Tanzania ni zaidi ya CCM, Chadema na CUF

Tanzania ni zaidi ya CCM, Chadema na CUF

sokoinei

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2012
Posts
1,832
Reaction score
566
Tanzania ni miongoni mwa nchi chache sana ktk bara la Afrika kama sio duniani yenye Amani ambayo imedumu kwa takriban miaka 35 tangia kupaikana kwa Uhuru.
Tangia miaka zaidi ya 20 ya utawala wa Rais wa kwanza wa Tanganyika Mwl Julius K Nyerere na miaka 10 ya utawala wa rais wa pili Alhaji Hassan Mwinyi,Tanzania ilikua ni nchi ya mfano kwa Nchi za Afrika na Dunia kwa ujumla.

Baada ya Utawala wa awamu ya tatu chini ya rais mstaafu Benjamin Mkapa Amani yetu ilianza kutoweka taratibu huku tukishuhudia 2001 maelfu ya Wazanzibar wafuasi wa CUF wakiuawa na Polisi kwa kisingizio cha kuandamana bila kibali. Si hivyo tu lakini matukio mengi ya hapa na pale yakitokea yakiwemo ya watu mmoja mmoja kupigwa risasi na polisi.

Utawala wa awamu ya nne wa chini ya Mh,Kikwete(CHAGUO LA MUNGU) nao ukaingia madarakani kwa NGUVU,ARI,NA KASI MPYA huku yale yale ya utawala wa tatu yakiendelezwa kwa Kasi,Ari,na Nguvu mpya.

Tofauti na tawala zote zilizotangulia utawala huu wa nne tumeshuhudia Mmomonyoko wa maadili ktk viongozi,tumeshuhudia nyufa ya UDINI ukikua kwa kiwango kikubwa hali iliyosababisha baadhi ya viongozi wa Dini kuuwawa na tumeshuhudia pia milipuko ya Mabomu ktk nyumba za ibada na ktk mikutano ya Siasa kitu ambacho hatukuwahi kukishuhudia.

Ni ktk utawala huu wa awamu ya 4 tumeendelea kuona Chombo kikuu cha kuisimamia serikali (yaani Bunge) likipoteza heshima kwa kutumika na serikali kuitetea.

Tumeendelea pia kushuhudia CCM chama tawala na chenye Serikali kikitumia Jeshi la polisi kuendelea kunyanyasa vyama Pinzani na wafuasi wake hususan CDM kwa kuwaweka Rumande mara kwa mara Viongozi na wafuasi wake na hata kuwaua,kuwajerihi na Kuwafungulia kesi za Ugaidi ili tu kuwaogopesha.

Tumeendelea kuona Chama kikuu cha Upinzani CDM kikitumia Nguvu ya Umma kwa maandamano na mikutano ya hadhara kupinga unyanyasaji wanao fanyiwa na Ccm kwa kutumia jeshi la polisi huku wafuasi wake wakipoteza maisha na wengine wakiishia kupata vilema vya maisha.

Ni miaka hii hii ya utawala wa awamu ya 4 tunashuhudia Mwenyekiti wa taifa CUF pro Ibrahim Lipumba akifanya siasa Misikitini kiti ambacho hatukuwahi kukishuhudia ktk awamu za tawala zote zilizopita.

Ufike sasa wakati Viongozi na watawala wajue kwamba Tanzania ni zaidi ya CCM,CDM na CUF. kwani kuendelea kuviruhusu vyama hivi kufanya haya wanayofanya kwa sasa ni kupoteza tunu hii ya Amani ambay inakaribia kupotea. Japo kuna wale wanao sema Tz hakuna amani ila kuna Utulivu lakini basi tuendelee kuiyenzi huu utulivu ulioko.

Ccm + Cdm + Cuf = Kutoweka kwa Amani Tz.
Mungu ibariki Tanzania!!
 
Ukilirejeasiasa za Tanzania tangu 1992 mfumo wa vyama vingi ulipo rejeshwa nchini utabaini kwamba CCM ina mzio/allergy na vyama vikuu vya upinzani.

Mziowa CCM dhidi ya vyama vikuu vya upinzani umeleta maafa mengi nchini, hebufuatilia
1995-2000: NCCR Ikiongozwa na Mreama ilikuwa chama kuku cha upinzani nchini.Walipigwa mabomu na kuzushiwa kila aina ya TUHUMA za UKABILA na CHUKI naikakisambartisha hadi Mrema akahamia TLP na kumwachia Mbatia NCCR. Wakati huu CHADEMAwalisifiwa kuwa Chama cha kistarabu nchini.

