakosa bao lingine la wazi kwa shuti lake kutoka nje na kuwa gooal Kick, ilikuwa hatari lango la Singida Utd
45+2' Kuelekea kuwa mapumziko uwanja wa Taifa
Naaaaaaaam kipindi cha kwanza kimekamilika ambapo Simba wanatoka uwanjani wakiwa mbele ya goli moja bila dhidi ya Singida Utd
Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Taifa katika TPL, hakuna mabadilko kwa sasa kwa pande zote
Simba SC 1-0 Singida United
49' Gooooooooooaaal Gooooooooooaaal
Kichuya anaipatia Simba bao la pili ni pasi safi kutoka kwa Cleoutus Chota Chama
Simba SC 2-0 Singida Utd
Anakwenda kwa Obina upande wa Singida lakini wanashindwa kutulia eneo 18
55' Gooooooooooaaal kwa mara nyingine tena Shinza Ramadhan Kichuya anaandika bao la tatu..Kazi nzuri ya Cleoutus Chama 'Triple C'
Simba SC 3-0 Singida United
63' Simba wanakataliwa bao baada mpira kuingia wavuni. Mpira ulipigwa na Bocco
68' Anatoka Nicholas Cyan, anaingia Zana Coulibaly..Upande wa Simba
Kandanda safi linatandazwa hapa uwanja wa Taifa. Simba wanatakata
71' Simba SC 3-0 Singida Utd
Mpira unakwenda mbele ya lango Singida katikati uwanja Simba wanazidi kutawala mchezo
80' Singida wanacheza vizuri wakiwa na utulivu eneo kati
86' Okwi anakosa nafasi nzuri ya kuandika bao la nne hapa
Simba SC 3-0 Singida United
Kwa dakika hizi sidhani kama Singida wanaweza kufanya maajabu
90+3' Wakati wowote mpira utakuwa umemalizika
Naaaaaaaam mpira umekwisha uwanja wa Taifa katika TPL ambapo Simba SC wanaibuka kwa ushindi mnono wa mabao matatu bila majibu dhidi ya Singida United, Shiza Kichuya akifunga mabao mawili na kusaidia moja.
Simba SC 3-0 Singida United
Asanteni..
Ghazwat..