Ndahani
Platinum Member
- Jun 3, 2008
- 18,119
- 9,049
Tanzania nchi yangu, yenye uso wa kungaa,
Afrika na Ulimwengu, sifa tele tapakaa,
Wahindi nao wazungu, hakuna wa kuhadaa,
Jinsi ilivyo sifika, kwa uongozi thabiti.
Ilijulikana pote, Tanzania ya mwalimu,
Iliheshimu yoyote, aliyependa nidhamu,
Kaunda naye Obote, na asiye kichwa ngumu,
Tanzania ya mwalimu, nchi yenye msimamo
Umoja wetu wa ndani, kamwe hukutisika,
Utaifa akabuni, ukabila kufutika,
Akaipa uthamani, ikawa ya kutuka,
Ndivyo ilivyosifika Tanzania nchi yangu.
Akatua madaraka, ili kuipa uwezo,
Maendeleo haraka, demokrasia kigezo,
Yeye kote akawika, kwa hizo zake sifazo.
Mwalimu akangatuka, kutuachia mfumo
Nini kimetetereka, hata kufikia hapa,
Rushwa imetuchakaza, sasa tunatapatapa,
Viongozi wasowaza,kula fujo kama papa,
Nchi inaharibika, rushwa tele zimejaa.
Tamaa iso kipimo, ya mali na madaraka,
Viongozi waliomo, utajiri wa haraka,
Wamelisahau somo, mambo yameharibika,
Tunatengeneza bomu, ambalo litalipuka,
Bomu litaja lipuka, kwa kukosa msimamo,
Watu wataja wehuka, wakijua yaliyomo,
Tubadilike haraka, rushwa iwe na kikomo,
Bado tunaweza fika, salama bila madhara
Uongozi ni kigezo, kile kinahitajika,
Kutujengea uwezo, tuweze tena sifika,
Kwa siasa na michezo, popote tutaja fika,
Turudishe tunu yetu, ili kuongoza vema.
Tusione vyaelea, tukasahau vyaundwa,
Mwalimu kapigania, wetu uhuru kulindwa
Malengo alifikia, maadui wakashindwa
Tanzania ilingaa , pande zote za dunia.
Tujichunguze makini, tujue nini tatizo,
Tuache huu uhuni, tunaleta machukizo,
Tatizo lipo jamani, tutatue kwa mawazo,
Tanzania tufanyaje, kuboresha yetu hali
Afrika na Ulimwengu, sifa tele tapakaa,
Wahindi nao wazungu, hakuna wa kuhadaa,
Jinsi ilivyo sifika, kwa uongozi thabiti.
Ilijulikana pote, Tanzania ya mwalimu,
Iliheshimu yoyote, aliyependa nidhamu,
Kaunda naye Obote, na asiye kichwa ngumu,
Tanzania ya mwalimu, nchi yenye msimamo
Umoja wetu wa ndani, kamwe hukutisika,
Utaifa akabuni, ukabila kufutika,
Akaipa uthamani, ikawa ya kutuka,
Ndivyo ilivyosifika Tanzania nchi yangu.
Akatua madaraka, ili kuipa uwezo,
Maendeleo haraka, demokrasia kigezo,
Yeye kote akawika, kwa hizo zake sifazo.
Mwalimu akangatuka, kutuachia mfumo
Nini kimetetereka, hata kufikia hapa,
Rushwa imetuchakaza, sasa tunatapatapa,
Viongozi wasowaza,kula fujo kama papa,
Nchi inaharibika, rushwa tele zimejaa.
Tamaa iso kipimo, ya mali na madaraka,
Viongozi waliomo, utajiri wa haraka,
Wamelisahau somo, mambo yameharibika,
Tunatengeneza bomu, ambalo litalipuka,
Bomu litaja lipuka, kwa kukosa msimamo,
Watu wataja wehuka, wakijua yaliyomo,
Tubadilike haraka, rushwa iwe na kikomo,
Bado tunaweza fika, salama bila madhara
Uongozi ni kigezo, kile kinahitajika,
Kutujengea uwezo, tuweze tena sifika,
Kwa siasa na michezo, popote tutaja fika,
Turudishe tunu yetu, ili kuongoza vema.
Tusione vyaelea, tukasahau vyaundwa,
Mwalimu kapigania, wetu uhuru kulindwa
Malengo alifikia, maadui wakashindwa
Tanzania ilingaa , pande zote za dunia.
Tujichunguze makini, tujue nini tatizo,
Tuache huu uhuni, tunaleta machukizo,
Tatizo lipo jamani, tutatue kwa mawazo,
Tanzania tufanyaje, kuboresha yetu hali