2000-2010: CUF ilikuwa chama kikuu cha upinzani: Mabomu yakahamia kwao, walipigwamabomu sawasawa, walizushiwa kila aina ya tuhuma za ugaidi, mtakumbuka visu namapanga ya Mahita na lugha kama za Ngangali na Ngunguli. Lakini ni kipindi hikiambapo Tanzania ilizalisha wakimbizi kwa mara ya kwanza katika historia(Wakimbizi wa SHIMONI –Mombasa), Mpaka leo CUF hufanya makumbusho ya maafa ya January21.

2010:2015 : CHADEMA ni Chama kikuu cha upinzani : Mabomu, tuhuma zile zilezilizokuwa zinaelekezwa NCCR na CUF zimehamishiwa kwa CHADEMA na Vifo dhidi yaraia wema vinaendelea kuwa sehemu ya utamaduniwetu.
Suruhisho:
Ilikuliokoa Taifa na maafa ya raia wasio nahatia, CCM inahitaji kujengewa Uwezo wakuishi na kufanya kazi na vyama vikuu vya upinzani bila kumwaga damu yaWatanzania.

Hili linawezekana kwa kujengea CCM mfumo na uratibu wa kuwapata viongozi waadilifu, weledina waliobobea katika fani wanazo ziongoza, tofauti na sasa ambapo,wenye pesahata za uwizi, wezi wa vyeti na ndugu/marafiki hupewa madaraka yanayo wazidikiimo.
 
Mie siilaumu CCM bali vyama vya upinzani vyenyewe. Chama kimoja kikiandamwa vilivyosalia vinajiona vyenyewe ni "watoto" kipenzi cha CCM. CUF ilipokuwa inahujumiwa na watu wake kuuwawa kule Zenji kama hivi sasa CHADEMA inavyofanyiwa kuna baadhi ya vyama vya upinzani viliungana na CCM kuikejeli CUF.

Ufumbuzi ni vyama hivi kujitambua kuwa ni vyama vya upinzani na kuwa wamoja kupinga udhalimu wa CCM kwa nguvu zote. Udhaifu huu wa vyama vya upinzani unawapa nafasi watu kama kina Pinda kujiropokea watakavyo kama alivyofanya leo bungeni
 
Kuna unafiki mkubwa sana katika vyama vya upinzani. Ni kweli vyama vyenyewe huhujumiana na kuzungukana...na wapo hata ma"agent" wa chama tawala ndani ya vyama vya upinzani. Mfano mzuri ni Lyatonga aliyeuuza upinzani huko nyuma. Hata hivyo hatuwezi kubisha kuwa allergy ya CCM kwa upinzani ipo na ilianzishwa na Nyerere mwenyewe wakati wa uongozi wake. Aliwanyamazisha na kuwasweka ndani watu, na ku injika utawala mkuu wa chama tawala - party supremacy. Hiyo hangover bado haijawatoka!
 
Kwani Tanzania ni ya Nani?

Sent from my BlackBerry 9780using JamiiForums
 
Sasa kama vyama vyote vikuu vinagombana na CCM na vikishakufa CCM haivijali, huoni kuwa tatizo ni CCM?

Kama ingelikuwa hivyo, mbona hatujasikia vyama vya upinzani vikipigana vyenyewe kwa vyenyewe?

Muwe na aibu wakati mwingine eti SIILAUMU CCM................. Aisifiaye Mvua, kweli imemnyea.
Mie siilaumu CCM bali vyama vya upinzani vyenyewe. Chama kimoja kikiandamwa vilivyosalia vinajiona vyenyewe ni "watoto" kipenzi cha CCM. CUF ilipokuwa inahujumiwa na watu wake kuuwawa kule Zenji kama hivi sasa CHADEMA inavyofanyiwa kuna baadhi ya vyama vya upinzani viliungana na CCM kuikejeli CUF.

Ufumbuzi ni vyama hivi kujitambua kuwa ni vyama vya upinzani na kuwa wamoja kupinga udhalimu wa CCM kwa nguvu zote. Udhaifu huu wa vyama vya upinzani unawapa nafasi watu kama kina Pinda kujiropokea watakavyo kama alivyofanya leo bungeni
 
Ni wakati mwafaka kwa wananchi kuchuja uhalali wa vyama na dola katika nchi hii. Lasivyo tunakokwenda ni kubaya zaidi.
 
Ni wakati mwafaka kwa wananchi kuchuja uhalali wa vyama na dola katika nchi hii. Lasivyo tunakokwenda ni kubaya zaidi.
 
Wakuu JF, Amani iwe Nanyi.

Mara Nyingi sana Kauli za Viongozi wa CHADEMA mara inapotokea Kutendewa Mabaya na Serikali na CCM Yake zimekuwa too Diplomatic.
Msimamo wa Viongozi wa CHADEMA katika Matukio yanayotekea ndiyo umekuwapa ukiwapa Bichwa CCM na Serikali yake
Kuendeleza Ukandamizaji, Udhalilishaji na Mambo kama Hayo.
Tumeona Kauli za Kudhalilisha Kabisa zitolewazo na Viongozi wa Serikali na CCM Kwenye Matukio Mbali mbali, Kauli hizo zinachagizwa sana na Misimamo wanayoonesha Viongozi wa CHADEMA pale panapotokea Sintofahamu Baina ya Serikali / CCM na CHADEMA.
Rejea Msimamo wa Mgomo ulioitishwa na CHADEMA kushinikiza Kujiuzulu Kawambwa na Mulugo Baada ya Matokeo ya Kidato cha Nne.
Rejea jinsi Viongozi wa CHADEMA walivykubaliana na IGP kusitisha Maandamano eti kisa Ziara ya Rais wa China on the same Date.
Rejea Kauli za Viongozi wa CHADEMA kwa wana Arusha, kauli kama "Tulieni, tunafanya Mawasiliano na Serikali", "Vuteni Subira" n.k Kimsingi zinavunja Morali ya Nguvu Kubwa ya Wa Tanzania iliyo Nyuma yenu.
Nimekuwa wakati Mwingine najiuliza je, Labda Viongozi wetu wa CHADEMA hawaijui Nguvu Kubwa ya Umma liyonyuma yao ambayo Kimsingi inasubiri tu Muongozo kutoka Kwao?????
Kwa Matukio yanayotokea Arusha, ilitosha Kabisa Kuwaonesha watawala na CCM Nguvu Kubwa ya Umma ambayo CHADEMA inayo, Lakini Viongozi wetu wakaishia kuwa Soft Kabisa.
Hebu angalia Kauli za Ku dhalilisha za Chagonja, "Mbowe amejificha, kama amekomaa Kisiasa na ajitokeze"
Hiki Kiburi cha Wa Tawala na CCM kinaongezeka kwa kuona kuwa Viongozi wetu wa CHADEMA wanashindwa Kuitumia Nguvu kubwa ya Umma iliyo Nyuma yao.
Ona Kauli za Pinda Bungeni leo, Huu ni Udhalilishaji wa Hali ya JUU kwa CHAMA ambacho kina Nguvu Kubwa na Support ya Umma.
Kimsingi CCM na Serikali yake kwa Sasa wako Busy kuidhoofisha Nguvu Kubwa Kabisa ambayo iko Nyuma ya CHADEMA na ambayo kwa sasa wamegundua kuwa Viongozi wa CHADEMA wanashindwa Kuitumia Nguvu hiyo kwenye Fursa Mbali mbali Kabisa.

Viongozi Mkionesha Uoga,mnawaambukiza uoga pia na Wa Pambanaji, inakuwa ni Kama Askari Vitani ambaye anaiona Hofu ya Kamanda wake, Je yeye atakuwa katika Hali Gani.

cc
Dr.W.Slaa John Mnyika , Molemo Tumaini Makene Crashwise Mungi Arushaone, Mikael P Aweda

Angalizo,

===============================================================
Najua kuna Lumumba Project ambao watakuja Hapa na Povu, Mkia Juu Kutaka kupindisha Mjadala.
Naomba wapuuuzwe kwa Kiwango cha Juu Kabisa kwa Kutojibizana nao
===============================================================
 
Last edited by a moderator:
Wanajamvi habarini za mchana! Nimekuwa nikifatilia kwa umakini mkubwa seleka la hivi vyama viwili ambavyo vinajiita ni vyama vikuu ya upinzani tanzania, kimsingi nimegundua kuwa vyama hivi vyote havina nia ya dhati ktk kumsaidia mwananchi na ndo maana kila chama kinajaribu kurusha mpira kwa mwenzake kuhusu kuhusika na vurugu hizo. Kimsingi viongozi wa vyama hivi wapo ktk kupigania matumbo yao na ndio maana hawaoni hasara ktk kupoteza maisha ya watanzania wasiokuwa na hatia. Mwisho kbs namalizia kwa kusema kuwa Watanzania tuwe makini na vyama hivi kwani maisha na amani ya Tanzania na Watanzania wake ni zaidi ya vyama hivi viwili na chama kingine chochote kisichojali maisha ya Watanzania. Thanx!
 
Kumekuwa na mwendelezo ya uvunjifu wa amani katika nchi yetu hasa inapotokea maslahi ya kisiasa kuingiliwa. Yanayoendelea sasa, si mageni katika Taifa hili kwani tuliyashuhudia mwaka 1995 chini ya upinzani mkali wa NCCR-Mageuzi, mwaka 2000 chini ya upinzani wa CUF, na sasa chini ya CHADEMA. Kuna bahati moja kubwa tu inayofanya nchi iendelee kuwa na utulivu wa mashaka; kwamba hakuna ushirikiano baina ya vyama vya siasa. Wakati CUF wakifanyiwa matendo hayo miaka zaidi ya 10 iliyopita ikiwa pamoja na mateso na mauaji ya Pemba, jamii iliona kuwa si suala linalowahusu watanzania bali ni ukaidi wa chama cha CUF. Hata hivyo, watanzania walijisahau na wanaendelea kujisahau kwamba adui wa CCM si NCCR, CUF wala Chadema. Ni chama chochote cha upinzani chenye nia ya kweli yakukitoa CCM madarakani na kushika Dola. Chama chochote kitakachokuwa na ndoto hizo lazima kikutane na mkono wa CCM. Au kwa kifupi, adui wa CCM ni demokrasia yeyote itakayotoa fursa ya kuruhusu chama chote cha siasa kuwa na haki ya kushika dola na kuwatumikia wananchi. Ni katika kutolitambua hilo ndio maana Chadema hawakuona kuwa yaliyokuwa yakiwakuta CUF, na wao yangekuja kuwakuta. Ni kutokana na sababu hizo leo NCCR, TLP, CUF wanaona yanayowakuta CHADEMA wao hayawahusu. Huku ni kujidanganya kwa vyama vya siasa na watanzania kwa ujumla. Maana halisi ya mfumo wa Demokrasia ya vyama vingi ni kutoa uweledi kwa wananchi katika kupima na kuamua nani awe kiongozi wao-si vinginevyo. Wakati fulani, nashawishika kuamini kuwa Chadema ndio wakorofi na wakaidi. Hata hivyo, napuuzia kuamini hivyo kwa kuwa Chadema si wa kwanza kuyapata hayo. NCCR, CUF yaliwafika dhidi ya chama kilekile kinachowasulubu Chadema leo, CCM.
Je CCM ina haki hiyo kufanya inayofanya? Jawabu ndio. Kwanini? Ina dola, ina Serikali, ina Jeshi ina Polisi ina Mahakama, ina Mgambo, ina Magereza. Ni vyombo hivi ndivyo vilivyomfanya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kufungulia "mlango wa uani" kwa Polisi namna ya kukabiliana na "wakorofi".

Hata hivyo kuna jambo moja la msingi ambalo CCM hawana budi kulifanyia kazi. HALI ZA MAISHA YA WANANCHI NA TOFAUTI YA KIPATO. Kasi ndogo au kutokuwepo mipango ya makusudi na madhubuti ya kupunguza tofauti ya kipato na kuwafanya watu waweze kumudu japo milo miwili kutaondoa LADHA ya CCM katika kutawala. Ni bahati njema CCM na jamii leo inashuhudia mageuzi makubwa ya namna ya kudai haki ambayo wananchi wanaitaka. Tumeona haya Tunisia, Misri na kwingineko. Ni muda mfupi tu umepita, Serikali ya Majiji makubwa ya BRAZIL (Rio de Janeiro na Sao Paolo) ambapo wananchi wanaandamana kupinga ukali wa maisha pamoja na ongezeko la Nauli ya usafiri wa UMMA. Pamoja na Serikali kudai kuwa ongezeko hilo ni dogo lakini imesalimu amri na kurejesha nauli ya zamani. Lakini maandamano ya Brazil yana takwimu za kufundisha na kuelimisha.
56%-wanapinga kupanda kwa nauli
40%-wanapinga rushwa kwa viongozi wa Serikali
31% dhidi ya vitendo vya uonevu kwa raia
24% wanataka mfumo mzuri wa usafiri
Lakini jambo la kushangaza ni kuwa 71% wanaandamana kwa mara ya kwanza na 53% ni vijana walio na umri chini ya miaka 25. Aidha chanzo cha maandamano kimeelezwa ni kupinga kwa nauli lakini kumejitokeza watu ambao walikuwa na sababu zaidi ya hizo. Sasa wanataka mifumo bora ya elimu, afya na miundombuni pamoja na huduma za jamii (Safari moja huanzisha nyingine). Agenda si nauli tena. Tujifunze hapa kutoka Brazil, na Serikali jifunzeni kwamba binaadamu ni nyoka anapochokozwa na kuchoka.


Adha zinazowafanya wabrazil kuandamana hazitofautiani na adha wanazokumbana nazo watanzania. Ndiyo kusema TANZANIA SI KISIWA LINAPOKUJA SUALA LA MACHAFUKO NA MAANDAMANO. Na mbaya zaidi, pamoja na Serikali kurudisha nauli ya zamani, haikusaidia kuwaondoa waandamanaji barabarani. Ndiyo madhara ya kuachia au kuandaa hali ya kufikia watu kupandisha hasira na kuandamana. Majibu wa Waziri mkuu, bungeni bila shaka yamepungua hekima kwa nafasi aliyo nayo. Ni kauli ambayo iko siku itakumbukwa na kutafutwa ilipo ikwa watu wataendelea na maisha ya kusubiri Daladala Posta ya kumfikisha Kimara toka saa 10 jioni hadi saa 4 usiku na kupambana na foleni inayomfikisha kwake saa 7 usiku huku akihitajika kuamka saa 10 akfajiri kuanza siku mpya. Ni kauli itakayotafutwa iwe ushahidi aidha duniani au mbinguni. Ni ukweli usiopingika kwamba uweledi kwa jeshi la Polisi umepungua na chuki baina ya Polisi na Wananchi wa Kawaida inaongezeka hivyo kitendo cha kutoa kauli ya namna hii, itajenga aina mpya ushirikiano baina ya Polisi na Wananchi na hatimaye Wananchi na Serikali yao. Sababu kubwa ya watu kujitoa muhanga ni kutokuwa na matumaini yoyote ya kuishi vizuri duniani baada ya kuuawa kwa wazazi wake kwa sabau za kisiasa. Bila shaka watoto wa Mwangosi, na Judith wengine waliokufa au watakaokufa katika mazingira ya namna hiyo hawataipenda Serikali ya CCM katika maisha yao yote na ni mwanzo wa kutengeneza waasi wa kudumu wa Serikali. Hofu yangu ni idadi ya waasi watakaotengenezwa na Polisi katika mazingira ya namna hiyo kutokana na kauli ya Mh. Waziri Mkuu. Waacheni Chadema wafanye mikutano na maandamano, waacheni CUF wafanye mikutano na maandamano; waacheni NCCR wafanye hivyo; wananchi watawasikiliza lakini watapima; nyie simamieni Ilani ya Chama Chetu, wananchi ni wajuzi wa kuchambua na kuchagua na watatoa majibu kwenye sanduku la kura wala si kwenye mikutano.

Nikiwa mtanzania naomba kuwasilishamaoni yangu na kuiomba Serikali kupiga kazi ya kusimamia Ilani ya Chama Chetu badala ya kupoteza muda na hatimaye kujikuta watupu 2015 na hivyo kutumia nguvu kubwa zaidi ya hii mnayotumia sasa kutafuta ushindi wa nje ya kura.
 
Mie siilaumu CCM bali vyama vya upinzani vyenyewe. Chama kimoja kikiandamwa vilivyosalia vinajiona vyenyewe ni "watoto" kipenzi cha CCM. CUF ilipokuwa inahujumiwa na watu wake kuuwawa kule Zenji kama hivi sasa CHADEMA inavyofanyiwa kuna baadhi ya vyama vya upinzani viliungana na CCM kuikejeli CUF.

Ufumbuzi ni vyama hivi kujitambua kuwa ni vyama vya upinzani na kuwa wamoja kupinga udhalimu wa CCM kwa nguvu zote. Udhaifu huu wa vyama vya upinzani unawapa nafasi watu kama kina Pinda kujiropokea watakavyo kama alivyofanya leo bungeni

Sasa kama vyama vyote vikuu vinagombana na CCM na vikishakufa CCM haivijali, huoni kuwa tatizo ni CCM?

Kama ingelikuwa hivyo, mbona hatujasikia vyama vya upinzani vikipigana vyenyewe kwa vyenyewe?

Muwe na aibu wakati mwingine eti SIILAUMU CCM................. Aisifiaye Mvua, kweli imemnyea.

Sikonge unachoongea ni sawa. Lakini kwa upande mwingine CCM hawana mbinu halali za kuongoza nchi huku wakiwa wanapata upinzani mkali kutoka vyama vya upinzani, ilitakiwa wajifunze kutoka kwenye nchi ambazo zimefanikiwa kuendesha nchi kwa utulivu na amani chini ya mfumo wa vyama vingi.
Vyama vya upinzani vilitakiwa vishtuke ni kwa nini CCM wanatumia nguvu nyingi kudhoofisha chama chochote chenye nguvu katika upinzani, ilitakiwa vyama vya upinzani wakae chini pamoja kutafuta ufumbuzi wa hilo suala, badala yake wamekuwa wanafiki, akiandamwa mwenzao wao wanatulia. Kwa hapo lawama ni 50, 50 kwa CCM na kwa vyama vya upinzani.


Vyama vya upinzani kupigana sio lazima iwe mtaani. Tumeona bungeni mara kadhaa kuwa vyama vya upinzani haviungani kutetea hoja, tumeshuhudia vyama kadhaa vya upinzani vina side na CCM kupiga hoja ya chama kingine cha upinzani, huko ndio kupigana kwenyewe.
 
Hii ni Tanzania ambayo wengi wetu tumezaliwa na tukaikuta ikiwa ina utulivu na sio amani kama wanavyodai hawa wanaofikiria ya kuwa hatuna akili siku zote (CCM).

Hii ni Nchi yetu sote na sio Nchi ya CCM hata kidogo. Pale tunapoamua kufanya mabadiliko wanachanganyikiwa nini sasa?? wanafikiri watatawala miaka yote na familia zao na jamii zao??

Tumechoka na tunaumia sana kuona vitendo vya kumwagwa damu na CCM tena kipumbavu kabisaa...

2015 Hata sisi tutakuwa na utaratibu wa kuchukua Nchi ndo mjipange haraka sana. Chukueni Chenu Mapema kwa maana mwana wa CHADEMA ajapo 2015 mtashangaaaaaaaaa.
 
Tabia za pepo mchafu anayeitwa ccm hizi hapa

  1. Anaua na kuteka watu bila huruma kwa mabomu, sumu, na silaha za moto yeye cha msingi awe na madaraka. Udiwani tuu, anagiza bomu kulipua watu kwenye mkutano wa hadhara
  2. Ana kiburi na roho mbaya, ona kina kagonja na mwigula wanavyobehave, ni kwa sababu ya pepo ccm aliyewaingia
  3. Ufisadi kwake ndo maisha ya kila siku. Ili akupende lazima uwe fisadi, hakuna kulipa kodi, na kubali kuingia mikataba wa wizi kuuza nchi mfano kina Richmond, meremeta, buzwagi, na mingineyo. Mtu kama chenge ana nguvu sana maana anatimiza masharti ya pepo mchafu ccm
  4. ili upate cheo lazima uwe mtu wa madeals, na mwizi, ana uwe tayari kumwaga damu
  5. lazima uwe mtu mwenye uweze wa kudanganya na kufunika ukweli, kama vile lukuvi, pinda, wanavyofanya, na kutoa ahadi hela kwa mfano kikwete, nk
  6. Ukijaribu tuu kwenda kinyume na mashari ya pepo mchafu ccm , anakuua kwa sumu au risasi, mfano kina mwakembe, kolimba, nk
  7. Upati cheo kikubwa serikali au vyombo za usalama hadi ukubali masharti ya pepo mchafu ccm, mfano, kudanganya, kuiba, kuua, kuhamisha fedha, na kufanya biashara chafu
  8. Lazima ukabali kuvaa mafunguo ya pepo mchafu, ali mradi usilipe kodi
Pepo mchafu ccm ana sifa zote za shetani lusifa, mfano, kuua, kuiba, kuzini, roho mbaya, kukosa huruma, uchafu wa moyo, nk. Tunahitaji kuwaombea watanzania wenzetu ambao wameingilia na pepo machafu ccm, na kuendelea kukemea huyu pepo anayeangamiza taifa hii

Weka mengine unayoyajua kuhusu pepo mchafu ccm
 
hakuna hata mwanaccm mmoja mwenye huruma na mtanzania maskni, kwa sababu pepo mchafu ccm ana roho mbaya, na masharti yake lazima kuiba mabilioni kwenye halmashauri zote, hazina, na bot, na kukwepa kodi, pamoja na kushiriki kwenye tenda za uongo
 
Ndugu zangu wa Jf kwanza salam,

Nimejaribu kutafakari sana juu ya mwend mzima wa siasa zetu katika majukwaa,nimechambua sana,kwa hakika nimekuja na hiki kwamba SIASA ZISITUKISHE KATIKA KISIWA CHA MACHAFUKO.

Inasikitisha sana kuona wanasiasa wengi wanapkuwa majukwaani wanaacha kuzungumzia maendele ya wananchi na jinsi ya kujikomboa ktk dimbwi hili la umasikini matokeo yake wamekuwa wakipigana vijembe ambavyo mwisho wa siku inakuwa mbegu mbaya sana katika ustawi wa taifa letu.Sisi ni mashahidi juu ya matukio mengi sana ya uvunjifu wa amani ambayo mengi ya yametokana na siasa chafu.

Nasikitika kuona kwamba na wale wanapandikizwa hizo chuki za machafuko wanazilea na kuzipalilia na kukua,nisingependa kuona tunalipeleka Taifa letu kwenye hari mbaya kama ya Siria,DRC,Sudani n.k.Tukumbuke kwamba taifa letu limekuwa mfano wa nchi nying sana duniani kama kisiwa cha amani na watu wanajifunza mengi sana kutoka kwetu.

Siasa ni nguvu za hoja zenye mashiko ambazo zinaitaji hekima ya hali ya juu,na si kutafuta umaarufu kwa kutukanana,na kuanzisha mipang ya ajabu.

Haijarishi kwamba wewe ni nani katika nchi hii,hakuna aliye juu ya sheria na ndo maana kuna vyombo vya dola vinavytuongoza,sasa inapotokea tunaenda kinyume na maelekezo ya vyombo vya dola ambavyo vipo kisheria katika kulinda na kuhakikisha amani ya nchi,kukinzana na maelekezo yao ilimradi tu ujipatie umaarufu kwa wanachama wako huko ni kusababisha uvunjifu wa amani na hakjuna ataye vumila katika isipkuwa sheria itachukua mkondo wake kwa mujibu wa utawala wa sheria.

Nimesikitika sana kuona Mh.Mbowe kwa jinsi ulivoywahadaa wananchi kwamba una ushahidi wa kile kilichotokea arusha,na watu wakawa makini sana kusubiri nini unacho,lakini kwa kile tunachokiita kwamba kutojiamini ukashindwa hata kusemama lolote na matokeo yake ukakana hauna ushahidi ila cha ajabu ulipotoka nje tu kwa waandishi wa habari ukapindua na kusema una ushahidi ili wananchi waendelee kukuamini...sasa nauliza kweli kabisa bado unanunua fikra za watu kwa uongo wako na uzandiki ili wakuonee huruma wa kukupa kura zaidi...lah hasha.

hiy haitoshi Mh.Raisi akakuambia kama hauna imani na plisi peleka ushahidi ikulu bado umeendelea kuwatolea machoo wananchi na kujikanyagakanyaga ukidai tume huru,umesahahu kwamba hiyo tume huru itaundwa na nani na kupeleka hiyo taarifa wapi.Nakuomba kama siasa huziwezi ni bora ukaendelee kuendesha casino yako kuliko kutaka kutupeleka kule ambako hatukuwai kukufiria hata siku mooja.

Vyama vya upinzani popote pale uendapo ni chachu ya maendele ya nchii yoyote ile,tunavipenda sana vyama vya uypinzani lakini nafikiri vimekosa viongozi sahihi.
 
Ndugu zangu wanasiasa na hasa viongozi wakuu kutoka chama tawala cha CCM, tambueni kuwa Tanzania ni nchi nzuri, ya amani na tulivu. Kwa hiari yetu tulikubali kuingia katika mfumo wa vyama vingi. Bila shaka viongozi na wanachama wa CCM, wanatambua kwa nini tuliamua kuingia katika mfumo huu.
Nchi inaelekea kubaya ikiwa mikononi mwao. Wana CCM inaelekea bado wameganda na mfumo wa chama kimoja, ambapo serikali iliyopo madarakani aghalabu huendelea kuvitumia vyombo vya dola kulinda na kuendeleza utawala wao.
Inapofika msimamizi na mtendaji mkuu wa shughuli za serikali (PM), anabariki polisi kuwapiga raia kwa namna yoyote ile, kwa kweli mwananchi wa kawaida anahoji ni nani aghalabu atakaribia kuvifikia viatu vya hayati mpendwa wetu Edward Moringe Sokoine. Hekima ya kawaida iko wapi? Jamii itashangaa vipi itakapoona polisi wetu wakiua raia wasio na hatia? Sote tunatambua idadi ya raia waliouawa na polisi (Mwangosi akiwa shahidi), lakini jamii ilikuwa ikijiiliza jeuri hii ya polisi kuua raia wake inatoka wapi! Leo mkuu wa nchi anapobariki unyama huu kupitia kwa PM wake, kwa kweli mmoja anauliza upendo, uadilifu, udemokrasia wa viongozi wetu uko wapi?
Kiongozi mmoja wa kambi ya upinzani amekaririwa akisema kama serikali yetu haikuwa tayari kuruhusu mfumo wa vyama vingi na demokrasia kuwepo hapa Tanzania kwa nini walikubali?
Hatujifunzi toka kwa majirani zetu? Sote tumeshuhudia wakenya walivyofanya maandamano kupinga wabunge kujiongezea mishahara. Polisi walisindikiza maandamano yale wakiwa umbali upatao mita 200, kamwe hawakudiriki kuingilia maandamano yale!
Au viongozi hawa wa CCM wanataka yale maandamano kama ya Misri na Tunisia yatokee Tanzania?
 
Ndugu zangu wanasiasa na hasa viongozi wakuu kutoka chama tawala cha CCM, tambueni kuwa Tanzania ni nchi nzuri, ya amani na tulivu. Kwa hiari yetu tulikubali kuingia katika mfumo wa vyama vingi. Bila shaka viongozi na wanachama wa CCM, wanatambua kwa nini tuliamua kuingia katika mfumo huu.
Nchi inaelekea kubaya ikiwa mikononi mwao. Wana CCM inaelekea bado wameganda na mfumo wa chama kimoja, ambapo serikali iliyopo madarakani aghalabu huendelea kuvitumia vyombo vya dola kulinda na kuendeleza utawala wao.
Inapofika msimamizi na mtendaji mkuu wa shughuli za serikali (PM), anabariki polisi kuwapiga raia kwa namna yoyote ile, kwa kweli mwananchi wa kawaida anahoji ni nani aghalabu atakaribia kuvifikia viatu vya hayati mpendwa wetu Edward Moringe Sokoine. Hekima ya kawaida iko wapi? Jamii itashangaa vipi itakapoona polisi wetu wakiua raia wasio na hatia? Sote tunatambua idadi ya raia waliouawa na polisi (Mwangosi akiwa shahidi), lakini jamii ilikuwa ikijiiliza jeuri hii ya polisi kuua raia wake inatoka wapi! Leo mkuu wa nchi anapobariki unyama huu kupitia kwa PM wake, kwa kweli mmoja anauliza upendo, uadilifu, udemokrasia wa viongozi wetu uko wapi?
Kiongozi mmoja wa kambi ya upinzani amekaririwa akisema kama serikali yetu haikuwa tayari kuruhusu mfumo wa vyama vingi na demokrasia kuwepo hapa Tanzania kwa nini walikubali?
Hatujifunzi toka kwa majirani zetu? Sote tumeshuhudia wakenya walivyofanya maandamano kupinga wabunge kujiongezea mishahara. Polisi walisindikiza maandamano yale wakiwa umbali upatao mita 200, kamwe hawakudiriki kuingilia maandamano yale!
Au viongozi hawa wa CCM wanataka yale maandamano kama ya Misri na Tunisia yatokee Tanzania?

well said soon wazee wa mtapisho watatiririka na uzi usikatishwe tamaa
 
Rubani ameshakufa ndege iko kwenye autopilot ikiishiwa mafuta ndo kwa heri.
 
Back
Top Bottom